Binti aliyechukua uamuzi huu,,ungemsamehe?

Binti aliyechukua uamuzi huu,,ungemsamehe?

Himidini

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2013
Posts
5,534
Reaction score
4,190
^^
Huyu ni binti ambaye tumepotezana nae miaka mingi.Lakini milima haikutani,binadamu hukutana..Nilipomuuliza juu ya mwanaume waliyependana sana kuwa wanaendeleaje na familia yao? Nilijibiwa kwa machozi kwanza.Kisha akaanza kunisimulia,,
..
Anasema alimpenda sana rafiki yangu,tena sana.Lakini rafiki yangu aliamua kuondoka kijijini kwao na kwenda kutafuta maisha mjini.Kutokana na upendo mkubwa baina yao mawasiliano ya simu hayakutosha kukidhi ukamilifu baina yao.
Hivyo wote walikubaliana binti atoroke kwao amfuate mpenzi wake mjini.Tatizo lilianzia hapo,,NAULI.
...
Mwanaume akatuma nauli ambayo kusema kweli ilikuwa haitoshi.Kulikuwa na upungufu wa kiasi cha elfu 20. Mwanaume alilijua hilo na binti akamwambia asihofu shangazi yake ambae alijua kiasi gani,wawili hawa wanapendana atamuongezea nauli iliyobaki.Lakini haikuwa hivyo,,shangazi hakuwa nayo!
...
Binti akaona ili kujitoa kwa ampendae akaamua kumchuna kijana aliyemfuatilia kwa muda mrefu ili apate hiyo 20 elfu.Kijana akaona pesa haitoki hivi hivi,,lazima ampe penzi kwanza.Binti akawazaa akaona potelea mbali,akakubali.
Wakakutana gesti,,na pasipo bahati,watu waliojua uhusiano wa wawili hawa wakamjulisha yule kijana wa mjini.
Alipofuatilia akajua ni kweli,ukawa mwisho wa uhusiano wao.
Binti yupo kwao anajutia uamuzi wake,,mwaka wa pili sasa
...
Binti aliniomba msaada nimuombee msamaha kwa rafiki yangu huyo,aliepo mjini lakini kila jaribio langu limekwama.Wote wapo single.
Najiuliza swali,,je sadaka ya upendo wa aina hii,haistahili kusamehewa?
^^
 
ahahaaaa..aiseee hapo kijiji hakuna jamaa mwingine maana miaka 2 mmmmh
 
Inamaana siku nyingine akikwama mahali atautumia mwili kuvuka, na dunia hii ya magonjwa!!
Hapana, aendelee tu na maisha yake, au arudi kwa huyo aliyempa elf 20.
 
poverty.....

kijiji gani unatokea?

^^
The Boss
Si vema nitaje kijiji lakini kuhusu umasikini,,ni kweli binti anatoka familia masikini,,ni yatima asie na baba.
^^
 
Last edited by a moderator:
ahahaaaa..aiseee hapo kijiji hakuna jamaa mwingine maana miaka 2 mmmmh

^^
The same question anauliza,huyu rafiki yangu aliepo mjini.Kuwa ina maana hapo kijijini hakuna wanaume? Bt nachoweza kukiona ktk uso wake,,ni majuto ya kumkosa ampendae.
^^
 
pesa ndo kila ki2 ktk maisha ya sasa, had ktk mapenz money z very important, jamaa angekua na mkwanja wa kutosha angemtumia demu wake pesa za kutosha, swali kama nauli tu imekua shida mjini angemlishaje? kingekua chakula cha wenye...
 
Inamaana siku nyingine akikwama mahali atautumia mwili kuvuka, na dunia hii ya magonjwa!!
Hapana, aendelee tu na maisha yake, au arudi kwa huyo aliyempa elf 20.

^^
Maelezo ni kuwa yule aliyempa 20 elf,,alitoweka na hana mawasiliano tena.
^^
 
Kama alitoweka hapo mtihani zaidi. Mm naielewe hali ya kuishiwa na kuwa na kiu ya kitu lkn huna uwezo, ila uamuzi wa kutumia mwili unanifanya nimwogope, kwamba alisugua kichwa akaona hakuna njia nyingine? Akaona ni bora kumsaliti mtu ampendaye?
Halafu suala la kuwa walienda guest house mara moja na kukamatwa haliniingii, lazma itakua walifanya mahusiano kwa muda kiasi cha watu kugungua na kumtonya mpenzi wake, si mara moja ya kupata elf 20
 
Jamaa alimtumia shilingi elfu moja nini, maana naona itakuwa mbali sana na mjini kama jamaa alikuwa amejikakamua lakini bado ikahitajika 20 thousand du patakuwa mbali huko maybe Dar to KG ama Dar to Bukoba
 
Ikiwa jamaa alituma nauli na alijua fika haitamuwezesha mwenzie kufika alipo huo tayari ni mtego nachokiona hapo jamaa alipofika mjini tu akakutana na wapaka wanja na kutomuitaji mchumba wake tena naisi ni wazo la kumtema kikubwa coz alijua hataweza pata pesa ya kumfata pole dada huo ni mpango tu tafuta mwingine songa mbele mama.
 
NDIO! watu husema 'no confort in truth' yaan bora asngeambiwa.kile mke huliwa ila mme acjue akjua ndo mwanzo wa matatzo.kama yalvyomkuta dada angu.USHAUR,jamaa achukue mwingne ambae hajui profil yake na dada nae atafute mwngne ambae haljui profil lake.hapo ngoma droo na itabak kua historia ya mapenz 2
 
^^
Huyu ni binti ambaye tumepotezana nae miaka mingi.Lakini milima haikutani,binadamu hukutana..Nilipomuuliza juu ya mwanaume waliyependana sana kuwa wanaendeleaje na familia yao? Nilijibiwa kwa machozi kwanza.Kisha akaanza kunisimulia,,
..
Anasema alimpenda sana rafiki yangu,tena sana.Lakini rafiki yangu aliamua kuondoka kijijini kwao na kwenda kutafuta maisha mjini.Kutokana na upendo mkubwa baina yao mawasiliano ya simu hayakutosha kukidhi ukamilifu baina yao.
Hivyo wote walikubaliana binti atoroke kwao amfuate mpenzi wake mjini.Tatizo lilianzia hapo,,NAULI.
...
Mwanaume akatuma nauli ambayo kusema kweli ilikuwa haitoshi.Kulikuwa na upungufu wa kiasi cha elfu 20. Mwanaume alilijua hilo na binti akamwambia asihofu shangazi yake ambae alijua kiasi gani,wawili hawa wanapendana atamuongezea nauli iliyobaki.Lakini haikuwa hivyo,,shangazi hakuwa nayo!
...
Binti akaona ili kujitoa kwa ampendae akaamua kumchuna kijana aliyemfuatilia kwa muda mrefu ili apate hiyo 20 elfu.Kijana akaona pesa haitoki hivi hivi,,lazima ampe penzi kwanza.Binti akawazaa akaona potelea mbali,akakubali.
Wakakutana gesti,,na pasipo bahati,watu waliojua uhusiano wa wawili hawa wakamjulisha yule kijana wa mjini.
Alipofuatilia akajua ni kweli,ukawa mwisho wa uhusiano wao.
Binti yupo kwao anajutia uamuzi wake,,mwaka wa pili sasa
...
Binti aliniomba msaada nimuombee msamaha kwa rafiki yangu huyo,aliepo mjini lakini kila jaribio langu limekwama.Wote wapo single.
Najiuliza swali,,je sadaka ya upendo wa aina hii,haistahili kusamehewa?
^^

Hivi! Ni sahihi nikikwambia hiyo task uliyonayo ni kubeba roba la misumari?
Unajua Himidini sisi binadamu tunatofautiana mitazamo, mimi kama mimi ningemsamee huyo binti, lakin kuna watu bora uwakosee lolote ktk mapenz lakin si kutoa utu wako. Nawezasema jamaa yuko sahihi kwa hilo! Coz ikiwa hana excuse kwa hilo hata akimsamee hatoweza kuishi nae kwa amani na uaminifu, baya zaidi iyo ishu imeshasambaa.
Just do ur own bussiness otherwise jamaa atakuchkulia poyoyo kwa ku-support upuuzi wa huyo x wake!
 
Mwanaume makini na jasiri hawezi kwenda kumuombea msamaa kwa upuuzi alioufanya uyo bint. Kama me ukinifuata razima Nikuzingue
 
Umaskini mbaya sana,unauza utu wako hivi hivi.Na haya hutokea kweli
 
Kha! Kama nauli tu ya kumleta dada wa watu mjini imemshinda ndo angeweza kumlisha!?....au ndo ubahili! Ila huyo dada nae hafai!

Sent from my BlackBerry using JamiiForums
 
^^
The same question anauliza,huyu rafiki yangu aliepo mjini.Kuwa ina maana hapo kijijini hakuna wanaume? Bt nachoweza kukiona ktk uso wake,,ni majuto ya kumkosa ampendae.
^^

niunganishe nao niwapatanishe maana hisia za penzi lao bado zimo kwenye mioyo yao
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom