Bilioni 79 kwa mradi wa miaka 5

rodrick alexander

JF-Expert Member
Feb 12, 2012
14,923
19,614
Juzi juzi rais jakaya kikwete amezindua mradi mkubwa wa maji huko mbeya mradi huo ambao umegharimu shilingi bilioni 79 utadumu kwa muda wa mpaka mwaka 2017 ambapo inategemewa hadi kufikia muda huo vyanzo vingine vya maji vitakuwa vimepatikana.source gazeti la mwananchi
swali la kujiuliza hivi kwanini tuwekeze pesa nyingi kiasi hicho kwa mradi ambao life span yake ni miaka 5 .je ni uvivu wa kufikiri,kutafuta sapoti ya kisiasa au tu ni ulimbukeni.kwa pesa kiasi hicho tulitakiwa tuwekeze kwenye mradi ambao utachukua angalau si chini ya miaka 40.kuna baadhi ya maeneo yangeweza kuvutiwa maji toka ziwa victoria,nyasa na sehemu nyinginezo ambazo mradi huo ungekuwa wa kudumu.ni kichekesho kujisifu kwa miradi kama hiyo ambayo kwa upande mwingine ni ufujaji wa pesa. Hatutakiwi tufanye miradi ya zimamoto
au ni kwa sababu waziri wa maji wa aliyekuwepo alitokea huko mbeya ndio akaona ajipendelee?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom