Isabel dos Santos,
bintiye Rais wa Angola Jose Eduardo Dos Santos, , amekuwa mwanamke wa
kwa kwanza wa Afrika kuwa Bilionea .
Hii ni kwa mujibu wa jarida la kiuchumi nchini Marekani la Forbes.
Bi Isabel mwenye umri wa miaka 40 anamilikihisa katika makampuni kadhaa
nchini Portugal, ikiwemo kampuni moja ya televisheni na benki moja
nchini Angola.
Hisa hizo zote zimefikisha mali anayomiliki kuwa na thamani ya mabilioni
na hivyo kumuweka kwenye orodha ya watu wenginewanaomiliki mabilioni
barani Afrika.
Kulingana na jarida hilo ambalo huandika zaidi kuhusu watu matajiri
duniani, biashara yake ya kwanza ilikuwa ya mkahawa mjini Luanda
ulioitwa, Miami Beach.
Watu wengi nchini Angola , nchi yenye utajiri mkubwa, wanaishi kwa
kipato cha chini ya dola mbili kwa siku.
Angola inajitahidi kukabiliana na athari za vita vya wenywe kwa wenyewe
vilivyodumu miaka 27, baada ya nchi hiyo kujipatia uhuru wake kutoka kwa
Portugal.
Alisomea uhandisi katika chuo kikuu cha King's College mjini London,
ambako alilelewana mamake.
Vita vya Angola vilikamilika mwaka 2002 na nchi hiyo imeweza kuibuka
kama mzalishaji mkubwa wa mafuta barani Afrika,pamoja na kuwa uchumi
wake unakuwa kwa kasi .
Familia ya Rais Jose Eduardo Dos Santos ambaye amekua mamlakani kwa
miaka 33 , inadhibiti sehemu kubwa ya uchumi wa nchi hiyo.
Duru zinasema kuwa Bi dos Santosa hapendi sana kujionyesha hadharani
licha ya kufanikiwa sana kibiashara.
Tangu mwaka kuanza biashara yake ya mkahawa, mjini, Luanda, mwaka 1997,
amekuwa mfanyabiashara mwenye ushawishi mkubwa nchini Angola na
Portugal.
Akiwa na asilimia 28.8 ya hisa katika kampuniya Zon, yeye ni mwanachama
wa bodi ya kampuni hiyo na mmiliki mkubwa wa hisa zake , kulingana na
Forbes.