sirluta
JF-Expert Member
- Nov 28, 2012
- 6,324
- 2,494
Ni wiki hii tu kumefanyika mabadiliko ya Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, leo imeripotiwa kuna bilion 100 zimeyeyuka BOT.
Kuna gazeti limeripoti ngoja litafutwe.
========
Bilioni 100/- zayeyuka Hazina
SIKU moja baada ya kutimuliwa kazi aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Servacius Likwelile, Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) imebaini ufisadi wa Sh. bilioni 100.5 ambao unaihusisha Hazina na Wizara ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Ufisadi huo ulibainika mjini hapa jana kwenye kikao cha kamati hiyo iliyokuwa ikipitia hesabu za TAMISEMI kwa mwaka wa fedha 2014/15 uliofanyika wakati ofisi hiyo ikiwa chini ya Waziri Mkuu.
Akipitia kitabu cha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) juu ya hesabu za wizara hiyo, Mbunge wa Sikonge, Joseph Kakunda (CCM), alisema vitabu vya hesabu za TAMISEMI vinaonyesha kwa mwaka huo wa fedha, ofisi hiyo ilipewa Sh. bilioni 286 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kwamba asilimia 99.9 ya fedha hizo zilitumika.
Chanzo: Nipashe
Kuna gazeti limeripoti ngoja litafutwe.
========
Bilioni 100/- zayeyuka Hazina
SIKU moja baada ya kutimuliwa kazi aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Servacius Likwelile, Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) imebaini ufisadi wa Sh. bilioni 100.5 ambao unaihusisha Hazina na Wizara ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Ufisadi huo ulibainika mjini hapa jana kwenye kikao cha kamati hiyo iliyokuwa ikipitia hesabu za TAMISEMI kwa mwaka wa fedha 2014/15 uliofanyika wakati ofisi hiyo ikiwa chini ya Waziri Mkuu.
Akipitia kitabu cha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) juu ya hesabu za wizara hiyo, Mbunge wa Sikonge, Joseph Kakunda (CCM), alisema vitabu vya hesabu za TAMISEMI vinaonyesha kwa mwaka huo wa fedha, ofisi hiyo ilipewa Sh. bilioni 286 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kwamba asilimia 99.9 ya fedha hizo zilitumika.
Chanzo: Nipashe