nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Thursday, May 5, 2011,
Makala na Uchambuzi, Rai
http://www.newhabari.com/2011/05/05/bila-mapinduzi-z’bar-ingekuwa-kama-a-kusini/#respond
Na Siyovelwa Hussein
HIVI karibuni nilizungumzia suala la kuutazama upya uhuru wa nchi za Afrika.
Miongoni mwa mambo niliyoyasema ni lile la ukweli kwamba hakuna nchi ya Kiafrika iliyopata uhuru wake kwa juhudi zake yenyewe.
Nchi zote zilipata uhuru kwa utashi wa wakoloni. Mtetereko wa uchumi uliyaandama mataifa ya wakoloni baada ya Vita Kuu ya Pili ndio uliowalazimisha kubuni mtindo mpya wa kuzinyima nchi za Kiafrika bila kuzitawala moja kwa moja.
Miaka ya mwanzo ya 1960 ikashuhudia nchi nyingi zikijipatia kile kilichoitwa uhuru japokuwa karibia viongozi wote waliopatiwa uhuru huo walikuwa mawakala wa wakoloni.
Hata hivyo kwa vile uhuru huo ulitolewa kwa hila na kwa maslahi ya wakoloni, aina ya uhuru huu ilitofautiana kutoka sehemu moja hadi nyingine. Wakati katika nchi nyingine wakoloni walilazimika kuwatengeneza watu wa kuwaachia madaraka, popote palipokuwa na matabaka miongoni mwa wananchi waliokabidhiwa uhuru huo walikuwa lile tabaka bora.
Katika baadhi ya nchi za Kiafrika kulikuwa na aina mbili ya ukoloni kwa wakati mmoja. Kulikuwapo mkoloni mkuu anayetambulika lakini hata miongoni mwa watawaliwa nako kulikuwa na aina nyingine ya ukoloni.
Matabaka ya mabwana na watwana. Hali hii ambayo ndiyo iliyokuwapo katika Visiwa vya Zanzibar nchi za Afrika ya Kusini kama vile, Namibia na Zimbabwe ambako kundi la walowezi chini ya Cecil Rhodes lilijitwalia mamlaka ya kuitawala nchi baada ya Wakoloni wa Kiingereza. Nchini Afrika Kusini mpaka mwaka 1910 nchi hiyo ilikuwa chini ya ukoloni wa Kiingereza lakini walikuwapo pia makaburu ambao pamoja na kujiita Waafrika ya Kusini lakini hawakuwahi kuwaona watu Weusi wenye asili ya chini hiyo kuwa ni ndugu zao.
Kama ilivyokuwa kwa Waarabu wa Zanzibar, kilichowafanya makaburu kuendesha harakati za kumwondoa ukoloni wa Kiingereza haikuwa kutaka uhuru wa nchi utakaomaanisha haki na usawa wa kiraia isipokuwa nafasi ya wao kuwatawala wenyeji wa Afrika Kusini. Mara baada ya Waingereza kujiondoa nchini humo tukashuhudia miaka takriban 80 ya ubaguzi, ukandamizaji, ubabe na unyanyasaji wa makaburu kwa raia wa asili wa Afrika Kusini.
Zimbabwe nako mambo yalikuwa yale yale. Baada ya Waingereza kujiondoa utawala wa nchi ukabaki chini ya Ian Smith na huo ukawa mwanzo wa utawala wa ukandamizaji na ubaguzi kuliko ilivyokuwa wakati wa ukoloni wa mwingereza.
Kwa bahati mbaya haya ndiyo yaliyotaka kutokea katika Visiwa vya Zanzibar.
Kuanzia mwaka 1890, Zanzibar iliyokuwa chini ya Sultan Khalifa bin Harub iliwekwa chini ya uangalizi wa Waingereza.
Sultan akaendelea na utawala wake lakini mambo yote ya kiserikali yakawa chini ya Waingereza mpaka katika miaka ya katikati ya 1950 ambapo harakati za kisiasa zilianza visiwani humo.
Hata hivyo, katikati ya mgwanyiko uliojengwa na Waingereza chini ya mwamvuli wa Sultan Khalifa aliyefariki dunia mwaka 1960, harakati nyingi za kisiasa ambazo baadae ziligeuka kuwa vyama vya siasa zilifuata makundi ya kiasili.
Zilikuwapo harakati za Kiarabu ambazo zilikumbatiwa na Sultan na malengo yake makubwa yakiwa kuendeleza utawala wa Kisultan baada ya kuondoka Waingereza.
Kulikuwapo harakati za kihindi ambazo zililenga zaidi ustawi wao wa kibishara pamoja na harakati za makabila mengine kama Waafrika na Washirazi.
Mwaka 1957 na Januari 1961, Waingereza waliendesha uchaguzi wa kisiasa katika Zanzibar huku wao wenyewe wakionekana wazi kukipendelea chama kilichokuwa na uhusiano na Sultan.
Kwa bahati mbaya Sultan Khalifa alikuwa swahiba mkubwa wa Waingereza. Pamoja na ukweli kwamba chama cha ASP kilikuwa na wapiga kura wengi zaidi lakini katika chaguzi zote hizo mbili mshindi alishindwa kupatikana kutokana na hila za wasimamizi wa uchaguzi ambao ni Waingereza. Kila walipokaribia kushinda uchaguzi uliharibiwa na kutakiwa kurudiwa ambapo katika muda wa kusubiri uchaguzi mwingine mambo mengi yalitokea ikiwa ni pamoja na baadhi wa watu kushawishiwa kukihama chama cha ASP na kuhamia vyama vingine au kuunda vyama vipya. Moja ya vyama hivyo ni kama vile ZPPP cha Mohamed Shamte ambacho kilijitoa katika ASP kwa kisingizio kwamba ASP inakumbatia zaidi Uafrika wakati kinajiita ni cha Waafrika na Washirazi.
Baada ya chaguzi hizo mbili kushindwa kutoa mshindi Waingereza waliandaa uchaguzi mwingine Juni 1961, ambapo kwa hila zile zile ZPPP na ZNP ziliunganisha nguvu zao na kujizolea viti 13 dhidi ya viti 10 vya ASP na kupata haki ya kuunda serikali ya ndani chini ya waziri mkuu Mohamed Shamte.
Ikumbukwe kwamba pamoja na Shamte kuwa Mwafrika kutokea Pemba lakini alikuwa akiukumbatia sana Uarabu na kwa hila akawa akitumikia maslahi ya Waarabu. Kwa hila ZNP wakamwachia uwaziri mkuu ili kuonekana hawana ubaguzi huku wenyewe wakiendesha mambo kwa mlango wa nyuma.
Desemba 10, 1963 Waingereza walitoa uhuru kamili kwa visiwa vya Zanzibar chini ya Sultan Jamshid bin Abdulah na Serikali ya Waziri Mkuu Mohamed Shamte. Huu ukawa mwanzo wa ukoloni mwingine kwa waafrika na washirazi waliokuwa wengi katika visiwa vya Zanzibar. Uhuru kama ule wa Afrika Kusini, Zimbawe na Namibia ukatolewa Zanzibar.
Wakati Afrika Kusini waliopatiwa uhuru walikuwa makaburu na hivyo kujizolea haki ya kuwatawala Waafrika kwa miongo kadhaa visiwani Zanzibar uhuru ukaachwa chini ya mikono ya Sultan.
Siku sita tu baada ya kupatiwa uhuru kamili Desemba 16, 1964, Shamte akapewa nafasi ya kuhutubia katika Umoja wa Mataifa na punde akapatiwa uanachama na Kenya.
Kwa vyovyote uhuru huu na hatua zilizofuatia zilikuwa zimepangwa na Waingereza. Ndiyo maana hata hatua za kupata uanachama katika Umoja wa Mataifa zilikwenda haraka haraka.
Hata hivyo, kwa wananchi wengi wa Zanzibar uhuru huu haukuwa na maslahi kwao.
Waliuona kama jinamizi jipya baada ya kuondoka lile la Waingereza. Ndipo mipango ya mapinduzi ilipopangwa chini ya mwasisi wake Kasim Hanga, Saleh Sadala, na Abdulaziz Twala.
Kwa sababu yanayosemwa juu ya mapinduzi ni mengi hatuwezi kuandika kwa uhakika walipata msaada wapi na wapi lakini Januari 12, mwaka 1964 walifanikiwa kufanya mapinduzi na kuingoa si tu Serikali ya Mohamed Shamte lakini hata utawala wa Sultan Jamshid.
Pengine cha kujiuliza hapa ni kwamba kama kweli Sultan hakuwa na tatizo na Waafrika ilikuwaje yeye awe wa kwanza kuikimbia nchi wakati waliopinduliwa walikuwa Serikali ya Shamte. Na wala hakuna hata mtu mmoja katika familia ya sultan au mpambe wake aliyeshambuliwa au kukamatwa.
Kuonyesha urafiki uliokuwapo baina ya Waingereza na usultan, mara baada ya kupinduliwa, wakati viongozi wa Serikali akiwamo Shamte mwenyewe walikamatwa baada ya kujisalimisha.
Sultan Jamshid alipewa ulinzi na Waingereza na kupelekwa Dar es Salaam ambako alipatiwa usafiri kwenda Uingereza.
Mara baada ya mapinduzi Uingereza hawakuipenda Serikali mpya kwa vile hawakuwa na imani nayo.
Tangu awali hawakutaka ASP ishinde katika chaguzi na ilipoingia kwa mapinduzi juhudi zilizofuatia zilikuwa kuibana Serikali mpya hasa baada ya kuonekana imejumuisha makomredi wa chama cha UMMA ambao wao walikiona kilichojaa wanapanduzi wenye mirengo ya Kimaxist na Kikomunisti.
Kwa mtazamo wao wakaona Zanzibar chini ya Serikali ya Mapinduzi itageuka kuwa Cuba ya Afrika, na hivyo ikawabidi wafanye mbinu zozote kutoiachia kuwa huru baada ya kushindwa majaribio ya kumrejesha Sultan.
Pengine hizi zikawa sababu za mwanzo za muungano wa Tangayika na Zanzibar.
Kinyume cha hapo ni lazima tuifikirie ambavyo ingekuwa hali za Zanzibar kama yasingetokea mapinduzi.
Kwanza pasingetokea muungano kwa vile Zanzibar ingeendela kuwa chini ya utawala wa Sultan, kwa baraka za Uingereza na msaada wa Oman.
Ikumbukwe kwamba Masultan hawa asili yao ilikuwa Oman ambapo yule kwanza Sayyid Said alikuwa akitawala Oman na Zanzibar. Basi ingekuwaje hali ya Waafrika Weusi na hata makabila mengine kama Washirazi na Wapemba kama Zanzibar ingeendelea kuwa chini ya Sultan. Kwa vyovyote ingekuwa kama Sahara Magharibi ambayo mpaka leo inatawaliwa na Moroco. Ingekuwa kama miaka 80 ya utawala wa makaburu pale Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia. Si kila uhuru ulijali maslahi ya walio wengi. Bado nasisitiza kuungalia upya uhuru wa Afrika.
uhalisi@yahoo.co.uk
0787013385/0655013385
Makala na Uchambuzi, Rai
http://www.newhabari.com/2011/05/05/bila-mapinduzi-z’bar-ingekuwa-kama-a-kusini/#respond
Na Siyovelwa Hussein
HIVI karibuni nilizungumzia suala la kuutazama upya uhuru wa nchi za Afrika.
Miongoni mwa mambo niliyoyasema ni lile la ukweli kwamba hakuna nchi ya Kiafrika iliyopata uhuru wake kwa juhudi zake yenyewe.
Nchi zote zilipata uhuru kwa utashi wa wakoloni. Mtetereko wa uchumi uliyaandama mataifa ya wakoloni baada ya Vita Kuu ya Pili ndio uliowalazimisha kubuni mtindo mpya wa kuzinyima nchi za Kiafrika bila kuzitawala moja kwa moja.
Miaka ya mwanzo ya 1960 ikashuhudia nchi nyingi zikijipatia kile kilichoitwa uhuru japokuwa karibia viongozi wote waliopatiwa uhuru huo walikuwa mawakala wa wakoloni.
Hata hivyo kwa vile uhuru huo ulitolewa kwa hila na kwa maslahi ya wakoloni, aina ya uhuru huu ilitofautiana kutoka sehemu moja hadi nyingine. Wakati katika nchi nyingine wakoloni walilazimika kuwatengeneza watu wa kuwaachia madaraka, popote palipokuwa na matabaka miongoni mwa wananchi waliokabidhiwa uhuru huo walikuwa lile tabaka bora.
Katika baadhi ya nchi za Kiafrika kulikuwa na aina mbili ya ukoloni kwa wakati mmoja. Kulikuwapo mkoloni mkuu anayetambulika lakini hata miongoni mwa watawaliwa nako kulikuwa na aina nyingine ya ukoloni.
Matabaka ya mabwana na watwana. Hali hii ambayo ndiyo iliyokuwapo katika Visiwa vya Zanzibar nchi za Afrika ya Kusini kama vile, Namibia na Zimbabwe ambako kundi la walowezi chini ya Cecil Rhodes lilijitwalia mamlaka ya kuitawala nchi baada ya Wakoloni wa Kiingereza. Nchini Afrika Kusini mpaka mwaka 1910 nchi hiyo ilikuwa chini ya ukoloni wa Kiingereza lakini walikuwapo pia makaburu ambao pamoja na kujiita Waafrika ya Kusini lakini hawakuwahi kuwaona watu Weusi wenye asili ya chini hiyo kuwa ni ndugu zao.
Kama ilivyokuwa kwa Waarabu wa Zanzibar, kilichowafanya makaburu kuendesha harakati za kumwondoa ukoloni wa Kiingereza haikuwa kutaka uhuru wa nchi utakaomaanisha haki na usawa wa kiraia isipokuwa nafasi ya wao kuwatawala wenyeji wa Afrika Kusini. Mara baada ya Waingereza kujiondoa nchini humo tukashuhudia miaka takriban 80 ya ubaguzi, ukandamizaji, ubabe na unyanyasaji wa makaburu kwa raia wa asili wa Afrika Kusini.
Zimbabwe nako mambo yalikuwa yale yale. Baada ya Waingereza kujiondoa utawala wa nchi ukabaki chini ya Ian Smith na huo ukawa mwanzo wa utawala wa ukandamizaji na ubaguzi kuliko ilivyokuwa wakati wa ukoloni wa mwingereza.
Kwa bahati mbaya haya ndiyo yaliyotaka kutokea katika Visiwa vya Zanzibar.
Kuanzia mwaka 1890, Zanzibar iliyokuwa chini ya Sultan Khalifa bin Harub iliwekwa chini ya uangalizi wa Waingereza.
Sultan akaendelea na utawala wake lakini mambo yote ya kiserikali yakawa chini ya Waingereza mpaka katika miaka ya katikati ya 1950 ambapo harakati za kisiasa zilianza visiwani humo.
Hata hivyo, katikati ya mgwanyiko uliojengwa na Waingereza chini ya mwamvuli wa Sultan Khalifa aliyefariki dunia mwaka 1960, harakati nyingi za kisiasa ambazo baadae ziligeuka kuwa vyama vya siasa zilifuata makundi ya kiasili.
Zilikuwapo harakati za Kiarabu ambazo zilikumbatiwa na Sultan na malengo yake makubwa yakiwa kuendeleza utawala wa Kisultan baada ya kuondoka Waingereza.
Kulikuwapo harakati za kihindi ambazo zililenga zaidi ustawi wao wa kibishara pamoja na harakati za makabila mengine kama Waafrika na Washirazi.
Mwaka 1957 na Januari 1961, Waingereza waliendesha uchaguzi wa kisiasa katika Zanzibar huku wao wenyewe wakionekana wazi kukipendelea chama kilichokuwa na uhusiano na Sultan.
Kwa bahati mbaya Sultan Khalifa alikuwa swahiba mkubwa wa Waingereza. Pamoja na ukweli kwamba chama cha ASP kilikuwa na wapiga kura wengi zaidi lakini katika chaguzi zote hizo mbili mshindi alishindwa kupatikana kutokana na hila za wasimamizi wa uchaguzi ambao ni Waingereza. Kila walipokaribia kushinda uchaguzi uliharibiwa na kutakiwa kurudiwa ambapo katika muda wa kusubiri uchaguzi mwingine mambo mengi yalitokea ikiwa ni pamoja na baadhi wa watu kushawishiwa kukihama chama cha ASP na kuhamia vyama vingine au kuunda vyama vipya. Moja ya vyama hivyo ni kama vile ZPPP cha Mohamed Shamte ambacho kilijitoa katika ASP kwa kisingizio kwamba ASP inakumbatia zaidi Uafrika wakati kinajiita ni cha Waafrika na Washirazi.
Baada ya chaguzi hizo mbili kushindwa kutoa mshindi Waingereza waliandaa uchaguzi mwingine Juni 1961, ambapo kwa hila zile zile ZPPP na ZNP ziliunganisha nguvu zao na kujizolea viti 13 dhidi ya viti 10 vya ASP na kupata haki ya kuunda serikali ya ndani chini ya waziri mkuu Mohamed Shamte.
Ikumbukwe kwamba pamoja na Shamte kuwa Mwafrika kutokea Pemba lakini alikuwa akiukumbatia sana Uarabu na kwa hila akawa akitumikia maslahi ya Waarabu. Kwa hila ZNP wakamwachia uwaziri mkuu ili kuonekana hawana ubaguzi huku wenyewe wakiendesha mambo kwa mlango wa nyuma.
Desemba 10, 1963 Waingereza walitoa uhuru kamili kwa visiwa vya Zanzibar chini ya Sultan Jamshid bin Abdulah na Serikali ya Waziri Mkuu Mohamed Shamte. Huu ukawa mwanzo wa ukoloni mwingine kwa waafrika na washirazi waliokuwa wengi katika visiwa vya Zanzibar. Uhuru kama ule wa Afrika Kusini, Zimbawe na Namibia ukatolewa Zanzibar.
Wakati Afrika Kusini waliopatiwa uhuru walikuwa makaburu na hivyo kujizolea haki ya kuwatawala Waafrika kwa miongo kadhaa visiwani Zanzibar uhuru ukaachwa chini ya mikono ya Sultan.
Siku sita tu baada ya kupatiwa uhuru kamili Desemba 16, 1964, Shamte akapewa nafasi ya kuhutubia katika Umoja wa Mataifa na punde akapatiwa uanachama na Kenya.
Kwa vyovyote uhuru huu na hatua zilizofuatia zilikuwa zimepangwa na Waingereza. Ndiyo maana hata hatua za kupata uanachama katika Umoja wa Mataifa zilikwenda haraka haraka.
Hata hivyo, kwa wananchi wengi wa Zanzibar uhuru huu haukuwa na maslahi kwao.
Waliuona kama jinamizi jipya baada ya kuondoka lile la Waingereza. Ndipo mipango ya mapinduzi ilipopangwa chini ya mwasisi wake Kasim Hanga, Saleh Sadala, na Abdulaziz Twala.
Kwa sababu yanayosemwa juu ya mapinduzi ni mengi hatuwezi kuandika kwa uhakika walipata msaada wapi na wapi lakini Januari 12, mwaka 1964 walifanikiwa kufanya mapinduzi na kuingoa si tu Serikali ya Mohamed Shamte lakini hata utawala wa Sultan Jamshid.
Pengine cha kujiuliza hapa ni kwamba kama kweli Sultan hakuwa na tatizo na Waafrika ilikuwaje yeye awe wa kwanza kuikimbia nchi wakati waliopinduliwa walikuwa Serikali ya Shamte. Na wala hakuna hata mtu mmoja katika familia ya sultan au mpambe wake aliyeshambuliwa au kukamatwa.
Kuonyesha urafiki uliokuwapo baina ya Waingereza na usultan, mara baada ya kupinduliwa, wakati viongozi wa Serikali akiwamo Shamte mwenyewe walikamatwa baada ya kujisalimisha.
Sultan Jamshid alipewa ulinzi na Waingereza na kupelekwa Dar es Salaam ambako alipatiwa usafiri kwenda Uingereza.
Mara baada ya mapinduzi Uingereza hawakuipenda Serikali mpya kwa vile hawakuwa na imani nayo.
Tangu awali hawakutaka ASP ishinde katika chaguzi na ilipoingia kwa mapinduzi juhudi zilizofuatia zilikuwa kuibana Serikali mpya hasa baada ya kuonekana imejumuisha makomredi wa chama cha UMMA ambao wao walikiona kilichojaa wanapanduzi wenye mirengo ya Kimaxist na Kikomunisti.
Kwa mtazamo wao wakaona Zanzibar chini ya Serikali ya Mapinduzi itageuka kuwa Cuba ya Afrika, na hivyo ikawabidi wafanye mbinu zozote kutoiachia kuwa huru baada ya kushindwa majaribio ya kumrejesha Sultan.
Pengine hizi zikawa sababu za mwanzo za muungano wa Tangayika na Zanzibar.
Kinyume cha hapo ni lazima tuifikirie ambavyo ingekuwa hali za Zanzibar kama yasingetokea mapinduzi.
Kwanza pasingetokea muungano kwa vile Zanzibar ingeendela kuwa chini ya utawala wa Sultan, kwa baraka za Uingereza na msaada wa Oman.
Ikumbukwe kwamba Masultan hawa asili yao ilikuwa Oman ambapo yule kwanza Sayyid Said alikuwa akitawala Oman na Zanzibar. Basi ingekuwaje hali ya Waafrika Weusi na hata makabila mengine kama Washirazi na Wapemba kama Zanzibar ingeendelea kuwa chini ya Sultan. Kwa vyovyote ingekuwa kama Sahara Magharibi ambayo mpaka leo inatawaliwa na Moroco. Ingekuwa kama miaka 80 ya utawala wa makaburu pale Afrika Kusini, Zimbabwe na Namibia. Si kila uhuru ulijali maslahi ya walio wengi. Bado nasisitiza kuungalia upya uhuru wa Afrika.
uhalisi@yahoo.co.uk
0787013385/0655013385