Bil 25.4/- kukarabati barabara Pwani

Bil 25.4/- kukarabati barabara Pwani

diana chumbikino

JF-Expert Member
Joined
May 29, 2018
Posts
428
Reaction score
368
671660205270bd572cd3a4e97896b3dd.jpg


WAKALA wa Barabara (TANROADS) mkoani Pwani unatarajia kutumia Sh bilioni 25.4 kwa ajili ya kufanya matengenezo ya barabara zake mbalimbali. Hayo yamesemwa mjini Kibaha na mhandisi wa wakala huo Zuhura Aman wakati wa kikao cha bodi ya barabara cha mkoani humo na kusema fedha hizo ni za bajeti ya mwaka 2018/2019.

Amesema hadi kukia Septemba 2018 zimepokelewa Sh milioni 958.7 kwa ajili ya matengenezo ya barabara hizo. "Katika kipindi hicho shilingi bilioni mbili zimetumika kufanya matengenezo mbalimbali kwenye barabara kuu," amesema. Alisema kazi ya matengenezo ilichelewa kuanza kutokana na taratibu za manunuzi na uhakiki wa mikataba ambayo huchukua muda mrefu kukamilika, hasa mikataba inayohakikiwa kwa mwanasheria mkuu wa serikali.

"Mkoa umepanga kufanya miradi ya maendeleo ya barabara zenye urefu wa kilometa 32.5 zenye thamani ya Shilingi bilioni 2.3," alisema. Aidha alisema kwenye miradi hiyo ya maendeleo Sh bilioni 1.3 ni bajeti ambapo Sh milioni 969 ni kutoka mfuko wa barabara. Vilevile bilioni 7.5 ni kutoka serikali zitafanya ukarabati kwa kiwango cha changarawe na udongo. Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Evarist Ndikilo alisema ili kuboresha barabara za mkoa huo watendaji wanapaswa kuwa waadilifu. Ndikilo alisema kutokana na mkoa kuwa na viwanda vingi uboreshaji wa miundombinu ya barabara utasaidia kuinua uchumi wa wananchi na taifa
 
Wanaweka molamu baada ya mwaka mmoja wanaomba tena hela warekebishe hyo hyo barabara ....sasa mi najiuliza kwanini wasiweke lami moja kwa moja

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pwani ilikuwa imelala kakini sasa ni tishio, safi sana!
 
Mkoa wa Pwani upo nyuma sanaa ktk upande wa barabara makao yao makuu Kibaha hawana hata barabara ya km2 ya lami ni vumbi na barabara zenye mashimo mwanzo mwisho, mi nashaur Kibaha ingerudishwa dar maana Pwani hamna jipya, hakuna sehem unaweza kumpeleka mtu na kumuonyesha kuwa hapa ndo mjini hata Wilaya yoyote ya mkoa tofauti na Pwani inaishinda Pwani. Inasikitisha sanaa watu wamejitahidi kujenga soko la Loliondo lkn mvua ikinyesha hapaingiliki ni tope mwanzo mwisho too shame. Mkiulizwa barabara ya lami mnaonyesha ya kwenda Morogoro, jengeni za kwenu za ndani ya kwenda bagamoyo toka kibaha imewashinda ya kwenda kisarawe toka kibaha imewashinda too shame za mitaani kibaha ndo makorongo unaweza hata kufugia samaki jifunzeni hata kutoka kwa majirani wa ubungo tu maana tukisema mkoa hamuwezi lbd mkajifunze wilayani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkoa wa Pwani upo nyuma sanaa ktk upande wa barabara makao yao makuu Kibaha hawana hata barabara ya km2 ya lami ni vumbi na barabara zenye mashimo mwanzo mwisho, mi nashaur Kibaha ingerudishwa dar maana Pwani hamna jipya, hakuna sehem unaweza kumpeleka mtu na kumuonyesha kuwa hapa ndo mjini hata Wilaya yoyote ya mkoa tofauti na Pwani inaishinda Pwani. Inasikitisha sanaa watu wamejitahidi kujenga soko la Loliondo lkn mvua ikinyesha hapaingiliki ni tope mwanzo mwisho too shame. Mkiulizwa barabara ya lami mnaonyesha ya kwenda Morogoro, jengeni za kwenu za ndani ya kwenda bagamoyo toka kibaha imewashinda ya kwenda kisarawe toka kibaha imewashinda too shame za mitaani kibaha ndo makorongo unaweza hata kufugia samaki jifunzeni hata kutoka kwa majirani wa ubungo tu maana tukisema mkoa hamuwezi lbd mkajifunze wilayani.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hua nashindwa kuelewa pale mailimoja mjini ni wapi maana nikifananisha hata na handeni ukiuliza mjini ni wapi unaelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaan kiukwel m mwenyewe nmeshindwa kuelewa kwamba kibaha mjini Ndio wapi kila nkipitaga coz panaonekana Kam wilayani ilihali ndiyo makao makuu ya mkoa wa pwani wakat mwingne nlijisemelea si Bora ata Bagamoyo pangekuwa makao makuu coz binafsi cjapaelewa kibaha mji ulio karibu na dar(umbali wa km 35) Af bado Duuh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ama kweli nchi kubwa labda kote kupo hoi lakini hiki kipande cha kutoka nyakanazi kuelekea Burundi, Rwanda, Congo na Uganda Kweli kina tuhusu?

Bandari ya dar inayo tija kweli kwa barabara isiyokuwapo kama hii iliyotelekezwa miaka yote?
 
Back
Top Bottom