mfuga kuku
JF-Expert Member
- Jul 14, 2014
- 750
- 544
Habari wanabodi, napenda kutumia fursa hii kuwashukuru Sana, sana tena sana! nilianzia na kuomba jina la biashara kwa ajili ya kuanzisha biashara ya stationery ambayo kwa kiasi kikubwa idea nimeivuna kutoka jukwaa hili, biashara yangu sasa inaenda vizuri miezi sita ya mwanzo nilitamani kughairi biashara hii maana mauzo kwa siku yalikuwa hayazidi Tsh 3000/=( Alfu Tatu) lkn sasa namshukuru Mungu kuna Muda nauza hadi LAKI TANO kwa siku kipindi kile cha November na December, na January. siku zingine za kawaida nauza Laki moja adi Mbili.
Kwa sasa nimeongeza na biashara za Miamala ya simu, pamoja na Vitafunwa kama Korosho za kuoka na zile mbichi.
Jana nimepata wazo la kuweka na spare parts za mashine za photocopy, naomba kama kuna mdau ana fahamu chimbo la bidhaa hizi kwa karikoo anijulishe, aweke hapa ili na wengine pia waone.
Napokea maswali kwa mwenye kuhitaji kuanza biashara ya stationery ili walau nimpatie A, B, C'S.
Natanguliza Shukrani, Mbarikiwe sana watu wangu wa nguvu.
Kwa sasa nimeongeza na biashara za Miamala ya simu, pamoja na Vitafunwa kama Korosho za kuoka na zile mbichi.
Jana nimepata wazo la kuweka na spare parts za mashine za photocopy, naomba kama kuna mdau ana fahamu chimbo la bidhaa hizi kwa karikoo anijulishe, aweke hapa ili na wengine pia waone.
Napokea maswali kwa mwenye kuhitaji kuanza biashara ya stationery ili walau nimpatie A, B, C'S.
Natanguliza Shukrani, Mbarikiwe sana watu wangu wa nguvu.