mihadarati
JF-Expert Member
- Aug 27, 2013
- 268
- 74
Wadau habari za Jumapili;
Leo nimeingia jiji la Arusha nikitokea Dar nikakutana na rafiki yangu ambaye tulisoma nae chuo akaniambia anataka anishirikishe jambo kuhusu biashara ya mtandao kampuni inayoitwa Organo..
Na mimi kwa sababu sijafanya utafiti juu ya hiyo biashara kwa ujumla kwani bado n changa, nikasema niwashirishe wadau humu jamvin huenda kuna ambao tayari wameshajiunga.
biashara yenyewe ni ya mtandao kampuni inaitwa Organo Gold ambayo kidogo ingefanana na ile ya Forever living sema tofauti kwamba wao Organo wanadeal na kinywaji cha kahawa pekee na wanaproduce kahawa zenye taste mbalimbali zilizoongezwa virutubisho kama uyoga Mwekundu, na unalipa hela ya kuingia ambyao kuna madaraja tofauti, baada ya hapo utapata idadi ya kahawa kulingana na daraja uliloingilia..mim nataka kupata uzoefu kwenu kama kuna ambaye amekwishifanya hiyo biashara humu..
Ahsanteni