Biashara ya nyanya kwa msimu huu

Biashara ya nyanya kwa msimu huu

kamugishacharles

New Member
Joined
May 3, 2016
Posts
2
Reaction score
1
Ndugu wapendwa naomba kupata ushauri wa namna ya kupata masoko ya kuuza nyanya hasa katika kipindi ambacho kwa sasa nyanya zimefurika sokoni.Natarajia kuanza kuuza wiki moja ijayo. Je utaratibu mzuri ni upi? kuuza kwa kiloa au ndoo au tenga.
 
jamani mie nina kilio changu kwenu wakulima wa nyanya.
minyanya ya siku hizi sijui ni mshumaa gani.
ama ni ya GH?
yaani nyanya haiivi, ni ngumu adi ina mizizi. haina ladha si kwa kuila mbich ama kuipika
ukweli badilini mbegu wakulima wa nyanya.
nafkir kama mlitaka hybrid ya longevity gene basi this gene works antagonistic with taste. nendeni kwa ile mbegu ya zaman jaman
 
Nguvu ya soko ndo determinant wa kipimo ndg yangu otherwise hizo nyanya zitakunyanyasa usipomsikiliza mlanguzi.
 
jamani mie nina kilio changu kwenu wakulima wa nyanya.
minyanya ya siku hizi sijui ni mshumaa gani.
ama ni ya GH?
yaani nyanya haiivi, ni ngumu adi ina mizizi. haina ladha si kwa kuila mbich ama kuipika
ukweli badilini mbegu wakulima wa nyanya.
nafkir kama mlitaka hybrid ya longevity gene basi this gene works antagonistic with taste. nendeni kwa ile mbegu ya zaman jaman
Mkuu kilio chako ungekielekeza kwa viwanda wazalishaji wa mbegu na wasambazaji. Mkulima akitaka mbegu anaenda duka la pembejeo kwa hitaji la "nataka mbegu zinazodumu kwa muda mrefu" anafanya hivyo ili aendane na matakwa ya mteja wa kati sio mlaji.
 
Huku kwetu mbona bei ipo chini sana 5000 kwa debe na mzunguko wa pesa ni mdogo ile mbaya!
 
nakaribia kuanza kuvuna nyanya. ni nyanya za kawaida na zile ndogo (cherry tomatoes). mwenye uhitaji wa jumla tafadhari tuwasiliane mapema
 
Mkuu kilio chako ungekielekeza kwa viwanda wazalishaji wa mbegu na wasambazaji. Mkulima akitaka mbegu anaenda duka la pembejeo kwa hitaji la "nataka mbegu zinazodumu kwa muda mrefu" anafanya hivyo ili aendane na matakwa ya mteja wa kati sio mlaji.
anautaalamu? ama maana kuuza kwenyewe hawezi sasa kuunda mbegu si itakuwa kasheshe
 
Wakuu mimi nyanya zangu zimebakiza wiki mbili nianze kuvuna na nimelimia Mwanza kama eka moja hv. Nauliza soko lipoje kwa sasa
 
Back
Top Bottom