Biashara ya kuuza Pweza

Biashara ya kuuza Pweza

Yahee pweza njoo ununue kwetu huku zanzibare tunauza bei nafuu sana kuliko huko tanganyika.
Hahaha nakubalina na wewe,ila changamoto ni usafirishaji.
Air Tanzania ndio ilikuwa mkombozi,ila Precision Air kwa flight ya Zanzibar-Mwanza ni changamoto kubwa saana.

Ila ata hivyo,Zanzibar sio rahisi saana pia,maana mahoteli ya kitalii ni mengi saana kuliko Dar,sasa demand ni kubwa mno kupita maelezo.Maana hata ukienda Vijiji vya Pwejuu na Paje ambapo idadi kubwa hupatikana huko bado ni ghali saana.Maana wanuzwa kwenye mahoteli kwa bei mbaya.
Labda mtu atumie kununua kisiwani Pemba ambapo hakuna changamoto kubwa ya Mahoteli,maana hata wafanyabiashara wa hapa Zanzibar wale wanaooza Jumbo Prawns wanawaagiza Pemba huko kwa Wakojani.
Unajua ukiwa na connection nzuri ya usafiri inalipa,ila hili ndio changamoto,maana bidhaa ikiharibika ni bonge la hasara.
Mliopo Dar hembu niambieni Kilo moja ya Pweza ni Kiasi gani?
 
Hahaha nakubalina na wewe,ila changamoto ni usafirishaji.
Air Tanzania ndio ilikuwa mkombozi,ila Precision Air kwa flight ya Zanzibar-Mwanza ni changamoto kubwa saana.

Ila ata hivyo,Zanzibar sio rahisi saana pia,maana mahoteli ya kitalii ni mengi saana kuliko Dar,sasa demand ni kubwa mno kupita maelezo.Maana hata ukienda Pwejuu na Paje ambapo idadi kuwa hupatikana huko bado ni ghali saana.Maana wanuzwa kwenye mahoteli kwa bei mbaya.
Labda mtu atumie kununua kisiwani Pemba ambapo hakuna changamoto kubwa ya Mahoteli,maana hata wafanyabiashara wa hapa Zanzibar wale wanaooza Jumbo Prawns wanawaagiza Pemba huko kwa Wakojani.
Unajua ukiwa na connection nzuri ya usafiri inalipa,ila hili ndio changamoto,maana bidhaa ikiharibika ni bonge la hasara.
Mliopo Dar hembu niambieni Kilo moja ya Pweza ni Kiasi gani?
Mawazo mazuri sana haya, na unajua sana kujenga hoja zako.

Big up sana and keep it up
 
wana JF naomba mchanganuo wa biashara ya pweza , niwe na mtaji wa shilingi ngapi? na naitajika kuwa na vitu gani ili kufanikisha biashara hii?
 
Wakuu samahani kwa usumbufu Mimi nikijana Mdogo tu nasoma Chuo kimojawapo hapa mwanza,kilichonileta kwenu leo niswala la kutaka kujua kuhusu biashara ya supu ya pweza kwani nataka nifungue banda kwa hapa mwanza usiku niuze supu ya pweza maeneo nitaomba msaada badae pia nitawasilisha Yale niliyo yakusudia mm badae ila kwa sasa naombeni mnisaidie kwa haya machache...
1) upatikanaji wa pweza dar(feli)
2)bei zake
3)utunzaji bila kuharibika
4)nini zaidi nizingatie
5)mengineyo niliyo yasahau

Tafadharini sana kwa wale wazee wa kukatisha tamaa sijawaiteni hapa ...
Km upo tayali bei ya pwza kg 1 ni 7500 huku dar pale soko la ferry
Km unahitaji ni pm tufnye biashara
 
GHARAMA:Bei ya pweza kwa sasa ni 7500/= kg 1,ingawa huwa inatabia ya kupanda na kushuka, kutokana na upatikanaji wake.
NB
Pia bei inabadilika kulingana na ukubwa wa nyama yenyewe.

UTUNZAJI WAKE:Nyama ya pweza huitaji ubaridi wa kutosha.Hivyo ni vema uwe na jokofu au uwe unanunua mabarafu yale makubwa na kuyakatakata ndani ya chombo utakacho hitaji kuifadhia hiyo nyama ya pweza.

USAFIRISHAJI WAKE: Unatakiwa kutafuta ndoo au jaba( kulingana na wingi wa mzigo wako).Kisha unawaweka humo na hapo unaweka na mapande ya barafu,ili kuzuia wasije kuaribika.
NB
Chombo cha usafiri,unaweza kutumia wa aina yoyote ile,cha msingi uzingatie mabarafu uliyoyaweka katika mzigo wako.

Nadhani ufahamu wangu,unaishia hapa.Ngoja wenye maarifa zaidi,watoe mchango wao pia.

""KILA LA KHERI,MKUU."""
 
Nahitaji kuanza biashara ya Pweza, kwa aliyewahi kufanya au anafanya biashara hii tafadhali aniambie niandae shingapi , na anipe njia ya kumdhibiti dogo nitakaye muweka asiniibie. Asanteni.
 
Back
Top Bottom