karv
JF-Expert Member
- Dec 26, 2019
- 1,799
- 3,221
BIASHARA YA MTUMBA
Mtumba ni biashara ambayo wengi wanaipuuzia sana lakini ni kati ya n biashara zenye faida sana hasa ukiwa makini
Mfano unaweza ukanunua nguo kwa kupoint 500 ukifua ukaja kuiuza hata elfu 2
Biashara ya mtumba haihitaji mtaji mkubwa sana maana hata elfu 50 inaweza kutosha kwa kuanzia
Baadhi ya nguo za mtumba zenye soko sana kwa sasa
*Offsholder kwa dar na mwanza pia mikoa yenye joto
*Makoti hasa mbeya na sehemu zenye baridi
*Nguo za watoto
*Mashati ya wanaume
*Jinsi kwa wote
*Sidiria
Kama mtaji wako ni mdogo unaweza ukaanza kwa kupoint yan unawahi mapema sana mda wanakata unaanza kuchagua baada ya hapo unaenda kuziuza maisha safi hii unaweza kuanza kwa mtaji wwt
Kununua balo zima hii unaweza kununua peke yako au ukashare na mtu mkanunua balo moja halafu mkagawana maana balo moja bei ndogo kabisa ni kama laki 3 na kuendelea kutegemeana na aina ya bidhaa utanunua
Pia kama mtaji hautoshi mnaweza kuwa hata 4 mkanunua halafu mkauza
Pia kwa wale mitaji mikubwa mnaweza kuagiza huko ughaibuni
Wapi utapata mtumba mzuri
*MWANZA kwa wakazi wa kwanza nenda pale mlango mmoja Jumatatu mapema sana huwa wanachana mabalo kwa kupoint ila tatizo lako hadi wale walioweka oda wachukue zinazobaki unaweza ukachukua na wewe mf mashati yanaanzia elfu 2 wale wakishachagua yaliyobaki ni elfu 3 ambayo ni mazuri
Pia, hapo hapo kuna sehemu wanauza viatu mabegi suti za kike yan kwa kifupi hapo mlango mmoja utapata kila mtumba iyo siku ujanja ni kuwahi tu
*MOROGORO sio mzoefu sana kwa kuchukua mtumba Morogoro ila soko la mji mpya siku ya jumanne na kariakoo ya Morogoro stendi ya zamani ya hiace kuna kama kasoko fulani hivi ukiingia humo utapata nguo za watoto elfu 2 hadi elfu 5 ambazo ukiziweka vizuri utauza elfu 7 na zaidi na penyewe uwahi asubuhi sana
*DAR ES SALAAM
kwa mtumba huku ndio funga kazi sasa maana huku mtaji pia ujanja kuwahi dar tembelea sehemu zifuatazo
KArume hapa achana na madalali wa nje ingia kule ndani kabisa utakutana na nguo hadi za mia 7 chagua nenda kazifue halafu uza safi kabisa narudia tena ingia kule ndani kabisa achana na madalali wa nje
KARIAKOO huko ndio funga kazi kabisa japo mitaa sijui vizuri na sijui baada ya hamisha hamisha ya wamachinga ila we tembea mle utakutana nazo tu
BUGURUNI huku kunasifika kwa pochi kali za akina dada kama ushawahi kupita mwenge usiku ushakutana na pochi elfu 5 sasa hao wanazitoa huku Buguruni narudia tena huku ni pochi kaliiiii
MNAZI MMOJA huku ni kwa wale wenye mabalo ya mtumba ambao wanauza hebu angalia stendi ya gongo la Mboto utaona tu mageti yamechorwa mabalo ya mtumba kwa wale wanaotaka balo unaweza kufika huko ukapata mali saaafi
NBia kwa Dar kuna baadhi ya watu wanaofisi zao za kuuza mtumba tofauti na maeneo tajwa hao huwa wanauza hata nusu balo na pia bali kamili na hata kwa kupointi sasa hao wametapakaa sehemu nyingi kuna mawasiliano kawe mbezi Manzese huko kote wapo
Pia baada ya hama hama ya machinga sijajua baadhi ya vitu bado hasa karume na kariakoo
HASARA YA KUNUNUA BALO
*Hasara kubwa hapa unaweza kununua malonya lonya ambayo hayauziki hivyo kufanya uuze kwa bei ya hasara
KIPI UZINGATIE
*KWA WANAOPOINT: kagua sana nguo yako kabla hujachagua sana sana huwa tuna angalia
1)mashati kola na makwapa kama hayana madoa maana yale madoa ya kwapa ukifua ni vigumu kutoka
2)shifon na offsholder kama zimechanika kokote
Kwa ujumla angalia nguo kama haijachanika haina madoa inavutia kwa kutazama na inayopunguzika kwa urahisi
FAIDA YA KUUZA MTUMBA :faida kubwa hii biashara inalipa sana maana kwa nguo moja unaweza kuzalisha faida hata nusu ya bei ya kununua
Kikubwa cha kuzingatia pendelea kuwa na watu maalumu wa kuchukua mizigo kwao maana kuna muda wanaweza kukujali hata kwa ziada na mambo mengine na kukutaatifu kama kuna mzigo mpya umeingia na mengineyo
MASOKO YAKE :
1)kwenda kuuza kwenye minada vijijini
2)kutembeza sehemu maalumu kama ofisini na vyuoni
3)kwa belo unaweza kulichana kwenye minada au ukawa na watu wanapoint kwako
4)kwa wamama unaweza hata ukawa unakopesha safi tu
5)kwa wahuni mtaani mtaani
NB:nguo za watoto wanawake na viatu vya shule vinauzika sana kuliko mashati na suruali za wanaume
Kama kuna mtu ananyongeza au cha ziada anaweza kushare na sisi
Pia kama utahitaji ushauri unaweza kuja PM tukaelekezana maana hiyo ni biashara iliyonipa shavu sana wakati nipo chuoni kwenye matumizi madogo madogo
Ahsante
Mtumba ni biashara ambayo wengi wanaipuuzia sana lakini ni kati ya n biashara zenye faida sana hasa ukiwa makini
Mfano unaweza ukanunua nguo kwa kupoint 500 ukifua ukaja kuiuza hata elfu 2
Biashara ya mtumba haihitaji mtaji mkubwa sana maana hata elfu 50 inaweza kutosha kwa kuanzia
Baadhi ya nguo za mtumba zenye soko sana kwa sasa
*Offsholder kwa dar na mwanza pia mikoa yenye joto
*Makoti hasa mbeya na sehemu zenye baridi
*Nguo za watoto
*Mashati ya wanaume
*Jinsi kwa wote
*Sidiria
Kama mtaji wako ni mdogo unaweza ukaanza kwa kupoint yan unawahi mapema sana mda wanakata unaanza kuchagua baada ya hapo unaenda kuziuza maisha safi hii unaweza kuanza kwa mtaji wwt
Kununua balo zima hii unaweza kununua peke yako au ukashare na mtu mkanunua balo moja halafu mkagawana maana balo moja bei ndogo kabisa ni kama laki 3 na kuendelea kutegemeana na aina ya bidhaa utanunua
Pia kama mtaji hautoshi mnaweza kuwa hata 4 mkanunua halafu mkauza
Pia kwa wale mitaji mikubwa mnaweza kuagiza huko ughaibuni
Wapi utapata mtumba mzuri
*MWANZA kwa wakazi wa kwanza nenda pale mlango mmoja Jumatatu mapema sana huwa wanachana mabalo kwa kupoint ila tatizo lako hadi wale walioweka oda wachukue zinazobaki unaweza ukachukua na wewe mf mashati yanaanzia elfu 2 wale wakishachagua yaliyobaki ni elfu 3 ambayo ni mazuri
Pia, hapo hapo kuna sehemu wanauza viatu mabegi suti za kike yan kwa kifupi hapo mlango mmoja utapata kila mtumba iyo siku ujanja ni kuwahi tu
*MOROGORO sio mzoefu sana kwa kuchukua mtumba Morogoro ila soko la mji mpya siku ya jumanne na kariakoo ya Morogoro stendi ya zamani ya hiace kuna kama kasoko fulani hivi ukiingia humo utapata nguo za watoto elfu 2 hadi elfu 5 ambazo ukiziweka vizuri utauza elfu 7 na zaidi na penyewe uwahi asubuhi sana
*DAR ES SALAAM
kwa mtumba huku ndio funga kazi sasa maana huku mtaji pia ujanja kuwahi dar tembelea sehemu zifuatazo
KArume hapa achana na madalali wa nje ingia kule ndani kabisa utakutana na nguo hadi za mia 7 chagua nenda kazifue halafu uza safi kabisa narudia tena ingia kule ndani kabisa achana na madalali wa nje
KARIAKOO huko ndio funga kazi kabisa japo mitaa sijui vizuri na sijui baada ya hamisha hamisha ya wamachinga ila we tembea mle utakutana nazo tu
BUGURUNI huku kunasifika kwa pochi kali za akina dada kama ushawahi kupita mwenge usiku ushakutana na pochi elfu 5 sasa hao wanazitoa huku Buguruni narudia tena huku ni pochi kaliiiii
MNAZI MMOJA huku ni kwa wale wenye mabalo ya mtumba ambao wanauza hebu angalia stendi ya gongo la Mboto utaona tu mageti yamechorwa mabalo ya mtumba kwa wale wanaotaka balo unaweza kufika huko ukapata mali saaafi
NBia kwa Dar kuna baadhi ya watu wanaofisi zao za kuuza mtumba tofauti na maeneo tajwa hao huwa wanauza hata nusu balo na pia bali kamili na hata kwa kupointi sasa hao wametapakaa sehemu nyingi kuna mawasiliano kawe mbezi Manzese huko kote wapo
Pia baada ya hama hama ya machinga sijajua baadhi ya vitu bado hasa karume na kariakoo
HASARA YA KUNUNUA BALO
*Hasara kubwa hapa unaweza kununua malonya lonya ambayo hayauziki hivyo kufanya uuze kwa bei ya hasara
KIPI UZINGATIE
*KWA WANAOPOINT: kagua sana nguo yako kabla hujachagua sana sana huwa tuna angalia
1)mashati kola na makwapa kama hayana madoa maana yale madoa ya kwapa ukifua ni vigumu kutoka
2)shifon na offsholder kama zimechanika kokote
Kwa ujumla angalia nguo kama haijachanika haina madoa inavutia kwa kutazama na inayopunguzika kwa urahisi
FAIDA YA KUUZA MTUMBA :faida kubwa hii biashara inalipa sana maana kwa nguo moja unaweza kuzalisha faida hata nusu ya bei ya kununua
Kikubwa cha kuzingatia pendelea kuwa na watu maalumu wa kuchukua mizigo kwao maana kuna muda wanaweza kukujali hata kwa ziada na mambo mengine na kukutaatifu kama kuna mzigo mpya umeingia na mengineyo
MASOKO YAKE :
1)kwenda kuuza kwenye minada vijijini
2)kutembeza sehemu maalumu kama ofisini na vyuoni
3)kwa belo unaweza kulichana kwenye minada au ukawa na watu wanapoint kwako
4)kwa wamama unaweza hata ukawa unakopesha safi tu
5)kwa wahuni mtaani mtaani
NB:nguo za watoto wanawake na viatu vya shule vinauzika sana kuliko mashati na suruali za wanaume
Kama kuna mtu ananyongeza au cha ziada anaweza kushare na sisi
Pia kama utahitaji ushauri unaweza kuja PM tukaelekezana maana hiyo ni biashara iliyonipa shavu sana wakati nipo chuoni kwenye matumizi madogo madogo
Ahsante