ABDALLAH AMOUR
Member
- May 12, 2009
- 25
- 35
Ndugu wanajamvi, nimefuatilia kwa muda mrefu sana maudhui ya hii biashara ya kupokea wageni toka pande mbalimbali za dunia. kwa hakika ni biashara ambayo haina stress kabisa, cha msingi kujitangaza na kujiweka karibu na wageni ulimwenguni kupitia mitandao ambayo ndio kiungo kikuu cha mawasiliano kati yako na mgeni.
Nimeangalia sana kwa badhi ya wafanyabiashara ambao tayari wako sokoni kwa hii biashara , inaonekana kama kuna unafuu mkubwa katika kuiendesha na hata udhibiti wake wa hali ya juu kwani unajua wageni wanaoingia na kutoka katika sehemu yako.
unachotakiwa kufanya ni kujenga au kama tayari unayo sehemu ambayo unaweka ukatumia kama kianzio cha biashara yako, na kujisajili katika mitandao ya wageni kama www.airbnb,com na www.booking.com unaweka picha za sehemu yako na bei unaweza ukaaangalia kwa wale wenzako ambao wameshaanza, bei zao zikoje nawe ushushe kidog kwa ajili ya kuvutia wateja pamoja na kuboresha huduma za ziada kama breadfast iwe ya maana na iwe ya kiafrika zaidi yaani kwa vyakula ambavyo kwa wageni ni adimu kupatikana katika nchi zao.
natanguliza shukrani zako kwa wanajamvi kwa muktadha huo wa biashara nagalau tujitahidi kupambana na hali ngumu za maisha kwa wakati huu tulionao.
Nimeangalia sana kwa badhi ya wafanyabiashara ambao tayari wako sokoni kwa hii biashara , inaonekana kama kuna unafuu mkubwa katika kuiendesha na hata udhibiti wake wa hali ya juu kwani unajua wageni wanaoingia na kutoka katika sehemu yako.
unachotakiwa kufanya ni kujenga au kama tayari unayo sehemu ambayo unaweka ukatumia kama kianzio cha biashara yako, na kujisajili katika mitandao ya wageni kama www.airbnb,com na www.booking.com unaweka picha za sehemu yako na bei unaweza ukaaangalia kwa wale wenzako ambao wameshaanza, bei zao zikoje nawe ushushe kidog kwa ajili ya kuvutia wateja pamoja na kuboresha huduma za ziada kama breadfast iwe ya maana na iwe ya kiafrika zaidi yaani kwa vyakula ambavyo kwa wageni ni adimu kupatikana katika nchi zao.
natanguliza shukrani zako kwa wanajamvi kwa muktadha huo wa biashara nagalau tujitahidi kupambana na hali ngumu za maisha kwa wakati huu tulionao.