Biashara ya Hardware na workshop ya milango na frame za mbao

Biashara ya Hardware na workshop ya milango na frame za mbao

neggirl

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2009
Posts
4,860
Reaction score
2,149
Habari wakuu,
Nina wazo la kuanzisha workshop ndogo ya furniture specifically milango na frame za mbao kwa lengo la kupanua wigo wa biashara na ku compliment biashara ya hardware mfano kuongeza mzunguko wa bidhaa zitakazohitajika katika matengezo ya milango au zinazotoka na milango mfano Vitasa.

-Kwa nia ya kuongeza ufahamu zaidi; kwa walio na hardaware does it real worth?
-Naomba ushauri mashine gani lazima niwe nazo?
-Mambo muhimu ya kuzingatia kadri navyojipanga
Natanguliza shukrani
 
-Kwa nia ya kuongeza ufahamu zaidi; kwa walio na hardaware does it real worth
Thamani ipo, kitu chochote kinachofanyika hakikosi thamani, tena ukikifanya kwa kukiongezea thamani kitahitajika sana.
Kwa vile itakuwa mwanzo kidogo matokeo hayataonekana mapema ila yatakavyo onekana sinmilango tu bali vitu vingi vitahitajika na itakuwa faida kwako kubwa.
 
Naomba ushauri mashine gani lazima niwe nazo?
Mashine ndogo za benchi kama router mashine, engle grenda, drill mashine, compressor, jig saw , secular saw zinawesa kutosha kuanzia.
Mashine nyingine kubwa kama za kuranda, kuchana, spindle unaweza kupata kule utakapo nunua mbaona kwa mongozo wa fundi wakati wa maandalizi.
 
Mambo muhimu ya kuzingatia kadri navyojipanga
Muhimu kutafuta soko kwa kutangaza na kuwa na milango ya kuonyesha.
Mlango ukiwa na fremu ni bora zaidi
Aina za mbao eneo husika kuwa na mlango ya aina kadhaa ya mbao na bei iwe rafiki.
Mafundi ni wa kuzingatia sana, maana fundi ndie atakutengenezea soko na faida.
Siku mteja atakuja na sample na vipimo vyake na muundo wake, fundi ndie atakae fanya makadirio,hivyo kuwa makini asizidishe sana bei wala kupunguza sana
Vipimo vya milango ya sample viwe kati ya centimeters 85-90/200-220
Mengine fundi atakupa mwongozo

Nakutakia kufanikiwa.
 
Mashine ndogo za benchi kama router mashine, engle grenda, drill mashine, compressor, jig saw , secular saw zinawesa kutosha kuanzia.
Mashine nyingine kubwa kama za kuranda, kuchana, spindle unaweza kupata kule utakapo nunua mbaona kwa mongozo wa fundi wakati wa maandalizi.
Pendaelli Nakushukuru sana sana kwa madini haya. Hapo kwenye mashine kubwa unamaanisha sio lazima niwe nazo naweza chukua mbao mfano zimerandwa tayari, na workshop nikawa na randa ndogo ya mkono?
 
Pendaelli Nakushukuru sana sana kwa madini haya. Hapo kwenye mashine kubwa unamaanisha sio lazima niwe nazo naweza chukua mbao mfano zimerandwa tayari, na workshop nikawa na randa ndogo ya mkono?
Ndio sio lazima kuwa nazo, ingawa zenyewe ukiwa nazo ni biashara nyingine yenye faida kama sehemu yako ina mzunguko mzuri.

Lakini ukiwa na mashine ndogo hizi ambaazo wastani wa milion unaweza kuzipata zote zinazo tosha kuanza kazi.

Huko utakapo nunua mbao nadhani ndiko utakapo randa kunyoosha na ikija karakana kwako ni maandalizi madogo na finishing , ndivyo tunavyo fanya sisi kwa muda mrefu na hatujawahi kukutana na changamoto hata kazi ikiwa kubwa kiasi gani.
 
Ndio sio lazima kuwa nazo, ingawa zenyewe ukiwa nazo ni biashara nyingine yenye faida kama sehemu yako ina mzunguko mzuri.

Lakini ukiwa na mashine ndogo hizi ambaazo wastani wa milion unaweza kuzipata zote zinazo tosha kuanza kazi.

Huko utakapo nunua mbao nadhani ndiko utakapo randa kunyoosha na ikija karakana kwako ni maandalizi madogo na finishing , ndivyo tunavyo fanya sisi kwa muda mrefu na hatujawahi kukutana na changamoto hata kazi ikiwa kubwa kiasi gani.
Barikiwa..asante sana
 
Back
Top Bottom