Biashara: Ikitokea una manunuzi mengi kuliko mauzo

Biashara: Ikitokea una manunuzi mengi kuliko mauzo

Hizo hela za manunuzi mengi umetoa wapi kama mauzo kiduchu ? Unless umetoa hela kwenye vyanzo vingine ukaamua kuongeza mzigo/mtaji ! Maelezo yako hayako sawia !
 
Labda kama unaongeza mtaji wako ila manunuzi huwa yanategemea mauzo isipokuwa tu kama mauzo yako huzidi thamani halisi ya bidhaa unazouza kwa zaidi ya 50%
 
Maana yake una ukwasi mwingi kupita kiasi na hiyo biashara huijui vizuri na yumukini wateja wako huwajui vizuri vionjo vyao.
Mara nyingi hali hiyo huwapata sana wastaafu baada ya kupata malipo ya mkupuo na kujiingiza moja kwa moja kwenye biashara kwa kufuata mkumbo maarufu wa kujaza bidhaa hadi nje ya duka.
Kwa bidhaa zenye ukomo wa matumizi huishia kuteketezwa, ambayo kimsingi ni kuteketeza mtaji na kuwa mlango wa kutokea.... Kufunga biashara!.
 
Back
Top Bottom