Biashara 5 unazoweza kufanya ukiwa na mtaji mdogo

Emmanuel josh

New Member
May 13, 2019
0
11
Habari wana jukwaa wenzangu karibuni na msome makala yangu

Tuangalie biashara 5 za mtaji mdogo usiozidi Tshs. 100,000 unazoweza kufanya na zenye faida kubwa. Mtaji mkubwa unaohitajika unapoanzisha biashara ni muda na wala sio pesa kama utakavyojifunza hapa.

Mimi binafsi siamini kama kuna biashara ndogo, ila najua kuna biashara unaweza kuanza na mtaji mdogo na zikakuletea faida kubwa. Hiyo ambayo inaitwa “biashara ndogo” ukiifanya kwa ubora wa hali ya juu na bidii ipo siku itakutoa.

Nilipokuwa narudi mazoezini asubuhi ya leo, nilijiuliza je ni biashara gani unaweza kuanza na mtaji mdogo (isiyozidi laki moja)? Nilijua zipo ila sikufikiria kama zinaweza kuleta faida nzuri tu utakapo zifanya kwa ubora.

Hivyo, nikaanza kuziandika kwenye simu na baada ya dakika chache nikajikuta nina orodha ya bishara zaidi ya ishirini unazoweza kuanza na mtaji mdogo na zenye faida kubwa ambazo nitaziandika hapa chini.

Kabla hatujaenda kwenye hiyo orodha ya hizo bishara za mtaji mdogo, ningependa kuweka sawa maana yangu ninaposema “zenye faida kubwa”.

Faida kubwa haimaanishi mamilioni ya fedha, bali ni kwamba faida utakayoipata kulingana na mtaji wako ni nzuri na usipokata tamaa zitakufikisha mbali.

Zingatia: Unapotaka kuanzisha biashara yoyote ile, ni vyema kufuatilia utaratibu na sheria za mahali ulipo. Tafadhali ilinde biashara yako kwa kufuata kanuni zote zilizowekwa na Serikali. Baada ya kulisawazisha hilo, twende kwenye hiyo orodha ya biashara za mtaji mdogo kama zifuatazo;

1. KUPIKA KWA ODA​

Kama wewe ni mpishi mzuri au una mtu anayejua kupika, basi jitangaze kama unapokea oda za mapishi fulani. Tuchukulie unaweza kupika makande au wali nyama vizuri.

Unachoweza kufanya ni kwenda maofisi ya karibu yako na kuwaambia kwamba wakutafute wanapohitaji hicho chakula wakati wa mchana na wewe utawaletea.nUsisahau kuacha mawasiliano yako ili waweze kukutafuta. Wengi wao watapenda hiyo huduma kwasababu hawatohitaji kutoka tena kufata chakula.

2. UREMBO (MAKEUP, KUSUKA & KUCHA)​

Urembo ni gharama. Wanadada wanataka kupendeza wanapokwenda safari zao kama ni kazini ama shughulini. Uzuri ni kwamba hii ni biashara ya kila siku unayoweza kufanya. Baada ya kufanya utafiti wangu, nimebaini kwamba kufanya makeup, kutengeneza kucha na ususi wa nywele zinalipa vizuri tu.

Kuna watu wengi tu wanaendesha maisha yao kupitia biashara hizo. Kwanini wewe ushindwe? Na kama sio mtaalamu, hakuna tatizo. Chukua muda wako na kujifunza, ndani ya muda utaweza.

3. KUUZA JUISI NA ICECREAM​

Kujifunza kutengeneza juisi au icecream haitakuchukuwa muda mrefu. Ili kufanikiwa katika biashara hii, cha muhimu ni kujitofautisha. Muhimu zaidi unapofanya biashara ya kutengeneza juisi au icecream, ni kuweka mazingira yako safi na salama kwa wateja wako.

Uzuri wa biashara hii ni kuwa mtaji wake ni mdogo sana. Elfu kumi tu inatosha kuanzia na wapo waliofanya hivyo na wamekuza biashara zao kama vile Mak Juice au Zanana Juice Box.

4. KILIMO CHA MBOGAMBOGA​

Kilimo ni sehemu kubwa ya maisha ya watanzania na wale wa nchi nyingi za Afrika. Kila siku zikienda, kilimo huzidi kuwa ni biashara ya matajiri kwasababu shamba lina gharama kubwa.

Licha ya hivyo, bado kuna fursa ya kutengeneza kipato kupitia kilimo cha mbogamboga hata kama una mtaji mdogo. Anza na sehemu ndogo tu unayoweza kupata hata kama ni nyumbani.

5. UFUGAJI WA NDEGE (KUKU, BATA, N.K)​

Hii ni biashara ambayo ina faida kubwa lakini pia ina changamoto zake kama vile kuku wako kufa. Vifo vya mifugo huwaumiza sana wafugaji na mara nyingi husababishwa na mifugo hiyo kula uchafu. Hivyo, unapoingia kwenye ufugaji jitahidi uwe na mazingira safi na salama kwa mifugo yako.

Usafi wa mara kwa mara hasa hasa kwenye malisho yao utahitajika. Kwa vile mtaji ni mdogo, unaweza kuanza na kuku wa kienyeji, bata au hata njiwa. Japo kuwa wanachukuwa muda ila kuwa mvumilivu, faida utaiona
 
Kweye makaratasi hakuna biashara ngumu na biashara zote zina faida kubwa.
Mambo ya: Kila shimo utaweka Miche miwili.. Kila mche utazaa Matunda manne hivyo Kila shimo utapata Matunda 8... Jumla una mashimo 2000, hivyo utakua na Matunda 16,000, ambapo ukiuza kwa hasara sana basi Kila tunda utauza 1000... Hivyo jumla utakua na pesa taslim 16,000,000 ndani ya miezi miwili tu!!!! Sasa Ingia Field ..
 
Mambo ya: Kila shimo utaweka Miche miwili.. Kila mche utazaa Matunda manne hivyo Kila shimo utapata Matunda 8... Jumla una mashimo 2000, hivyo utakua na Matunda 16,000, ambapo ukuuza kwa hasara sana basi Kila tunda utauza 1000... Hivyo jumla utakua na pesa taslim 16,000,000 ndani ya miezi miwili tu!!!! Sasa Ingia Field ..
Mambo ya motivation speakers na unamkuta yeye kwapa limemloa jasho kwa kupuyanga kwa miguu mitaani
 
Watu bhana Sasa we ulitaka alete uzi kuwa biashara hazilipi watu wasifanye watafute ajira?? au ulitakaje yaani..?
Mambo ya: Kila shimo utaweka Miche miwili.. Kila mche utazaa Matunda manne hivyo Kila shimo utapata Matunda 8... Jumla una mashimo 2000, hivyo utakua na Matunda 16,000, ambapo ukuuza kwa hasara sana basi Kila tunda utauza 1000... Hivyo jumla utakua na pesa taslim 16,000,000 ndani ya miezi miwili tu!!!! Sasa Ingia Field ..
 
We una matatizo ya akili trust me, Sasa anzisha basi naww uzi uki-motivate watu wasifanye biashara au ufugaji wazurule na mabahasha ofisi za watu kuomba kazi...yaan mtu kutoa idea imekuwa kosa?? kwani we hujawahi kumshauri mtu kitu ambacho hujawahi hata kukifanya?? So far umejuaje Kama yeye anapuyanga kwa miguu mtaani?? Kuna watu wanapata business ideas humuhum JF hadi wanarudi kutoa special Thanks kwa wachangiaji husika waliotoa hizo idea. Kuwa Matured Mkuu.
Mambo ya motivation speakers na unamkuta yeye kwapa limemloa jasho kwa kupuyanga kwa miguu mitaani
 
We una matatizo ya akili trust me, Sasa anzisha basi naww uzi uki-motivate watu wasifanye biashara au ufugaji wazurule na mabahasha ofisi za watu kuomba kazi...yaan mtu kutoa idea imekuwa kosa?? kwani we hujawahi kumshauri mtu kitu ambacho hujawahi hata kukifanya?? So far umejuaje Kama yeye anapuyanga kwa miguu mtaani?? Kuna watu wanapata business ideas humuhum JF hadi wanarudi kutoa special Thanks kwa wachangiaji husika waliotoa hizo idea. Kuwa Matured Mkuu.
Niwe matured mara ngapi kijana mdogo. Unadhani hapa unaongea na mtoto mwenzio. Nimeshafanya shughuli nyingi nahisi kabla hujazaliwa. Ingia kwenye game uone sio unaleta theory tu hapa
 
We una matatizo ya akili trust me, Sasa anzisha basi naww uzi uki-motivate watu wasifanye biashara au ufugaji wazurule na mabahasha ofisi za watu kuomba kazi...yaan mtu kutoa idea imekuwa kosa?? kwani we hujawahi kumshauri mtu kitu ambacho hujawahi hata kukifanya?? So far umejuaje Kama yeye anapuyanga kwa miguu mtaani?? Kuna watu wanapata business ideas humuhum JF hadi wanarudi kutoa special Thanks kwa wachangiaji husika waliotoa hizo idea. Kuwa Matured Mkuu.
Amekuja mwenyewe sasa😆😆😆
 
Chief shukurani sana kwa ideas nzuri . It takes an optimistic mind to see the glass is half full and not half empty! Hakuna anayekosea hapo kati ya anayeona glass ya maji ipo nusu kujaa na anayeona ipo nusu kuwa tupu ila namna ya kuona ni tofauti(mtazamo)! .Na mtazamo ndicho kinachoathiri maamuzi yetu na uchukuaji wetu wa hatua au matendo dhidi ya fursa.

Barikiwa sana🙏🏽🙏🏽🙏🏽
 
Kuna biashara ya genge la mtaani, kuna kuuza vitabu vya watoto utembeze barabarani, kuna kununua maji na kuuza mtaani, kuna kuuza urembo kutembeza, kuna kuuza mitumba

Biashara zinahitaji uvumilivu, zinahitaji nidhamu ya pesa, zinahitaji kuendelea kujifunza kila siku kutoka kwa waliofanikiwa na waliofeli.

Ni vizuri kuwa na positive attitude lakini kwenye biashara ni vyema uingie ukiwa full informed ya risk zake zote ili usije anguka kwa pressure
 
Ufugaji kwa laki
Mkuu hiyo laki ni kubwa. Kuna mtu namjua alianza na kuku 2 wa kienyeji, mmoja tetea na mwingine jogoo. Kwa sasa ana kuku zaidi ya 500. Anawapunguza kwa kuuza kila mara. Sema changamoto ipo kwenye eneo la kufugia hasa ukiwa upo kwenye nyumba ya kupanga.
 
Back
Top Bottom