Chanzo cha harusi kutofungwa kilitokana na kutokuwa na mawasiliano mazuri na washenga wake ambao ni Bwana Amoni Mwangosi ambaye ni mshenga wa Bibi harusi na Bwana Angolile Mwakisilwa ambaye ni mshenga kwa upande wake wa Bwana harusi.
Bwana harusi alitumia watu wengine kupeleka nauli ya Sh. 24,000/= ya kumchukua bi harusi na mpambe wake bila kufuata taratibu za kimila za kuwajulisha washenga wake ndiyo waende kumchukua mchumba wake hata hiyo watu hao walikataliwa kwa kutotambuliwa na familia hiyo ya bi harusi na kutaka wahusika wafike ili wakabidhiane kwa taratibu zinazotambulikana.
Kwa upande wake wa Mzazi wa Bibi harusi Mzee Akimu Mwalukosya, amesema hana kinyongo bali yaliyopita si ndwele na wagange yajayo kwani makosa yaliyofanyika yanazungumzika.
Jana (Jumanne) jioni kamati ya maandalizi upande wa bwana harusi walikutana kujadili suala hilo. Hata hivyo kamati ya sherehe ya bwana harusi itakutana leo (Jumatano) kupata hatima ya harusi hiyo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.