OLESAIDIMU
JF-Expert Member
- Dec 2, 2011
- 19,139
- 9,574
Tungefuata hayo ni kiongozi gani angesimama?
Kama ni kujibu bora kujibu sawa ila kama unatumia akili na free will..jitazame upya!!!!!
Tungefuata hayo ni kiongozi gani angesimama?
Ha ha hili suala lipo wazi sana. Memorundum ama articles za kampuni toka lini zikaandika ushemeji?? Ukweli ni kwamba jamaa amempigia pande shemeji kupata tenda.
Jana katika mitandao kuna habari za uongo ambazo hazivumiliki zilienea kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ndugu Bernard Kamillius Membe anahusika na suala la ujenzi wa gati la Mbamba Bay kujengwa chini ya kiwango kulikofanywa na kampuni ya kandarasi iitwayo MODSPAN ambayo inahusishwa na shemeji yake.
Ukweli juu ya suala hili ni kwamba hakuna kitu kama hicho kinachomtia hatiani ndugu Bernard Kamillius Membe kwasababu ya mambo yafuatayo;
Moja,yeye sio mjumbe wa bodi ya tenda ambayo iliipa kampuni hiyo ya kandarasi kujenga gati husika.
Pili,walioeneza habari hii wameshindwa kutoa ushahidi usio na mashaka kwamba kweli mmiliki wa kampuni hii ya MODSPAN ni shemeji yake na ndugu Bernard Kamillius Membe iwe kwa kutumia hati ya kiapo au la!
Tatu,waliozusha jambo hili wameshindwa kuainisha kwa ushahidi wa kutosha ni wapi kuna dalili za rushwa ambazo ndugu Bernard Kamillius Membe anaweza akahusishwa nazo moja kwa moja zilizotumika yeye kumsaidia mmiliki wa kampuni ya MODSPAN kupata tenda ya ujenzi wa gati hii!?
Lakini kubwa zaidi ni kufeli kwa watoa habari ya suala hili kuweka hadharani Memarts za kampuni hii ya MODSPAN ili watu wajue kama ndugu Bernard Kamillius Membe anamiliki hisa kiasi fulani za kampuni hii.Mwisho tuhitimishe kwamba hizi sio habari za ukweli.
Zimelenga kumchafulia taswira hii ndugu Bernard Kamillius Membe ambaye anaonekana kuwa mwiba mkali kwa wanasiasa uchwara na mafisadi wanaosaka urais na vyeo ndani ya chama CCM.
Ndugu Bernard Kamillius Membe ni msafi pasipo na shaka linapokuja suala la maadili ya uongozi,diplomasia na ukada ndani ya CCM.
Imetolewa na Friends Of Hon. Membe!
Ukweli hutolewa sio kwa mazuri Tu, hata kwa mabaya yake, Hilo lipo wazi kwa Bw. Membe, SI msafi hata kidogo!
Ha ha hili suala lipo wazi sana. Memorundum ama articles za kampuni toka lini zikaandika ushemeji?? Ukweli ni kwamba jamaa amempigia pande shemeji kupata tenda.
Jana niliongea na mtu wa karibu na Mhe Membe,ameshangaa mno namna ambavyo watu hao wanavyojaribu kumhusisha Mh Membe na jambo hilo,ila yote ni Hofu ya wataka madaraka kumuogopa Membe na kujaribu kutengeneza tuhuma Bandia juu yake.Nimefurahi kuona friends of Membe Wameweka sawa jambo hili.Ni ukweli pasi na Shaka rekodi ya membe ndani ya ccm ni safi!