Benki ya CRDB yazindua SimBanking App mpya inayotumia teknolojia ya kisasa kutambua mahitaji ya wateja na kurahisisha miamala

Blasio Kachuchu

Senior Member
Sep 7, 2016
155
112

Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo, akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa SimBanking App inayotumia teknolojia ya kisasa zaidi inayowezesha kutambua mahitaji ya wateja na kurahisiha hudumana miamala yenye muunganiko wa teknolojia za kisasa na za hali ya juu ikiwamo akili bandia (Artificial intelligence), iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam leo tarehe 19 Julai 2023.

Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo, akiwa mbele ya kifaa kinachotumia teknolojia ya kisasa zaidi inayowezesha kutambua mahitaji ya wateja na kurahisiha huduma na miamala yenye muunganiko wa teknolojia za kisasa na za hali ya juu ikiwamo akili bandia (Artificial intelligence) ambayo inatumika katika SimBanking App mpya iliyozinduliwa leo katika hafla , iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa makao makuu ya Benki ya CRDB, jijini Dar es salaam leo tarehe 19 Julai 2023.

=========== =========
Wakati dunia ikishuhudia mabadiliko makubwa ya teknolojia yanayochagiza maendeleo katika nyanja mbalimbali za maisha, leo Benki ya CRDB inayoongoza kwa ubunifu nchini imezindua SimBanking App inayotumia teknolojia ya kisasa zaidi kutambua mahitaji ya wateja.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa programu hiyo, Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo amesema SimBanking App hii mpya imetengenezwa kwa muunganiko wa teknolojia za kisasa na za hali ya juu ikiwamo akili bandia (Artificial intelligence).

“Teknolojia iliyotumika katika SimBanking App hii inampa uwezo mteja kuchagua mpangilio wa huduma kwa namna ambavyo yeye mwenyewe angependelea, teknolojia hiyo pia ina uwezo wa kutambua ni huduma gani mteja anapendelea zaidi na kumrahisishia namna ya kuipata,” alisema.

Nshekanabo alibainisha kuwa teknolojia hiyo mpya ni ya kimapinduzi katika kufikisha huduma za fedha kwa wateja kwani itaongeza wigo wa huduma zinazoweza kutolewa kidijiti huku kasi ya miamala ya wateja ikirahishwa kwa kiasi kikubwa.

“Eneo jingine ambalo tumelipa uzito mkubwa katika SimBanking App hii mpya ni ulinzi na usalama wa taarifa na miamala ya wateja. Tunatumia teknolojia ya biometriki kuhakikisha usalama kwa wateja. Hii inatufanya kuwa Benki pekee nchini na kati ya chache barani Afrika inayotumia teknolojia hii,” aliongezea Nshekanabo.

Akizungumzia huduma mpya ambazo zimeongezwa, Meneja Mwandamizi wa Huduma za Kidijiti na Ubunifu wa Benki ya CRDB, Jacklina Jackson amesema SimBanking App inatoa fursa za uwekezaji kwa wateja kwa kuwawezesha kuwekeza kupitia akaunti za uwekezaji (Fixed Deposit) kidijiti.

“Wateja pia sasa hivi wanaweza kupanga uhamisho wa fedha na malipo yanayojiruida au ya mara kwa mara kwa urahisi. Uhamisho unaweza kupangwa kila siku, kila wiki au kila mwezi. Tumeboresha upande wa kumbukumbu za taarifa ya miamala ambapo wateja wanaweza kupata risiti ya miamala yote wakati wowote kwa urahisi,” alisema Jacklina.

Katika upande wa malipo, alisema SimBanking App imeboresha malipo kupitia watoa huduma za kidijiti kwa kuwezesha ukusanyaji wa malipo kupitia programu hiyo ambapo mteja ana uwezo wa kutoa ruhusa ya malipo kwa kutumia mfumo wa namba ya siri ya mara moja (one time passcode).

“Vilevile tumefanya maboresho katika huduma za bima kwa kuongeza kasi na muda wa upatikanaji wa huduma,” aliongezea Jacklina kuhusu huduma hiyo ya bima za vyombo vya moto ambayo ilizinduliwa kwa mara ya kwanza kupitia SimBanking App mwaka 2020 benki ilipofanya maboresho.

Aidha, SimBanking App mpya inakuja na programu ya uaminifu (loyalty program) inayowawezesha wateja kupata kupata alama wanapotumia application na kisha kujishindia zawadi. Wateja pia aplikesheni hii mpya pia inatoa fursa kwa wateja kutoa maoni yao kila wakati wanapokamilisha miamala mfumo unaohusisha uwasilishaji wa maandishi na matumizi ya emoji kuonyesha hisia juu ya huduma.

Hii ni mara ya pili kwa Benki ya CRDB kufanya maboresho makubwa katika huduma ya SimBanking baada ya maboresho yaliyofanyika mwaka 2020. Tarifa ya Benki hiyo inaonyesha sasa hivi asilimia 96 ya miamala yote inafanyika kidijitali huku SimBanking ikichangia sehemu kubwa.

Huduma ya SimBanking ambayo ilianzishwa mwaka 2022 imekuwa ikitajwa kuwa moja ya huduma bora zaidi za kidijitali ambazo zinatoa mchango mkubwa katika ujumuishi wa kifedha nchini na taasisi mbalimbali ndani na nje ya nchi.

SimBanking imepata tuzo mbalimbali ndani na nje ya nchi ikiwamo tuzo za Consumer Choice Awards, tuzo za za Global Finance zinazotolewa nchini Marekani, na hivi karibuni imepata tuzo ya huduma bora ya kidijitali katika tuzo za Tanzania Digital Awards.







 
Kweli Tz iko nyuma sana!
Artificial intelligence gani hiyo?kwa sababu hili neno ndio linaongelewa sana duniani, ndio nao wamelichomekea, wakati ni huduma za kawaida tu ila ni mpya kwao.
 
Kuna mahitaji ya mteja zaidi ya pesa? Kwamba inatambua mteja anataka kiasi gani inamuwekea kwenye account ama inafanyaje?
Kila kitu hapo ni mteja anajaza, badala ya karatasi, ni ama simu au kompyuta, sema Tz kila sekta inakuwa siasa sasa.
 
Back
Top Bottom