Benchika, kocha mwenye maamuzi magumu sana

1979Magufuli

JF-Expert Member
Feb 20, 2023
438
1,752
Huyu kocha leo nimemvulia kofia, kumchezesha Duchu ambaye tangu asajiliwe hakucheza mchezo wowote halafu leo unamuingiza akashikilie bomba ilikuwa jambo la hatari sana.

Kumuingiza kiungo Abdallah Hamis ambaye naye hakuwahi kucheza hata siku moja ilikuwa ngumu kumeza, kupaki basi kuanzia dakika ya 60 ni uamuzi mgumu ambao ulitufanya wengi tushike bomba.

Kujaza mabeki saba nyuma haijawahi kutokea kwa muda mrefu sana, maamuzi magumu ya Benchika ambaye anafanana kwa sura na Bongo Zozo.
 
Alitaka kasi zaidi kwenye kujilinda na kushambulia kwa counter attacking japokuwa John bocco muda mwingi alikuwa off position team inapokuwa na mpira na kushindwa kuendana na kasi nadhani chilunda angeingia badala ya bocco mambo yangekuwa tofauti leo pale kwa mkapa.
 
Kocha bora hafanyi majaribio bila fact. Inawezekana huko mazoezini kuna vitu anaviona ambavyo vinampa confidence ya kuwapanga
Muda ni lesson hatari sana kwa jambo lolote lile, tuendelee kusubiri muda (Mwalimu) tujue ni mihemuko tokana na ushindi wa mechi ya Makolokolo SC vs Wydad Casablanca au ni kweli sifa anazopewa Kocha mpya.
 
Muda ni lesson hatari sana kwa jambo lolote lile, tuendelee kusubiri muda (Mwalimu) tujue ni mihemuko tokana na ushindi wa mechi ya Makolokolo SC vs Wydad Casablanca au ni kweli sifa anazopewa Kocha mpya.
Kila mtu ashinde mechi zake.

Hamjasema bado.
 
Hata mechi 5 tu Simba SC haijacheza na Kocha mpya tayari mmeridhika, kweli Makolokolo hamna tofauti na Watoto wadogo kudanganyika kirahisi
Ni kweli sisi simba watu kadhaa kadhaa ni makolokolo, ila nyie pale jangwani wenye akili kichwani wanajulikana kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom