Ben Mkapa ampigia Pinda debe kiaina

Ben Mkapa ampigia Pinda debe kiaina

Kasent

Member
Joined
Sep 27, 2011
Posts
57
Reaction score
7
Mwanza. Rais mstaafu, Benjamini Mkapa amempigia debe Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kiana akisema ni kiongozi anayekubalika kwa wananchi, hivyo wananchi wamuunge mkono kwenye nafasi yake ya sasa.

Pia, Mkapa amesema uadilifu wa Pinda ndiyo chanzo cha watu kumwamini na kumkubali kutokana na kazi nzuri anayoifanya serikalini, hivyo ni kiongozi mfano wa kuigwa.

Mkapa alitoa kauli hiyo juzi usiku wakati akihitimisha harambee ya kuchangia fedha za mradi wa Mkapa Fellows kwa ajili ya kusaidia kuboresha sekta ya afya vijijini iliyoendeshwa na Pinda. Harambee hiyo iliandaliwa na Taasisi ya Benjamini William Mkapa HIV/AIDS.

"Naomba niwaambie ndugu zangu, kiongozi mzuri ni yule mwadilifu ambaye anakubalika kwa wananchi, hivyo naomba mumuunge mkono Pinda katika kazi yake ya sasa. Nasema hivi kwa sababu wote mmejionea wenyewe kazi aliyoifanya Waziri Mkuu hapa ni kubwa. Tumefanya harambee na watu wameitikia kumuunga mkono, hivyo ni wazi kwamba anakubalika na kuaminiwa na watu," Mkapa alisema alipopewa nafasi ya kutoa neno la shukrani katika hafla hiyo.

Kauli hiyo ya Mkapa imekuja siku moja baada ya vyombo vya habari kumtaja Pinda kwamba ni miongoni mwa wanaCCM wanaojipanga kuwania urais kupitia chama hicho.

Habari hizo zimedai kuwa tayari Pinda ameanza kuzungumza na makundi mbalimbali kuhusu nia hiyo, wakiwamo wanaCCM aliokutana nao mjini Mwanza juzi.

Kabla ya kuanza kwa harambee hiyo, Pinda alieleza jinsi alivyooteshwa kuwa harambee ingefanikiwa na ikawa hivyo.

"Sisi watoto wa Kifipa huwa tukioteshwa jambo linakuwa la kweli na mimi usiku huu nilioteshwa kuwa harambee hii itafanikiwa kwa kiasi kikubwa na kweli imefanikiwa," alisema Pinda huku akicheka.

Akizungumzia kuhusu uchangiaji fedha kwa ajili ya mradi huo, Pinda alisema licha ya mafanikio makubwa kwenye sekta ya afya, bado kuna changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni maambukizi ya Ukimwi kitaifa kuwa asilimia tano, huku vifo vya kina mama wajawazito kitaifa vikiwa juu kwa kina mama 454 kupoteza maisha kati ya wazazi 100,000.

Alisema Tanzania ina upungufu wa watumishi wa afya kwa asilimia 52, jambo ambalo si la kuridhisha... "Katika Kanda hii (ya Ziwa), asilimia 45 ya wanawake ndiyo wanaojifungua kwenye vituo vya afya na wajawazito 500 hufariki kila mwaka, maambukizi ya Ukimwi ni asilimia 4.8 na upungufu wa watumishi ni asilimia 39, hivyo kuna changamoto kubwa inayotakiwa kufanyiwa kazi," alisema Pinda.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko huo, Dk Ellen Senkoro alisema Kanda ya Ziwa ni moja ya maeneo yaliyonufaika kupitia miradi ya taasisi yake ikiwamo kuajiri watumishi mbalimbali wa kuhudumia miradi yake.

Chanzo: Mwananchi

 
Huyu huyu Mzee nasikia alishawai kumuita wassira akiwa Mwanza na kumuambia achukue fomu ya kugombea uraisi atamsapoti leo yuko kwa pinda tena sasa ajawa na msimamo.
 
Mwanza. Rais mstaafu, Benjamini Mkapa amempigia debe Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kiana akisema ni kiongozi anayekubalika kwa wananchi, hivyo wananchi wamuunge mkono kwenye nafasi yake ya sasa.

Pia, Mkapa amesema uadilifu wa Pinda ndiyo chanzo cha watu kumwamini na kumkubali kutokana na kazi nzuri anayoifanya serikalini, hivyo ni kiongozi mfano wa kuigwa.

Mkapa alitoa kauli hiyo juzi usiku wakati akihitimisha harambee ya kuchangia fedha za mradi wa Mkapa Fellows kwa ajili ya kusaidia kuboresha sekta ya afya vijijini iliyoendeshwa na Pinda. Harambee hiyo iliandaliwa na Taasisi ya Benjamini William Mkapa HIV/AIDS.

“Naomba niwaambie ndugu zangu, kiongozi mzuri ni yule mwadilifu ambaye anakubalika kwa wananchi, hivyo naomba mumuunge mkono Pinda katika kazi yake ya sasa. Nasema hivi kwa sababu wote mmejionea wenyewe kazi aliyoifanya Waziri Mkuu hapa ni kubwa. Tumefanya harambee na watu wameitikia kumuunga mkono, hivyo ni wazi kwamba anakubalika na kuaminiwa na watu,” Mkapa alisema alipopewa nafasi ya kutoa neno la shukrani katika hafla hiyo.

Kauli hiyo ya Mkapa imekuja siku moja baada ya vyombo vya habari kumtaja Pinda kwamba ni miongoni mwa wanaCCM wanaojipanga kuwania urais kupitia chama hicho.

Habari hizo zimedai kuwa tayari Pinda ameanza kuzungumza na makundi mbalimbali kuhusu nia hiyo, wakiwamo wanaCCM aliokutana nao mjini Mwanza juzi.

Kabla ya kuanza kwa harambee hiyo, Pinda alieleza jinsi alivyooteshwa kuwa harambee ingefanikiwa na ikawa hivyo.

“Sisi watoto wa Kifipa huwa tukioteshwa jambo linakuwa la kweli na mimi usiku huu nilioteshwa kuwa harambee hii itafanikiwa kwa kiasi kikubwa na kweli imefanikiwa,” alisema Pinda huku akicheka.

Akizungumzia kuhusu uchangiaji fedha kwa ajili ya mradi huo, Pinda alisema licha ya mafanikio makubwa kwenye sekta ya afya, bado kuna changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni maambukizi ya Ukimwi kitaifa kuwa asilimia tano, huku vifo vya kina mama wajawazito kitaifa vikiwa juu kwa kina mama 454 kupoteza maisha kati ya wazazi 100,000.

Alisema Tanzania ina upungufu wa watumishi wa afya kwa asilimia 52, jambo ambalo si la kuridhisha... “Katika Kanda hii (ya Ziwa), asilimia 45 ya wanawake ndiyo wanaojifungua kwenye vituo vya afya na wajawazito 500 hufariki kila mwaka, maambukizi ya Ukimwi ni asilimia 4.8 na upungufu wa watumishi ni asilimia 39, hivyo kuna changamoto kubwa inayotakiwa kufanyiwa kazi,” alisema Pinda.

Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko huo, Dk Ellen Senkoro alisema Kanda ya Ziwa ni moja ya maeneo yaliyonufaika kupitia miradi ya taasisi yake ikiwamo kuajiri watumishi mbalimbali wa kuhudumia miradi yake.

Chanzo: Mwananchi

Ametoa maoni yake kama mtanzania na aliyekuwa mkuu wa nchi huenda kuna jambo kaliona
 
Kwenye hiyo harambee "mamvi" na "marafiki" zake hawakualikwa? hawakuchangia? Au bado anatumikia "kifungo"?
 
Najaribu kupata picha jinsi Membe, Lowasa, Makamba na wengine walivyovimba baada ya kusikia utolewaji wa hiyo kauli........wanatamani wangeitwa wao kwenye hiyo Harambee......mpaka wakati ukifika tutasikia mengi, tuombe uzima.
 
Kwani yeye alikua msafi hata apige debe?tuachiwe kazi sisi wananchi tuchague Lowassa
 
hyu albinafssha migod miaka 100 anaongea nn xaxa,yan wanatia hacra magamba,hebu fkria mgod wa mwadui upo kishapu shy lakn hyo wilaya haina lami,maji ya uhakika,umeme sehem chache 2 upo,et ndo sehem yanapatkana madn admu dunian.pumbavu xana magamba nyie n wakolon weuc
 
hyu albinafssha migod miaka 100 anaongea nn xaxa,yan wanatia hacra magamba,hebu fkria mgod wa mwadui upo kishapu shy lakn hyo wilaya haina lami,maji ya uhakika,umeme sehem chache 2 upo,et ndo sehem yanapatkana madn admu dunian.pumbavu xana magamba nyie n wakolon weuc

Dogo uandishi gani huu wa xx?
 
Prof. Anna tibaijuka ndo habari ya mjini urais 2015

Piga ua watanzania twamuhitaji prof. Anna tibaijuka ndo awe rais 2015 na co vinginevyo
umelipwa shilingi ngapi na huyo mama? maana uko bize kumpigia debe ila cha kushangaza ni kwamba hujagundua hakuna hata mmoja anayeku-support humu zaidi ya wewe mwenyewe kwa kutumia ile ID ingine inayoishia kama sio kuanzia na LEO.
tumia kichwa kufikiria sio kufugia nywele tu.
 
Sasa ni zamu ya mkatoliki hatuhitaji mkristo mwengine yeyote .
 
Yawezekana ni zamu ya Mkatoliki kweli lakini Pinda na Membe no way,Labda Dr Slaa!
 
Pinda a cha uongo hakuna cha ndoto Uraisi huuwezi Mkuu uwaziri Mkuu umekushinda hats Jairo ulimwogopa
 
Huyu huyu Mzee nasikia alishawai kumuita wassira akiwa Mwanza na kumuambia achukue fomu ya kugombea uraisi atamsapoti leo yuko kwa pinda tena sasa ajawa na msimamo.

Kumbe angefanyaje wakati mh.Pinda alikuwa hajaoteshwa? Kama alioteshwa harambee kufanikiwa lazima alioteshwa pia kuwa atangaze nia mafanikio ni makubwa. Alipomweleza Mkapa kuwa wao vijana wa kifipa wakioteshwa jambo lolote hufanikiwa kwa asilimia kubwa na huku ameshashuhudia mafanikio ya harambee ulitegemea amjibu nini Pinda zaidi ya kumpamba? Sijui itakuwaje nae mh. Membe atakapooteshwa. Sasa tutakuwa na maraisi wangapi? Ninachoshukuru ni kuwa ameoteshwa na sio kutabiriwa.
 
Ametoa maoni yake kama mtanzania na aliyekuwa mkuu wa nchi huenda kuna jambo kaliona
infact Pinda anaweza ametenda mazuri mengi sana na kama yapo mabaya ni ubinadamu na yako machache sana kwakua yeye si malaika. alikosea kama binadamu tusihukumu mabaya yake tu. najua mnajua kua anayo mema zaidi ya mia ya mabaya ninkiongozi anayejua wajibu wake ni hakika anajua kwakua ana hekima ni mtaratibu na ni kiongozi wa kuigwa na wala Mkapa hajakosea amenena sahihi kusema na kua Pinda ni muadilifu sana, mnyenyekevu na anayo pia hekima mimi na watanzania wengi pia najua ama tunajua anaweza kua rais na akabadili maisha ya watanzania.. ikiwezekana apewe adhihirishe hilo na uwezo wake.. viva Pinda
 
Back
Top Bottom