DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Bei za mafuta ya petroli na dizeli zitakazotumika Oktoba mwaka huu nchini zimeendelea kupungua kwa kiwango tofauti ikilinganishwa na zilizokuwepo mwezi uliotangulia, huku upande wa mafuta ya taa ukiendelea kusalia vilevile.
Bei hizi zinapungua nchini wakati ambao kumekuwa na ongezeko katika soko la dunia kwa asilimia 2.80 kwa mafuta ya petroli, asilimia 3.65 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 3.57 kwa mafuta ya taa.
Pia taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) inaonyesha kuwa licha ya bei kikomo kupanda katika soko la dunia, gharama za kuagiza mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam zimepungua kwa wastani wa asilimia 1.95 kwa mafuta ya petroli.
Kwa upande wa dizeli zimeongezeka kwa asilimia 2.39 na hakuna mabadiliko kwa mafuta ya taa. Katika Bandari ya Tanga zimeongezeka kwa asilimia 6.38 kwa mafuta ya petroli na dizeli na katika Bandari ya Mtwara zimeongezeka kwa asilimia 0.49 kwa mafuta ya petroli na hakuna mabadiliko kwa mafuta ya dizeli.
Hali hiyo inafanya bei ya jumla sasa lita moja ya mafuta inayopitia katika bandari ya Dar es Salaam kuuzwa kwa Sh2,720 kutoka Sh2,807 iliyotumika Septemba mwaka huu, dizeli itanunuliwa kwa Sh2,704 kutoka Sh2,754 iliyokuwapo Septemba mwaka huu
Hata hivyo, kwa watumiaji wa mafuta ya taa yanayopitia katika bandari hiyo watalazimika kuendelea kutumia bei ya Sh2,774 iliyokuwapo Septemba mwaka huu.
Bei hizi zinapungua nchini wakati ambao kumekuwa na ongezeko katika soko la dunia kwa asilimia 2.80 kwa mafuta ya petroli, asilimia 3.65 kwa mafuta ya dizeli na asilimia 3.57 kwa mafuta ya taa.
Pia taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) inaonyesha kuwa licha ya bei kikomo kupanda katika soko la dunia, gharama za kuagiza mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam zimepungua kwa wastani wa asilimia 1.95 kwa mafuta ya petroli.
Kwa upande wa dizeli zimeongezeka kwa asilimia 2.39 na hakuna mabadiliko kwa mafuta ya taa. Katika Bandari ya Tanga zimeongezeka kwa asilimia 6.38 kwa mafuta ya petroli na dizeli na katika Bandari ya Mtwara zimeongezeka kwa asilimia 0.49 kwa mafuta ya petroli na hakuna mabadiliko kwa mafuta ya dizeli.
Hali hiyo inafanya bei ya jumla sasa lita moja ya mafuta inayopitia katika bandari ya Dar es Salaam kuuzwa kwa Sh2,720 kutoka Sh2,807 iliyotumika Septemba mwaka huu, dizeli itanunuliwa kwa Sh2,704 kutoka Sh2,754 iliyokuwapo Septemba mwaka huu
Hata hivyo, kwa watumiaji wa mafuta ya taa yanayopitia katika bandari hiyo watalazimika kuendelea kutumia bei ya Sh2,774 iliyokuwapo Septemba mwaka huu.