Bei ya vitunguu sokoni ipo vipi?

Bei ya vitunguu sokoni ipo vipi?

Nimekuelewa.
Lakini hujanijibu.
Ni kwamba vitunguu unachukulia shambani maana yake wanachambua wanapakia kwa gunia unaona au ubakuta tayari gunia wanakuambia hii grade 2 sh kadhaa.
Kazi ya mkulima inaishia kwenye kukata kitunguu kuanzia kuchambua kugonga na kupakia hiyo ni kazi ya mnunuzi

Huwa magari yanaingia mpaka shambani na ikiwa kuwa gari haliingii mnunuzi na mkulima watachangia hasara ya kupeleka kitunguu kwenye gari
 
Kazi ya mkulima inaishia kwenye kukata kitunguu kuanzia kuchambua kugonga na kupakia hiyo ni kazi ya mnunuzi

Huwa magari yanaingia mpaka shambani na ikiwa kuwa gari haliingii mnunuzi na mkulima watachangia hasara ya kupeleka kitunguu kwenye gari
Ahsante sana kwa maelezo haya.
 
Cha msingi uwe na dalali wa kukutafutia kitunguu kila gunia utampa 3000
Ahsante.
Nina swali mfano unataka kuchukua gunia 10. Maana yake hizo gunia hakuna uwezo wa kukodi gari nzima. Suala la usafiri kutoa shamba mpaka main road kusubiria gari inakuwaje?
 
Ni shambani ndo wanachukulia mara nyingi , ingawa kwa Arusha kuna soko la vitunguu linaitwa Kilombero , sasa huko ni Wakenya na wenye mitaji mikubwa ndo wanaenda chukua mzigo , Ila ukitaka kupata mzigo nzuri nenda shambani Mang'ola

Kuhusu suala la kuchambua ni gharama ya mnunuzi kiufupi gharama ziko hivi ( vifungashio + gharama ya vibarua kuchambua , kulalia kwenye magunia , kupandisha kwenye gari + gharama ya usafiri + ushuru ) .
Siku hizi hakuna wakenya wanaoingia soko la kilombero kununua vitunguu, wakenya wanaenda shambani moja kwa moja mang'ola kununua, hapa kilombero wanunuzi ni wamama na wafanyabiashara wengine wanaopeleka kwenye masoko ya ngaramtoni, usa river, sadala nk. pamekua pa tofaut sana kilombero sio kama zamani biashara ilikua inafanyika kwa cash siki hizi ni mkopo unapeleka mzigo pesa utaipata baada ya wiki moja au zaidi.
 
Ahsante.
Nina swali mfano unataka kuchukua gunia 10. Maana yake hizo gunia hakuna uwezo wa kukodi gari nzima. Suala la usafiri kutoa shamba mpaka main road kusubiria gari inakuwaje?
Tractor gunia moja huwa ni 2000
 
  • Thanks
Reactions: amu
Anhaa basi nilikuwa sijui , nina siku nyingi sijaingia humo sokoni
nilikua hapo jumamosi grade one ilikua 110,000 mpk 120,000
grade 2 ilikua 90,000 mpk 100,000 jana na leo sijaenda huko nijue hali ya soko. sema sasa hivi huenda itapanda tena maana wakenya wameshafungua mipaka ya wao kuweza kusafiri huenda wakaanza kuja kwa wingi huko mashambani na bei ikapanda. maana hapa kilombero 90% ya kitunguu yote inatoka mang'ola kuna siku wanashusha hadi gari 6
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom