Bei ya pamba inaumiza

Bei ya pamba inaumiza

Ok9

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2013
Posts
4,556
Reaction score
4,162
Naomba kilio hiki kifike mamlaka husika.
Mwaka juzi kilo ya pamba tuliuza kwa 1200
Mwaka jana tuliuza kwa 1100
Mwaka huu bei elekezi ni 1200.

Naomba mtambue kuwa msimu ulikuwa mbaya sana.
Hapakuwa na mavuno kwa upande wa mazao ya kilimo kutokana na kukosekana mvua.
Ndiposa tukalima kwa wingi pamba kama zao la biashara la kutukomboa kwa kuwa linavumilia sana ukame. Lakini ukame nao ulizidi hadi na lenyewe likashindikana.

Shamba la kutoa tani 1 limetoa kilo 300 tu.

Naomba angalau bei iwe 2,000 kwa kilo
 
Poleni sana.
Ila msitegemee rais afanye maamuzi kama ya korosho maana anajua kilichotokea
 
Ngoja labda tusubiri maybe Serikali itanunua yenyewe kama ilivyofanya kwa zao la KOROSHO
 
Ni vizuri mkachukua hata hicho kidogo,kuna wenzenu huku wameshapata magonjwa ya moyo na kisukari na wengine tumeshazika sababu ya kupigwa za uso kwenye korosho.
 
Naomba kilio hiki kifike mamlaka husika.
Mwaka juzi kilo ya pamba tuliuza kwa 1200
Mwaka jana tuliuza kwa 1100
Mwaka huu bei elekezi ni 1200.

Naomba mtambue kuwa msimu ulikuwa mbaya sana.
Hapakuwa na mavuno kwa upande wa mazao ya kilimo kutokana na kukosekana mvua.
Ndiposa tukalima kwa wingi pamba kama zao la biashara la kutukomboa kwa kuwa linavumilia sana ukame. Lakini ukame nao ulizidi hadi na lenyewe likashindikana.

Shamba la kutoa tani 1 limetoa kilo 300 tu.

Naomba angalau bei iwe 2,000 kwa kilo
Halafu unajua kuwa Nguo za pamba ndiyo zenye bei ghali zaidi. Shati la pamba jipya si chini ya 40,000/= Tshs. Halafu kilo moja ya pamba inatoa mashati zaidi ya mawili. Angalia sasa!!!
 
Ni vizuri mkachukua hata hicho kidogo,kuna wenzenu huku wameshapata magonjwa ya moyo na kisukari na wengine tumeshazika sababu ya kupigwa za uso kwenye korosho.
Hahaha uzuri wana sehemu ya kujifunza
 
Halafu unajua kuwa Nguo za pamba ndiyo zenye bei ghali zaidi. Shati la pamba jipya si chini ya 40,000/= Tshs. Halafu kilo moja ya pamba inatoa mashati zaidi ya mawili. Angalia sasa!!!
l

Ndo hapo tuone umuhimu wa viwanda vya nguo ili tuepukane na mitumba
 
Msilime tena pamba, wazee wa kichaga walivyoona zao la kahawa linawasumbua tu halina tija walifyeka mikahawa yoe wakapana migomba wakatulia tuli na hakuna alieambiwa kwa nini hulimi kahawa.
 
Back
Top Bottom