PreGE2025 BAWACHA: CHADEMA bado ipo imara, kwenye majimbo 30, wameondoka viongozi wanne tu

PreGE2025 BAWACHA: CHADEMA bado ipo imara, kwenye majimbo 30, wameondoka viongozi wanne tu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Just Pray

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
2,142
Reaction score
4,779
Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo- CHADEMA (BAWACHA) Kanda ya Kati Emmy Kibatala amesema kuhama kwa baadhi ya viongozi wa chama hicho hakujawateteresha hasa kuelekea uchaguzi mkuu ambapo amedai watashiriki ikiwa mifumo ya uchaguzi itawekwa sawa

Akizungumza katika Baraza la Mashauriano Mkoa wa Morogoro lililofanyika siku ya Jumatatu, Makamu Mwenyekiti huyo amesema kwenye kanda hiyo yenye majimbo 30 viongozi waliohama CHADEMA na kujiunga na vyama vingine ni wimbi tu linalopita na kanda iko imara kukilinda chama chao

Aidha Emmy Kibatala amesema katika kuendelea kuijenga kanda ya kati, BAWACHA wamepanga kuanza mikutano kuanzia Juni 4, 2025 ili kujenga uelewa kwa Watanzania juu ya dhamira ya chama hicho.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

BA
 
Back
Top Bottom