Chademakwanza
JF-Expert Member
- Jun 11, 2014
- 6,346
- 1,872
Baraza la vijana wa CHADEMA Taifa,jana waliufanya mji wa Bukombe kusimama kwa muda wa masaa Matano,walipo kuwa wakiingia Bukombe Viongozi hao machachari walipokelewa kwa msafara mkubwa wa Magari na Pikipiki zilizopambwa kwa bendera za CHADEMA hadi katika viwanja vya Mkutano.
Mkutano ulianza majira ya saa10 za jioni,ambapo uwanja ulilipuka kwa Shangwe na vigelegele huku sauti zikisikia kwa mbali,kwa namna Viongozi hao walivyo jipanga.Katika msafara huo Yupo Katibu Mkuu wa BAVICHA Julius Mwita,Naibu Katibu Mkuu Zanziba Omary Nassoro na Katibu Mwenezi wa BAVICHA Taifa Edward Simbeye.
Mashambuli yenye hoja yaliofanywa na viongozi hao,yaliwafanya wananchi wa BUKOMBE kupiga kelele na kusema ukombozi umekuja sasa,kilicho wavutia zaidi wananchi ni jinsi Katibu Mkuu wa Baraza hilo pamoja na Mwenezi wake wanavyo shambulia jukwaa hata kupelekea kupewa majina ya Washambuliaji hatari wa Fc Barca yani MESSI na NEYMAR.
Baada ya mkutano kumakizika,gari la viongozi hao lilisukumwa mpk katika Hotel waliyofikia kwaajili ya kupumzika.
Tathmini ya wananchi baada ya mkutano kwisha,ni kwamba vijana wa BAVICHA wameweza kujenga hoja na kuonesha muelekeo wa Taifa,na wameufunika mkutano wa Nape na Kinana kwakuwa hawakuwa na hoja bali ni matusi na Maigizo tu yaliotawala jukwaani.
Maswali yaliyobaki vichwani kwa Wananchi,ni kwamba kama vijana hawa wanauwezo kiasi hiki je wakubwa wao itakuaje????
Mkutano ulianza majira ya saa10 za jioni,ambapo uwanja ulilipuka kwa Shangwe na vigelegele huku sauti zikisikia kwa mbali,kwa namna Viongozi hao walivyo jipanga.Katika msafara huo Yupo Katibu Mkuu wa BAVICHA Julius Mwita,Naibu Katibu Mkuu Zanziba Omary Nassoro na Katibu Mwenezi wa BAVICHA Taifa Edward Simbeye.
Mashambuli yenye hoja yaliofanywa na viongozi hao,yaliwafanya wananchi wa BUKOMBE kupiga kelele na kusema ukombozi umekuja sasa,kilicho wavutia zaidi wananchi ni jinsi Katibu Mkuu wa Baraza hilo pamoja na Mwenezi wake wanavyo shambulia jukwaa hata kupelekea kupewa majina ya Washambuliaji hatari wa Fc Barca yani MESSI na NEYMAR.
Baada ya mkutano kumakizika,gari la viongozi hao lilisukumwa mpk katika Hotel waliyofikia kwaajili ya kupumzika.
Tathmini ya wananchi baada ya mkutano kwisha,ni kwamba vijana wa BAVICHA wameweza kujenga hoja na kuonesha muelekeo wa Taifa,na wameufunika mkutano wa Nape na Kinana kwakuwa hawakuwa na hoja bali ni matusi na Maigizo tu yaliotawala jukwaani.
Maswali yaliyobaki vichwani kwa Wananchi,ni kwamba kama vijana hawa wanauwezo kiasi hiki je wakubwa wao itakuaje????