Basi la Moro Best limepata ajali

Basi la Moro Best limepata ajali

ngonani

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2012
Posts
1,366
Reaction score
598
Basi la Moro best likitokea Dodoma kwenda Dar limepata ajali mbaya sana muda huu eneo la Kibaigwa, ni mwendo kasi na imekoswa koswa na maroli na basi kabla ya kutumbukia kwenye mtaro, maiti wawili tayari wametolewa, majeruhi ni wengi mno na huenda idadi ya waliokufa ikawa kubwa zaidi, tuko katika jitihada za kunasua watu walionasa.
Picha baadae.
 
Jitahidi ufanye mawasiliano na vyombo husika ili kutoa msaada wa kitaalamu na wa haraka.
 
Poleni sana wafiwa na majeruhi mpone fasta,kama kawaida uchunguzi utafanywa na geshi ra porish then hakuna kipya kitakachoendelea.wabarkatoum.
 
poleni sana majeruhi wote na Mungu azilaze roho za marehem wote mahali pema
 
Dah..poleni sana , naona mwisho wa mwaka umeanza mapema sana.
 
Moro best again! Na sababu ni ile ile mwendo kasi. Haya mabasi sasa yatazamwe kwa upana.
Poleni sana wafiwa na majeruhi
 
Gari za kampuni hii si ndo imetoka kuua juzi tena?
 
Tuyasusie kama Malaysian airlines ilivyosusiwa. juzi ndege ya watu mia tatu ilikua na watu wawili.
 
Hee! kwa Mara nyingine tena ndani ya miezi miwili tu? Lazima Kuna cha kuchunguzwa ndani ya hii kampuni ya Moro Best
 
Tuyasusie kama Malaysian airlines ilivyosusiwa. juzi ndege ya watu mia tatu ilikua na watu wawili.



Hivi hawa wamiliki wanaingiza ushirikina humo kwenye beiahsara zao au ni nini hasa kinafanyikia, kwakweli sasa ifike mahali tuwe na umoja ili tuyamalize haya makampuni yanayowamaliza raia wasio na hatia, na dawa pekee ni kuyasusia kama usemavyo

RIP Waliofariki
Mungu awape uponyaji majeruhi
 
Pole kwa wahanga wote!
Tupiamo ki snepu mkuu
 
Mungu awajalie majeruhi wapone,na azilaze roho za marehemu mahala Pena peponi.Amen.
 
Ee Mungu zilaze mahali pema roho za waliotangulia mbele ya haki na waponye majeruhi. Siyo Kibaigwa ajali imetokea Kati ya Gairo na Magubike
 
Nipo safarin naenda Dodoma,basi la Moro Best Limepinduka watu wamejeruhiwa hakuna aliyekufa.
Basi lilikua linatokea Mpwapwa,mashushuda wanasema lilikua lina overtake likakutana na gari lingine uso kwa uso ndo dereva akatanua nje ya barabara likapinduka,baadh ya majeruh wamepandishwa kwenye basi nililopanda wanarud eneo ambalo wanaweza kupata matibabu.hili eneo ni kilometa chache kufika Dumila kama unaelekea Dodoma
 
Back
Top Bottom