Basi la Kisbo Safari laua wawili Singida

Basi la Kisbo Safari laua wawili Singida

mdudu

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2014
Posts
7,029
Reaction score
10,025
Basi la kampuni ya KISBO SAFARI,lenye namba T534 CHX,lilokuwa likitoka Dar kwenda Mwanza,limepinduka vibaya kufuatia tairi la mbele kupasuka likiwa kwenye mwendo kasi,na kuua watu wawili papo hapo na wengine zaidi ya hamsini kujeruhiwa vibaya.

Ajali hiyo imetokea nje kidogo ya mji wa Ikungi mkoani Singida mida ya saa kumi na moja na nusu jioni ya leo.

Nimechelewa kupost maana simu yangu haina chaji na picha nashindwa kuziweka.

Chanzo ni mimi mwenyewe natoka Bukoba naenda Moro.
 
wakuu naomba tujiulize, hivi hiki kipande cha Singida-Manyoni mbona kina ajali za mfululizo kwa mabasi ya safari ndefu?
 
Ajali za barabarani hapa TZ ni zaidi ya ebola huko west africa.

Hiyo ni kweli kabisa, kila ajali utaambiwa mwendo kasi, sasa hao askari wa barabarani sijui wanafanya kazi gani, basi bovu askali wabovu barabara mbovu madeleva wabovu, full majanga. Jibu utawala wakizaifu.
 
Hii basi tu. Hebu niambieni, haya matairi na bust zake ni kutokana na barabara zetu au quality zake? Iwapo ni barabara mbovu, tunakimbilia wapi na ma spidi hayo? Kama ni quality, TBS wako wapi?
 
Iyo nikweli kabisa, kila ajari utaambiwa mwendo kasi sasa hao askari wa barabarani sijui wanafanya kazi gani, basi bovu askali wabovu barabara mbovu madeleva wabovu, full majanga. Jibu utawala wakizaifu
Na mwenye mali anaangalia wapi? Hivi kuna bima ya kuwalipa wanaoadhirika ktk ajali kama hizi?
 
Da poleni sana,sisi 2lisha wahi nusurika ajali ya basi 2kielekea mwanza,baada ya tairi la mbele kupasuka mita chache kabla ya kufika singida mjini.
Nadhani ajali nying zinazotokea mkoa wa singida zinachangiwa na upepo pia
 
Hii basi tu. Hebu niambieni, haya matairi na bust zake ni kutokana na barabara zetu au quality zake? Iwapo ni barabara mbovu, tunakimbilia wapi na ma spidi hayo? Kama ni quality, TBS wako wapi?

Tairi mchina anakula na TBS
 
Hii basi tu. Hebu niambieni, haya matairi na bust zake ni kutokana na barabara zetu au quality zake? Iwapo ni barabara mbovu, tunakimbilia wapi na ma spidi hayo? Kama ni quality, TBS wako wapi?

Mkuu mabasi ya bongo nimabovu sana kuanzia chini mpaka juu, haalafu yanaachwa yakimbie speed, wakati nchi zilizo endelea mabasi mapya na na barabara nzuri lakini yanaenda kwa masaa malumu, yaani unakua kwenye basi hata wasi wasi huna
 
Hiyo Kisbo ni gari ya kahama wiki iliyopita nimeipandia dom kuja dar aisee ule mwendo wake ilikua kama ndege ya ardhini' jamaa ilikua ni ku over take tu hakuna gari iliyompita
 
Na mwenye mali anaangalia wapi? Hivi kuna bima ya kuwalipa wanaoadhirika ktk ajali kama hizi?

Yaani nchi yetu ni yaajabu sana magari yana bima yabarabarani lakini watu wakipata ajari ata wakatike viungo vyote hawalipwi sasa sijui mtu ataishi vp naiyo bima inakazi gani, kazi yao kufuga vitambi ya dhambi tu
 
Hiyo KISBO ni gari ya KAHAMA. Wiki iliyopita nimeipandia Dom kuja Dar aisee ule mwendo wake ilikua kama ndege ya ardhini' jamaa ilikua ni ku over take tu hakuna gari iliyompita

Kuna yule mwenzeka wa rangi ya njano anaitwa LEINA TOUR naye anaenda KAHAMA. Hawa jamaa gari zao zinatembea ile mbaya.
 
Kuna yule mwenzeka wa rangi ya njano anaitwa LEINA TOUR naye anaenda KAHAMA. Hawa jamaa gari zao zinatembea ile mbaya.
Leina tours jana imepata ajali dar, eneo la kimara bucha likiwa inatokea kahama. Ogopa sana Kisbo safari, leina tours na city boy yote ya kahama, huwa yanaongozana na speed zake ni balaa...abiria unaweza tokwa haja ndogo hvi hvi
 
Back
Top Bottom