Tony Laurent
JF-Expert Member
- Jan 5, 2011
- 6,392
- 8,294
Wiki iliyopita nilisafiri na basi la Kilimanjaro express kutoka Dar kwenda Moshi. Mkanda wa siti niliyokaa pamoja na jirani yangu ilikuwa mibovu. Mikanda ipo lakini haiwezi kufunga kwa kutumia lock. Ilibidi nifunge kinyeji kama nafunga kamba. Nikahisi labda ni bahati mbaya watarekebisha. Jana nikawa narudi Dar kutoka Moshi kwa Kilimanjaro Express basi no. T 830 AXR. Basi zima siti hazikuwa na mikanda. Cha ajabu ni kwamba askari wa usalama barabarani walikuwa wanalikagua njiani, hakuna hata mmoja aliyehoji upungufu huo. Tena kuna askari mmoja alipanda Chalinze akashuka Kibaha, hakuhoji juu ya viti kukosa mikanda ya usalama. Tafadhali wahusika wote wa jambo hili, kuanzia wamiliki wa hii kampuni na askari wa usalama barabarani, timizeni wajibu wenu ili kurekebisha kasoro hii.