BASI LA BURUDANI LAUA
Basi la abiria la BURUDANI lenye namba ya usajili T 158 BXG (amabalo picha yake inaonyeshwa) linalofanya biashara ya usafierishaji wa abiria kati ya Lushoto na Dar es Salaam, limepata ajali na kusababisha kifo cha mtu mmoja papo hapo na majeruhi watano ambao hali zao ni mbaya sana, huku wengine wakipata michubuko na majeraha madogomadogo. Ajari hiyo iliyosababishwa na kugongana kwa magari mawili Basi la Burudani na lory scania lenye namba ya usajili T 150 ATU imetokea leo (09/10/2013) mnamo majira ya saa tatu asubuhi katika kijiji cha kwedikwazu mbele kidogo ya kabuku. Kwa maelezo ya mashuhuda ajari hiyo ilisababishwa na lory scania ambalo lilizima breki ghafla na kusimama kwenye kona pasipo kutoa ishara yoyote kwa dereva wa basi la Burudani ambalo lilikuwa likifukuziana na lory hilo kwa nyuma wakiachana kwa hatua chache. Kutokana na kuzima breck ghafla huko, ilimfanya dereva wa basi husika kushindwa kuzima breki ghafla na hivyo kujikuta akigonga gari hilo kwa nyuma na hivyo kusababisha matairi ya mbele yote kutoka na hivyo kuseleleka.
Dereva wa basi aliyejulikana kwa jina Godi alikimbia baada ya tukio kutokea; na hivyo kukosa maelezo yake. Hatahivyo, dereva wa lory alipotafutwa kutoa maelezo hakuonekana kwani naye alikimbia baada ya ajali hiyo. Majeruhi waliokuwa mahututi, wote walipelekwa kwenye hospitali Korogwe mjini kwa ajili ya huduma ya kwanza na matibabu, na mwili wa marahemu ulipelekwa kuhifandhiwa kwenye hospitali mjini korogwe. Hatahivyo, baada ya ukaguzi wa polisi wa barabarani, abilia waliendelea na safari huku wengine wakihairisha safari zao.
Awali ya ajali hiyo, kulitokea ajali mbili kwa nyakati tofauti kwenye eneo husika zikihusisha malory ya kubeba mizigo manne amabyo pia madereva wake hawakupatikana kutoa maelezo yao; Mapolisi wa barabarani walipo ulizwa juu ya ajari hizo hawakuwa tayari kuzungumzia ajali hizo kwa kusema kuwa walikuwa wamechanganyikwa kutokana na mfululizo wa ajali hizo katika eneo moja ila kwa nyakati toafauti.