Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Bashungwa acha uongo wewe! Hiyo Switzerland unajua vizuri kweli! Uchawa unakusumbua sana
Vumbi limejaa pale, wakazi wengine hata maji hakuna
======================
Mgombea wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Karagwe Mkoani Kagera na Waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania Innocent Bashungwa amesema ndani ya miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wilaya ya Karagwe imekuwa kama nchi ya Switzerland kutokana na ujenzi wa miradi mikubwa ya maendeleo pamoja na miundombinu ya barabara za Viwango vya lami pamoja na taa zake.
Wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu za Mgombea wa nafasi ya Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Viwanja vya Bashungwa, Kayanga, Karagwe leo Jumatano Oktoba 15, 2025, Bashungwa ameyataja baadhi ya mafanikio kuwa ni pamoja na ujenzi wa shule mpya 5 za Msingi pamoja na madarasa mapya 201, vyote vikigharimu Bilioni 5.5.
Vumbi limejaa pale, wakazi wengine hata maji hakuna
======================
Mgombea wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Karagwe Mkoani Kagera na Waziri wa mambo ya ndani wa Tanzania Innocent Bashungwa amesema ndani ya miaka minne ya Uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Wilaya ya Karagwe imekuwa kama nchi ya Switzerland kutokana na ujenzi wa miradi mikubwa ya maendeleo pamoja na miundombinu ya barabara za Viwango vya lami pamoja na taa zake.
Wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu za Mgombea wa nafasi ya Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye Viwanja vya Bashungwa, Kayanga, Karagwe leo Jumatano Oktoba 15, 2025, Bashungwa ameyataja baadhi ya mafanikio kuwa ni pamoja na ujenzi wa shule mpya 5 za Msingi pamoja na madarasa mapya 201, vyote vikigharimu Bilioni 5.5.