Bashe aanza kuwa kituko


KWA HIYO WALIPWE BILA KUFANYA KAZI? WALE KODI ZETU BILA KUWAJIBIKA? WATAKUWA NA TOFAUTI GANI NA MAKUPE? WABUNGE WA UPINZANI WANAGEUKA KUWA WANYONYAJI
 
Huyo bashe akili haijatuli itamchukua miaka mingi maana mzee MAKAMBA alimvuruga baada ya kumwambia si MTANZANIA. Mheshimiwa we ni kiongozi changia michango yako bila mihemko achana na hisia za mzee MAKAMBA
 
Akili za kiharamia, arudi tu kwao
 
Tuache kujitoa ufahamu hiv mbunge ambae hatoi hoja ye ni kuingia na kutoka alipwe ili iweje kwanza kakosea angesema posho zifutwe
 

Mbona kama wewe ndio kituko Zaidi manake umegoma kazi unataka ulipwe! Ebu kuwa serious bana ukisusa na kutoka pesa usipokee ikaongeze madawati mengine. Waombe waendelee kususa ili saving ifanyiwe kitu ingine manake hata wakiwa nje mambo si yanaenda tena kwa kasi Zaidi.
 
Siasa ina mambo yake....lakini nikuulize bro...kwani bungeni wameenda kufanya nini? Wanalipwa kwa activities gani? Tunaskia tu kususia hoja,mada...mijadala....mbona hatuwaskii wakikataa kulipwa hizo siku ambazo hawakueatumikia wananchi? Kiukweli hata kama ni wewe uko na genge lako la nyanya na muuzaji analeta mbwembwe....utafanyaje? Tuache ushabiki...ifike mahali tuseme ukweli...hata kama utatuumiza....Kususia kwenye siasa za Tanzania hakufanikishi jambo.
 
Labda ndio upeo wake ulipoishia. Hivi Magufuli akiwaambia wafute posho na wao wataacha kuchangia.
 
kasema usipochangia au ukisusia mkuu mbona mtoa mada huelwek
 
Kulala, kupiga vigeregere na ndiyooooooooo.
 
Kama wanasusa basi wasuse na posho ,wasiishie kususa mijadala tu,hatukuwachagua kwenda kufuata matakwa binfsi ya Mbowe na timu yake,wakumbuke hawakuchaguliwa na Mbowe huko majimboni
Wewe umemchagua nani mnafiki mkubwa wewe!?
 
Mleta mada acha kupotosha Nimemsikiliza vizuri Bashe hayo uliyoyaleta hapa ni uongo dhahiri na sijui malengo yako ni yapi....dhambi ya uongo ni mbaya sana
Tupe ukweli uliousikia mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…