BASATA yaonya wanaotumia vibaya mitandao

BASATA yaonya wanaotumia vibaya mitandao

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
26,681
Reaction score
59,181
BASATA wametoa siku saba kwa wamiliki wa wavuti, na wale wenye akaunti kwenye mitandao ya kijamii Kuondoa nyimbo zenye kusambaza chuki,matusi, kashfa, kejeli na udhalilishaji wa watu wa kada mbalimbali wakiwemo wanasiasa.


Katibu Mtendaji wa BASATA Godfrey Mngereza, amevitaka pia vyombo vya habari ikiwamo redio, luninga, kuondoa na kuacha mara moja kucheza au kurusha nyimbo zote zenye maudhui hayo.

============================

Update kwenye Magazeti;

Dar es Salaam. Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limetoa siku saba kwa wasanii, wamiliki wa wavuti, na wale wenye akaunti kwenye mitandao ya kijamii kuondoa nyimbo zote au maudhui yenye mwelekeo unaoenda kinyuma na maadili, matusi, kashfa, kejeli na udhalilishaji wa watu wa kada mbalimbali wakiwemo viongozi wa kisiasa na kitaifa.


Taarifa ya Basata iliyotiwa saini na Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, Godfrey Mngereza umevitaka pia vyombo vya habari ikiwamo redio, luninga, kuondoa na kuacha mara moja kucheza au kurusha nyimbo zote zenye maudhui hayo.


Mngereza alisema kuwa maudhui ya kashfa, matusi, kejeli, udhalilishaji zinatishia kuigawa jamii ya Watanzania katika kipindi hiki ambacho taifa linaendelea na kampeni za kisiasa na kujiandaa na uchaguzi mkuu.


Alivitaja kifungu namba 118 (a-d) cha Sheria ya Bunge namba 9 ya Mawasiliano ya Mtandao ya mwaka 2010 vinaeleza kuwa ni marufuku kwa njia yoyote kwa mtu au chombo chochote kutengeneza, kuzalisha, kusambaza au kutangaza ujumbe ambao una mlengo wa matusi, dharau, uzushi au jinai kwa lengo la kutukana, kutisha, kusumbua au kushusha hadhi ya mtu mwingine.


Alisema Sheria ya Bunge namba 4 ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 kifungu cha 45 (1) (a-c) kinatoa mamlaka kwa taasisi au mtu yeyote anayebaini uvunjifu wa sheria katika mitandao kutoa notisi kwa yeyote yule anayesambaza au kutangaza ujumbe au maudhui yanayovunja sheria za nchi kuacha mara moja au vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote anayekaidi.


“Kwa msingi huu, Basata linawaagiza wasanii wote nchini kuacha mara moja kubuni na kutengeneza kazi za sanaa zenye kuashiria kuigawa jamii katika misingi yoyote ya kibaguzi na zaidi kutumia sanaa kubomoa jamii badala ya kuijenga, ”alisema Mngereza.


Aitumia taarifa hiyo pia kuwasisitiza wamiliki wa vyombo vya habari wakiwamo wa radio na luninga na watangazaji kuhakikisha hawawi chanzo cha kusambaza maudhui yoyote ya sanaa yenye mlengo wa kuibua chuki, matusi, kashfa na mgawanyiko wa taifa.

Chanzo: Mwananchi
 
Waanze na TWAWEZA Kwani Wamehutumia Vibaya Mtandao..

Kutumia Vibaya Mtandao eti Ni Kusema Ukweli juu ya CCM.
 
Hebu weka walau hata picha basi mkuu...!
 
Ni mangapi tunashuhudia mchana kweupe kwenye vyombo ya habari vya serikali?

Tatizo lenu huwa mnahisi Tz haina sheria na pale zinapowekwa wazi mnahisi mnaonewa ..sasa kama ulisubiri kuambiwa kwamba matusi na kashfa si sehemu ya maadiri, basi mtafundishwa hilo na sheria husika.
 
Tatizo lenu huwa mnahisi Tz haina sheria na pale zinapowekwa wazi mnahisi mnaonewa ..sasa kama ulisubiri kuambiwa kwamba matusi na kashfa si sehemu ya maadiri, basi mtafundishwa hilo na sheria husika.

Nchi sio shule ambako sheria fulani ikivunjwa mkuu wa shule anatoa onyo kuwa atakayerudia ataadhibiwa. Nchi sheria ikishawekwa ni kutekeleza, ukivunja hatua stahiki zichukuliwe. Sikutegemea BASATA waje na onyo bali wachukue hatua kwa waliovunja. Waanze na Shilole waliyempiga ban ya mwaka na ameibukia kwenye matamasha ya mgombea wa CCM.

MY TAKE: Kama mgombea wa CCM anajua kuwa Shilole amesimamishwa na kwa makusudi anaendelea kumtumia basi mgombea huyu anaonyesha jinsi ambavyo atakuwa haheshimu maamuzi ya vyombo vingine vya serikali - sababu nyingine ya kutompa kura yangu.
 
Tatizo lenu huwa mnahisi Tz haina sheria na pale zinapowekwa wazi mnahisi mnaonewa ..sasa kama ulisubiri kuambiwa kwamba matusi na kashfa si sehemu ya maadiri, basi mtafundishwa hilo na sheria husika.

Hunijui,sikujui na sihitaji kukujua either, nafikiri umeongeza post kwa kuni quote ila sina hakika kama ulinielewa!
 


Baraza la Basata wameufungia wimbo wa msanii Roma Mkatoliki uitwao 'Viva Roma Viva ' na nyinginezo zenye ujumbe kama ule. Basata imesema sababu kubwa ya kuufungia wimbo huo wa Roma ni kwamba hakuna ushahidi wa vitu vilivyoimbwa katika wimbo huo.
SWALI NI JE?
KILA KINACHOIMBWA KWENYE NYIMBO KINAUSHAHIDI?
 
Tatizo lenu huwa mnahisi Tz haina sheria na pale zinapowekwa wazi mnahisi mnaonewa ..sasa kama ulisubiri kuambiwa kwamba matusi na kashfa si sehemu ya maadiri, basi mtafundishwa hilo na sheria husika.

Tatizo la basata wamegeuza ukweli kuwa uadui.NATOKA TANZANIA BY NIKKI MBISHI(nchi ambayo raisi ni mzito kwenye maamuzi/anafungia macho vigogo na walanguzi/vya msingi nyuma vya mbele ni vya kipuuzi/na juzi alikuwa kwenye msiba wa bongo movie)Umeelewa?
 
Nijuavyo mimi ni kuwa jambo lolote linalofanania na ukweli likisemwa basi ni utani tuu ...........na kama ni kweli basi utauma tu
 
Bob Marley - One Drop

Feel it in the one drop; And we'll still find time to rap...... VIVA ROMA VIVA.



Oo-oo-ooh, yea-ah. Wo-yoy! Wo-yoy! Wo-yoy! Wo-yoy-yoy-yoy!
Feel it in the one drop; And we'll still find time to rap;
We're makin' the one stop, The generation gap;
Now feel this drumbeat. As it beats within,
Playin' a riddim, Resisting against the system, ooh-wee!

I know Jah's never let us down; Pull your rights from wrong

(I know Jah would never let us down)
Oh, no! Oh, no! Oh, no!
They made their world so hard (so hard): Every day we got to keep on fighting (fighting);
They made their world so hard (so hard): Every day the people are dyin' (dying), yeah!
(It dread, dread) For hunger (dread, dread) and starvation
(dread, dread, dread, dread), Lamentation (dread dread),

But read it in Revelation (dread, dread, dread, dread): You'll find your redemption
And then you give us the teachings of His Majesty, For we no want no devil philosophy;
A you fe give us the teachings of His Majesty, A we no want no devil philosophy:

Feel it in the one drop;And we still find time to rap;
We're making the one stop, And we filling the gap:
So feel this drumbeat. As it beats within
Playing a riddim, uh! Fighting against ism and skism,

Singing: I know Jah's never let us down;
Pull your rights from wrong:
I know Jah's never let us down.
Oh, no! Oh, no! Oh, no!
They made their world so hard Every day (we got to keep on fighting), every day;
They made their world so hard........




 
Last edited by a moderator:
Nasikia na ile nyimbo maarufu ya Kuku kapanda Baiskeli iliyouimbwa na Mr. Nice imefungiwa maana hakuana ushahidi wa Kuku kupanda baikeli.
Kaazi kweli. Siasa zitatuuwa.
 
Baraza la Basata wameufungia rasmi wimbo wamsanii Roma Mkatoliki uitwao 'Viva Roma Viva ' na nyinginezo zenye ujumbe kama ule.

Basata imesema sababu kubwa ya kuufungia wimbo huo wa Roma ni kwamba hakuna ushahidi wa vitu vilivyoimbwa katika wimbo huo.


Nini maoni yako?


Chanzo : EATV
 
Back
Top Bottom