Baraza la mtihani(NECTA) hii imekaaje?Bring back our scores

Baraza la mtihani(NECTA) hii imekaaje?Bring back our scores

MR.NOMA

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
339
Reaction score
512
Wadau naandika huku nikiwa na machungu moyoni.Wakati nimeamaliza Kidato cha 4 Kwiro sekondari Morogoro mwaka 2002 nilipata Division 2 ya pointi 18,lakini nikaandikiwa nimepata div 3 eti kwasababu tu nilipata F ya hesabu,eti nikapigwa penalty.Sasa nimeona matokeo ya mwaka 2015 wanafunzi walipata div 1 & 2 wakaandikiwa kama matokeo yao yalivyo, huku wamefeli hesabu.Hii imekaaje jamani,hasa katika wakati huu wa uhakiki wa vyeti na wasomi;je sina haki ya kudai Division 2 yangu irudishwe kama ilivyo ili cheti changu kipendeze nisionekane kilaza,nimepata div 3 wakati ukweli nina div 2.hayo hapo chini ni baadhi ya matokeo ya mwaka 2015 ya kidato cha 4 nimeyanakili kama yalivyo toka tovuti ya NECTA.

S0234/0051-F -21 II CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' B/KNOWL - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'C' BIO - 'C' B/MATH - 'F'

S0234/0052-F- 21 II CIV - 'C' HIST - 'C' GEO - 'C' B/KNOWL - 'C' KISW - 'C' ENGL - 'C' CHEM - 'D' BIO - 'C' B/MATH - 'F'

Bring back our Scores
 
Ungetaka kipendeze ungejiitahidi usipate FA ya hesabu haiwezekan masomo mengine umetia juhudi ume pass alfu math ulifanyie uzembe
 
Hata kama ungepigwa penalty ingekuwa ni three ya 18. sio three ya 23
 
Hata kama ungepigwa penalty ingekuwa ni three ya 18. sio three ya 23
kinachonishangaza ni kuwa mbona nimeona matokeo ya mwaka 2015 watu wamefeli hesabu ila hawana penalty,sera gani imetumika hapo
 
Kumbuka sera ya elimu haiko specific kesho utakuta mambo ni tofauti na leo
 
Kwa kweli roho yangu huumia sana,kila nikitazama cheti changu cha form 4,
Pole sana. Pamoja ya mimi kuwa gwiji wa Hesabu lakini nadhani hii sera wangeiondoa. Inawezekana iliwekwa kuencourage watu wafaulu Hesabu ( nahisi inaply kwa Basic Subjects japo huonekana zaidi kwenye Maths) sidhani kama imesaidia. Hivyo Masomo yangekuwa yanakuwa graded equally! Na km ingekuwa nia watu wakazane wangeambiwa basi tangu mwanzoni all in all nadhani masomo yawe-graded equally.
 
Hicho Cheti chako kwa bashite ni almasi

he he he bashite cheti inachosemekana amekinunua kina div 3 ya 25 pts.. yaani div 3 ya mwisho..

mtu ambaye div 3 ya 25 ameiona almasi atashindwaje kuiona ni mgodi mzima cheti cha pts 18...

unapata f hadi kiswahili... hii ni zaid ya ukilaza
 
Ubaya au uzuri wa cheti unao taka ww hauwezi badilisha maisha yko kuyatoa hapo ulipo kwenda hatua ya mafanikio zaid, ushauri wangu mshirikishe Mungu ktk mambo yko, amua vzr na panga vzr tktk mikakati yko, jitume zaid utafanikiwa kuzid hata hao waliopata 1.7
 
Kwnz nkupongeze kw kusoma shule pendw sn kwiro boys nkukmbsh kdg baadh y maeneo utu vigoi nawenge mawasiliano apo vp
 
Kufaulu darasani si kufaulu maisha, Mshukuru Mungu ulifaulu na una CHETI halali, wengine wanatani wangekuwa na cheti chenye jina lake halisi, piga kazi mkuu maana hamna namna.
 
mkuu usilalamike na sisi ambao tupo chuo tukitaka na nyie vyeti vyenu vitolewe second class muweke pass kama sisi itakuwaje lakini
 
Back
Top Bottom