Field Mashal
Member
- Jan 16, 2013
- 36
- 13
Kuvunjwa kwa baraza hilo la madiwani kumependekezwa na wananchi wa manispaa kupitia vi-redio vya Bukoba, baada ya kuona kila kitu kinaenda mchafu koge, na kupelekea ongezeko ugumu wa maisha kutokana na wawakilishi wa wananchi kwenye kata kutozungumzia yanayowagusa kwenye halmashauri hiyo.
Leo Baraza limefunguliwa na Meya Aman, lakini wakabadili kanuni makusudi ili waandishi waondolewe kwenye kikao na kumpa Meya nafasi ya kujitanua na kupokea taarifa za utekelezaji wa kila kata ambapo saizi kinachoendelea ni agenda ya Mugambo wanaotumika kunyanyasa wananchi kwa kuvunja nyumba zao eti ni chafu, kupiga watu eti hawajalipa faini baada ya kukutwa hawana shimo la taka, pamoja na kubeba watoto na kuzunguka nao wanaokutwa kwenye nyumba ambayo mzazi pengine ameenda kazini badala ya kuchukua jina la mhusika ili kama nifaini akalipe kwa mujibu wa sheria.
Jambo hilo limekwishafikishwa kwa mkurugezi na waandishi wa habari lakini anashindwa kutoa majibu kwa kisingizio cha kusubiri Meya alizungumzie, kwasababu yeye ndiyo aliyeweka wanamgambo, ambapo kinachofanyika ni kusakama kata ambazo madiwani wake hawamuungi Meya mkono.
Sazi baraza linaendelea lakini waalikwa, na wanahabari wametolewa nje, je kunani zaidi ambacho hawataki wananchi wakijue?
Leo Baraza limefunguliwa na Meya Aman, lakini wakabadili kanuni makusudi ili waandishi waondolewe kwenye kikao na kumpa Meya nafasi ya kujitanua na kupokea taarifa za utekelezaji wa kila kata ambapo saizi kinachoendelea ni agenda ya Mugambo wanaotumika kunyanyasa wananchi kwa kuvunja nyumba zao eti ni chafu, kupiga watu eti hawajalipa faini baada ya kukutwa hawana shimo la taka, pamoja na kubeba watoto na kuzunguka nao wanaokutwa kwenye nyumba ambayo mzazi pengine ameenda kazini badala ya kuchukua jina la mhusika ili kama nifaini akalipe kwa mujibu wa sheria.
Jambo hilo limekwishafikishwa kwa mkurugezi na waandishi wa habari lakini anashindwa kutoa majibu kwa kisingizio cha kusubiri Meya alizungumzie, kwasababu yeye ndiyo aliyeweka wanamgambo, ambapo kinachofanyika ni kusakama kata ambazo madiwani wake hawamuungi Meya mkono.
Sazi baraza linaendelea lakini waalikwa, na wanahabari wametolewa nje, je kunani zaidi ambacho hawataki wananchi wakijue?