Barabara za Juu kwa Juu kweli ni kwa ajili ya kupunguza msongamano?

njia mojawapo ya kupunguza foleni badala ya kutengeneza mabarabara ya juu kwa juu ni kujenga outer drives...
Duh umekuwa mhandisi sasa! I don't understand what you want! no consistence in what you're saying. One minute you want feeder roads the next you want outer roads

For your information traffic jam occurs at the traffic lights. Having flyovers is a good start followed by introducing specific speeds to specific roads
 

Zipo flyover hizo za kujaza udongo na zipo za kujenga maguzo ya concrete. Nyumba zingine inabidi ziondoke. Gharama za kutokuwa na maendeleo ya barabara za uhakika ni kubwa kuliko majumba yanayobomolewa.
 

zomba, lugha mtihani...inanipiga chenga.
 
Hili suala linaitaji taaluma sio siasa...kila mwanasiasa akija na mawazo yake hakuna kitakachofanyika..

I agree with you Ritz...halafu lini tutaanza kuboresha miundo mbinu kama hatuna moyo wa uthubutu na nia ya kurekebisha makosa yaliyokwisha fanywa kabla. Miji yetu mingi haikupangiliwa na ndio chanzo cha matatizo leo tunapoanza kuona ongezo la watu na vitendea kazi mbali mbali. Kama bado tunaendesha fikra kisiasa tutaendelea kukwama maana siasa inataka kuenzi fikra za chama kwanza.
Naunga mkono hii step ya kuamua kujaribu kufanya kitu tofauti
 
zomba, lugha mtihani...inanipiga chenga.

Siku hizi watu hawana "excuse" hiyo. Unabandua kipande usichokijuwa unakibandika "google translate" mambo swaafi kabisa. Mie hata Wachina wakiniandikia Kichina nawajibu Kiswahili tunaelewana na kila mtu happy 快乐.

Chukuwa hilo neno la kichina libandike hapa uone mwenyewe kwa raha zako: Google Translate
 

teh teh teh...ndio maana nauheshimu sana mtandao huu. Kila siku najifunza kitu kipya. Naamini hata hii migongano ya mawazo ni kwania njema tu, ili tuweze kusonga mbele kama watu wamoja na Taifa moja. Ngoja niingie huko kwa google translate nipate mambo
 
Barabara za juu kwa juu zina umuhimu wake LAKINI si katika level hii ya maendeleo ya Jiji la Dar Es Salaam! Maji taka ya chini kwa chini yatushinde leo hii barabara za juu kwa juu tutaziweza? It's all about "na sisi tunazo" at least for now!
 
Kupanga ni kuchagua!
Ukitaka kila gari linalotoka jijini kuelekea Morogoro lipite UBUNGO, basi unahitaji barabara za juu kwa juu pale makutano ya UBUNGO. Lakini ukiwa na ubunifu kwamba si kila aendaye Moro ni lazima apite UBUNGO, basi utaanza na kile kilicho katika uwezo wako - tengeneza barabara mbadala kutoka maeneo mbalimbali kuelekea Kimara, Mbezi, bagamoyo, Kibaha, nk.

ndiyo 'na sisi tumo'
 
Mzee mwenzangu wacha wazijenge ziishie kuwa balaa la kitaifa. Kwa wanavyohongana unadhani zitakuwa salama? Tatizo si msongomano wa magari bali msongamano wa ujinga na mipango mibovu. Upo hapo mzee mwenzangu?
 
Mie CCM damu ila siko sana kisiasa kwenye masuala ya kitaalamu! Magufuli, some points to chew bro!

Maoni yako mazuri. Pamoja na u CCM damu wako ukweli ni kwamba utawala wa CCM hawamu zote baada ya Mwalimu umechukua mtindo wa "zima moto" kwa kila tatizo la nchi hii. Ninamtoa Mwalimu kwa sababu angaa alibuni kitu ambacho hadi leo hii kimeendelea kujadiliwa duniani kote - ujamaa. Kwa mtazamo wa mwalimu kuhusu ujamaa mkazo ulikwekwa kuboresha maisha ya vijijini ambako hadi leo hii asilimia zaidi ya 80 ya watanzania inaishi - hawa hawana habari na misongamano ya UBUNGo na TAZARA!! Hili lilikuwa na bado ni suala la kifalsafa. Ndio maana alitaka kuamishia makao makuu DODOMA!!
Turejee kwa post-mwalimu administrations: hawa waliamua kurejesha mkazo kuboresha maisha ya mijini (hususan Dar) lakini hawana dira bali kila kukicha 'zima moto' (iwe umeme, iwe maji, iwe afya, iwe usafiri, iwe misongamano ya magari). Hayo unayoyasema ni mawazo mazuri sana ambayo yalipaswa kuzingatiwa na hao damu damu muda mrefu kwa vile falsafa yao ya maendeleo ni urbanization au niseme darbanization - ndio maana walisitisha mpango wa kuhamishia makao makuu ya utawala DODOMA.
Siku moja ningeshukuru kama ungetueleza ni kitu gani kinakufanya uwe CCM damudamu!!!
 
Zipo flyover hizo za kujaza udongo na zipo za kujenga maguzo ya concrete. Nyumba zingine inabidi ziondoke. Gharama za kutokuwa na maendeleo ya barabara za uhakika ni kubwa kuliko majumba yanayobomolewa.

Tatizo letu hapo kwenye kubomoa nyumba kwani majengo mengi ya serikali yakiwa kwenye hifadhi tu ya barabara mara nyingi hayabomolewi lakini kiukweli kuna mitaa mingine Dar nyumba mtaa mzima zinatakiwa zibomolewe warekebishe miundo mbinu lakini kwa kuwa nchi inaongozwa na wanasiasa wasiojiamini utasikia hawa ni wapiga kura wangu inabidi serikali iangalie namna ya kuwasaidia matokeo yake hazibomolewi. Hii nchi wanasiasa wakikubali kuitwa wanoko kisa wanasimamia sheria na maamuzi nadhani mabadiliko yanawezekana maana fly over inahitaji space na si lazima katikati ya jiji tu hata nje ya jiji mambo yanawezekana pia
 
MPIGA ZEZE nakupa tano kwa analysis, unajua mtu yoyote anaejaribu kutetea falsafa yoyote kwa vitendo hata kama atashindwa mie namwona ni shujaa, wengi wanamlau mwalimu lakini at least alijaribu kuweka nadharia za ujamaa kwa vitendo japokuwa ili ujamaa uweze kufanikiwa lazima nchi iwe imejitosheleza kiuchumi kuweza kutoa huduma za jamii kwa usawa. Mie hawa nawaita wazee wa Trial and error mfano angalia barabara zetu nyingi kuu hata miaka 10 hazijaisha zinarudiwa coat nyembamba wakati kama zingetunzwa vizuri maana yake badala ya kurudishia lami zile ela zingejenga barabara zingine. Badala viongozi kupigania reli kwa kusafirisha mizigo mizito ili kulinda barabara zetu wao wanakomaa na kufanya ukarabati mkubwa kila baada ya miaka mitano.
 
Last edited by a moderator:

Mabadiliko ya miundombinu yameanza kwa kasi kipindi cha Kikwete kuliko wakati wowote ule na tunayaona.
 

Labda wana mitazamo ya kizamani ambayo WANAAMINI LAZIMA GARI ZIPITE UBUNGO KUDHIBITI WAHARIFU SI UNAJUA VICHWA VYETU VINAFIKIRI SIJUI NISEMEJE yaani kama zamani nilipokuwa primary school tulikuwa tunaambiwa Range Rover hakuna kupaki karibu na bank walikuwa wanaogopa fedha zikiibiwa hakuna wa kuweza kuikimbia maana miaka 80s ndo gari iliyokuwa inaaminika inakimbia (sijui kama kuna ukweli au zilikuwa story za kwenye kahawa).
 

Mkuu mimi nimefanya kazi na wajapan na miradi yao ya JICA. kuna siku moja bosi wangu aliniambia kuwa JICA huwa wanakaa na wakandarasi wao na kudesign miradi kwenye nchi masikini na kuishauri serikali yao ili hela itoke na waom wapate fungu hapo. Its purely business.

Hebu tuwe wakweli, pale TAZARA ukiweka hizo flyovers. zitaenda mpaka wapi? pale KAMATA kwenda kariakoo ni foleni tu, kwenda city centre ni barabara zile zile
Hata pale Ubungo mataa, ukifika jangwani utaenda wapi au ukifika pale Bahama mama unapita wapi mpaka ufike mbezi na kiluvya?

Suluhishmla kwanza ilitakiwa serikali ihakikishe magari ya umma (dala dala) ziwe na hadhi y mtu kupanda amevaa suti bila bugudha. we jaribu kupanda gari ya mbagala pale posta mpya au kivukoni jioni uone balaa lake.
Then city centre ilitakiwa magari yaingie kwa vibali maalum. sasa hata boda boda utaziona zinapita pale nje ya ikulu. sasa hapo foleni zitaishia wapi wakati city centre haina utaratibu wa kuingia?

Kama public transport ingekuwa reliable naamini wengi tungeacha magari yetu home.
Kwani wakienda huko nje hawaoni wenzao wanavyofanya?

Tatizo serikali etu uwezo wake wa kufikiria unaishia kwenye kiwango cha familia za watendaji wakuu wa serikali
 
Mabadiliko ya miundombinu yameanza kwa kasi kipindi cha Kikwete kuliko wakati wowote ule na tunayaona.

Miundo mbinu gani hiyo mbona naona mingi haijakamilika na miaka inazidi kuisha, Lakini hata Chinga boy alijitutumua maana kubomoa nyumba morogoro road kuanzia magomeni mpaka kimara kupisha ujenzi si mchezo
 

Salute kwenu Ritz na Ndahani maana sheria zinatungwa na wabunge na linapokuja suala la kutekeleza sheria ambazo kwa namna ama nyingine zinawaumiza wananchi wabunge hao hao wanarudi na kusema hawa ni wapiga kura wangu
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…