Mwakiluma
Senior Member
- Jan 23, 2012
- 120
- 47
Katika analysis yangu katika jimbo la kyela wananchi wanasema huenda ukawadia mwisho wa ccm katika jimbo la kyela mara itapofika mwaka 2015 huku barabara ya kyela-ipinda-matema haitakuwa imejengwa kwa kiwango cha lami...tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi na uchaguzi wa kwanza mwaka 95 wabunge wa CCM wamekuwa wakiahidi kuijenga barabara hiyo lakini hakuna kilichofanyika.
Mbunge wa kwanza alikuwa Kasyupa, akaja akaja mwakipesile na sasa Mwakyembe wote wametoa ahadi hizohizo...
Katika kampeni zake Mwakyembe aliwaambia wananchi wa kyela kuwa wampigie kura Kikwete kwa sababu amemwahidi kuijenga barabara hiyo.
Katika maelezo yake bungeni Mwakyembe alisema hawezi kudai ujenzi wa barabara ya wilaya wakati barabara za mikoa katika mikoa mingine bado hazijajengwa kauli ambayo ilileta minong'ono mingi miongoni mwa wananchi wa kyela...
Katika kata za Talatala, Ipinda, Lusungo, Makwale na Matema wamesema watalazimika kufanya mabadiliko iwapo barabara hiyo haitajengwa.
Hata baada ya kupewa unaibu waziri wa ujenzi wananchi wengi wa kyela wamekuwa wakiweka matumaini mengi kwa Mwakyembe lakini hadi hivi sasa ikiwa imebakia takribani miaka mitatu ya ubunge wake hakuna kilichofanyika.
CCM haina ushawishi wa kichama katika jimbo lolote lile bali kimebaki na ushawashi wa mtu binafsi tu,hivyo iwapo wananchi wa kyela wataamua kuachana na mwakyembe jimbo hilo litakwenda kwa upinzani maramoja...mathalani katika kata ya ipinda tayari chadema kilishapata diwani katika uchaguzi wa 2010 na katika kata nyingi kama ile ya makwale ccm ilipata upinzani mkubwa...vijiji vingi vya talatala, tenende, ipinda, kafundo, ikulu, bwato, lupaso, lukama, mpanda lusungo, kisale, mpunguti, makwale na matema vinapata usumbufu mkubwa wa usafiri ikiwemo gharama kubwa za usafiri kutokana na ubovu wa barabara....Mwakyembe itambidi afanye jithada kubwa kuweza kujenga barabara ile ili kuongeza ushawishi..HAKUNA MAENDELEO KATIKA JIMBO LA KYELA NA MWAKYEMBE AMEKUWA MTU WA KYENYE MAGAZETI TU NA SIO MAENDELEO YA JIMBO LA KYELA...HAELEWANI NA WATENDAJI WENGI WA JIMBO HILO.
Mbunge wa kwanza alikuwa Kasyupa, akaja akaja mwakipesile na sasa Mwakyembe wote wametoa ahadi hizohizo...
Katika kampeni zake Mwakyembe aliwaambia wananchi wa kyela kuwa wampigie kura Kikwete kwa sababu amemwahidi kuijenga barabara hiyo.
Katika maelezo yake bungeni Mwakyembe alisema hawezi kudai ujenzi wa barabara ya wilaya wakati barabara za mikoa katika mikoa mingine bado hazijajengwa kauli ambayo ilileta minong'ono mingi miongoni mwa wananchi wa kyela...
Katika kata za Talatala, Ipinda, Lusungo, Makwale na Matema wamesema watalazimika kufanya mabadiliko iwapo barabara hiyo haitajengwa.
Hata baada ya kupewa unaibu waziri wa ujenzi wananchi wengi wa kyela wamekuwa wakiweka matumaini mengi kwa Mwakyembe lakini hadi hivi sasa ikiwa imebakia takribani miaka mitatu ya ubunge wake hakuna kilichofanyika.
CCM haina ushawishi wa kichama katika jimbo lolote lile bali kimebaki na ushawashi wa mtu binafsi tu,hivyo iwapo wananchi wa kyela wataamua kuachana na mwakyembe jimbo hilo litakwenda kwa upinzani maramoja...mathalani katika kata ya ipinda tayari chadema kilishapata diwani katika uchaguzi wa 2010 na katika kata nyingi kama ile ya makwale ccm ilipata upinzani mkubwa...vijiji vingi vya talatala, tenende, ipinda, kafundo, ikulu, bwato, lupaso, lukama, mpanda lusungo, kisale, mpunguti, makwale na matema vinapata usumbufu mkubwa wa usafiri ikiwemo gharama kubwa za usafiri kutokana na ubovu wa barabara....Mwakyembe itambidi afanye jithada kubwa kuweza kujenga barabara ile ili kuongeza ushawishi..HAKUNA MAENDELEO KATIKA JIMBO LA KYELA NA MWAKYEMBE AMEKUWA MTU WA KYENYE MAGAZETI TU NA SIO MAENDELEO YA JIMBO LA KYELA...HAELEWANI NA WATENDAJI WENGI WA JIMBO HILO.