Barabara ya Magole-Kitunda yapata mfadhiri ndotoni

Barabara ya Magole-Kitunda yapata mfadhiri ndotoni

Charles Mkubya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2009
Posts
206
Reaction score
161
Jana nilipokea simu toka kwa Milard Ayo wa Clouds Media akinitaarifu nimekua mshindi katika moja ya michezo ya kubahatisha....TZS bilioni 1.
Akaniuliza swali moja “utaifanyia nini hii pesa??” Nikamwambia kwa adha ya barabara ninayopata, najitolea pesa yote hii itumike kwa ujenzi wa barabara ya Kitunda mpaka Magole mwisho. Kwa kuwa nilikua live clouds fm, zikapigwa simu nyingi kudhibitisha adha ya wakazi wa Magole na Bonge wa kipindi cha PB nae akadhibitisha hili..
Ukazuka mjadala mrefu na kizuri zaidi simu zikandelea kupigwa na katika watu wachache naokumbuka walipiga simu alikua mkuu wa Toyota Tanzania akisema nimetumia pesa nyingi kununua vipuli vya gari yangu (spare) sababu ya ubovu wa barabara hivyo anachangia kiasi cha pesa...., Mh mkuu wa mkoa, kaka yangu Makonda akachangia sehemu ya fedha huku akitoa maelekezo kwa wizara husika....Mh Lukuvi akajitolea kuchangia akisema itasaidia kuboresha makazi ya watu wa Magole, tukapata baadhi ya wakandarasi waliojitolea vifusi na kokoto na ndani ya dakika 30 tukawa na kiasi cha Bilioni 5.
Dakika za mwisho mkuu mwenyewe akapiga simu kushukuru kuona wananchi wanajitolea kusaidia serikali katika utatuzi wa kero zinazowazunguka na akauliza kama nina ombi lingine zaidi. Nikamwambia, “Mheshimiwa kwa sasa natamani hii barabara tu ikamilike na kama itakupendeza, hii kazi na pesa zote zilizopatikana apewe Kamanda Charles Mbuge, Brig Generali yule mahiri wa kusimamia ujenzi aisimamie...” wakati nasubiri mkuu atajibu nini, nikihisi labda nimekosea protocal........alarm ya simu ikaniamsha....kumbe nilikua naota tu usingizini🤦🏽‍♂️🤦🏽‍♂️🤦🏽‍♂️.

Natamani ndoto hii iwe kweli siku moja. Mungu ibariki Tanzania.
 
Huko mmeshasahaulika tu hamna namna, hiyo barabara imeanza kuzungumziwa siku nyingi sana wanajenga za kuonekana zaidi na sio za kujificha.
 
Huko mmeshasahaulika tu hamna namna, hiyo barabara imeanza kuzungumziwa siku nyingi sana wanajenga za kuonekana zaidi na sio za kujificha.

Labda kuna siku Mh Waitara atatukumbuka, ngoja tuvute subira kidogo lakini hali ya barabara ni mbaya
 
na kweli hii barabara ni mbovu hatari, kila ikifika weekend kwenda kumcheki bi mkubwa nawaza mara 2, 2
 
Pole sana. Wacha wamalizie kwanza hii ya kitunda - Msongola... Ikiwekwa lami ikawa fresh na matuta yakawa machache, jiji litakuwa limefungukaa...
 
Labda kuna siku Mh Waitara atatukumbuka, ngoja tuvute subira kidogo lakini hali ya barabara ni mbaya
Jinga hilo lipigaji kwanza nakuhakikishia hiyo barabara itaendelea kupigwa magreda ya kuiweka sawa hadi huyo mkurya atakapotoka Walai tata
 
Ujenzi wa barbara hiyo (japo ndotoni) uanzie Banana na sio Kitunda. Kile kipande kilichowekwa lami kutoka Banana hadi Kitunda kimechakaa hadi ni kero kuu.
 
Ujenzi wa barbara hiyo (japo ndotoni) uanzie Banana na sio Kitunda. Kile kipande kilichowekwa lami kutoka Banana hadi Kitunda kimechakaa hadi ni kero kuu.

Ni kweli mkuu, asante sana kwa wazo/ushauri wako. Wahusika nadhani watachukua
 
Back
Top Bottom