Bandari yawafuata wafanyabiashara 100

Hii ni habari katika gazeti la Mwananchi la siku ya leo tarehe 10/09/2016.

Chanzo:Star tv magazeti
Sasa Mkulu si alijifanya masikini jeuri kwa kutamba kuwa waliokimbia kutumia bandari ya Dar ni wale wafanyabiashara wakwepa kodi na akawaambia kuwa waende kwenye hizo bandari za nchi nyingine zinazoruhusu mizigo kupita bila kulipiwa kodi?

Sasa baada ya kuona bandari imekauka kabisa ndiyo anakuwa 'mpole' na kutaka kwenda kuwapigia magoti?

Hii nchi haitakiwi kuendeshwa kwa ubabe na matamko ya majukwaani, badala yake inatakiwa kuendeshwa kwa kufuata sheria za nchi na kusikiliza maoni ya wadau mbalimbali namna bora ya kuiendeleza nchi yetu.

Mkulu akiendeleza kuendesha nchi yetu kwa staili yake ya ONE MAN SHOW, hakika nchi yetu itakuwa inaelekea kuwa another Zimbabwe...............
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…