Kisoda2
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 2,475
- 745
Maringira ya yanayoizunguka shule hii yanahatarisha afya kwa wanafunzi na makazi ya watu wanaoizunguka shule hii iliyopo maeneo ya Mbeni.
Tatizo kuu ni ukosefu wa mifumo ya maji taka hasa mfumo mzima wa vyoo kwani maji taka hayo yamekuwa yakimwagika ovyo na kusambaa katika mifereji iliyopo kando ya barabara na kuwa kero kwa wananchi wakaazi wa eneo hilo.
Tatizo hili lilifika katika kamati ya ulinzi na mazingira eneo hilo na wakatumwa wawakilishi ili kwenda kuongea na uongozi wa shule lakini hawakuweza kuongea nao baada ya kujibiwa kuwa wao si wakaguzi ila wapo wanaoweza kujakuikagua shule,hivyo kiongozi mkuu huyo aliwataka waondoke eneo la shule.
Taarifa hizo alipewa DIWANI wa Mbweni Mh.Hashim Mbonde na kuahidi kutoa namba za wahusika wa jiji, kwa kamati ya mazingira.
Hadi sasa mazingira yako vile vile.Na hivi juzi tu,imeripotiwa kuwa El-nino Kuipiga Tanzania.
Je,kwa mazingira haya usalama upo kweli?
Je,hawa wanaokwenda kumkagua huyu kiongozi wa shule wana kagua nini ,na ni wa kutoka wapi?
Hali ndo kama inavyojionyesha katika picha hizi.
Naomba wadau mtusaidie tuwanusuru watoto wetu na maradhi ya mlipuko.
Tatizo kuu ni ukosefu wa mifumo ya maji taka hasa mfumo mzima wa vyoo kwani maji taka hayo yamekuwa yakimwagika ovyo na kusambaa katika mifereji iliyopo kando ya barabara na kuwa kero kwa wananchi wakaazi wa eneo hilo.
Tatizo hili lilifika katika kamati ya ulinzi na mazingira eneo hilo na wakatumwa wawakilishi ili kwenda kuongea na uongozi wa shule lakini hawakuweza kuongea nao baada ya kujibiwa kuwa wao si wakaguzi ila wapo wanaoweza kujakuikagua shule,hivyo kiongozi mkuu huyo aliwataka waondoke eneo la shule.
Taarifa hizo alipewa DIWANI wa Mbweni Mh.Hashim Mbonde na kuahidi kutoa namba za wahusika wa jiji, kwa kamati ya mazingira.
Hadi sasa mazingira yako vile vile.Na hivi juzi tu,imeripotiwa kuwa El-nino Kuipiga Tanzania.
Je,kwa mazingira haya usalama upo kweli?
Je,hawa wanaokwenda kumkagua huyu kiongozi wa shule wana kagua nini ,na ni wa kutoka wapi?
Hali ndo kama inavyojionyesha katika picha hizi.
Naomba wadau mtusaidie tuwanusuru watoto wetu na maradhi ya mlipuko.