Natumia neno zuri "ujinga" sio upumbavu. Jana mkubwa wa polisi Mbeya aliitisha mkutano na waendesha bajaji wote.
Iliamriwa kwamba waendeshaji wote wasiendelee kusafirisha abiria wakati wote wa kikao na RPC huyo.
Inaelezwa kwamba kikao hicho hakikuwa na lolote jipya zaidi ya blabla na kupotezeana muda. Sikuona sababu ya kusimamisha usafiri huo kwa kutwa nzima wakati mmiliki au mwakilishi mwingine angeweza kuhudhuria kikao hicho na kuiacha bajaji ikifanya kazi.
Ona sasa RPC kawasababishia waendesha bajaji hasara kubwa kwani vijana hao hawakufanya kazi kutwa nzima. Wakati waendesha bajaji wakikosa riziki kwa sababu ya kikao hicho, mwenzetu RPC sidhani kama anajali kwani yeye mshahara wake uko palepale!!
Sina hakika kama afande huyo anajali adha waliyoipata wakazi wa jiji la Mbeya kwa kukosa huduma hiyo.
Hakika waendesha bajaji wanapaswa kufidiwa kwa hasara hiyo iliyosababishwa na ufinyu wa busara za viongozi. Wakuu wajifunze kujali shida za vijana hawa wanaojishughulisha kwa kazi halali.
Ni wakati wa waendesha bajaji kuungana kutetea haki zenu. Epukeni viongozi ndumilakuwili. Fagieni viongozi wote wasaliti hata ikibidi "kuwaloga"!!!
Iliamriwa kwamba waendeshaji wote wasiendelee kusafirisha abiria wakati wote wa kikao na RPC huyo.
Inaelezwa kwamba kikao hicho hakikuwa na lolote jipya zaidi ya blabla na kupotezeana muda. Sikuona sababu ya kusimamisha usafiri huo kwa kutwa nzima wakati mmiliki au mwakilishi mwingine angeweza kuhudhuria kikao hicho na kuiacha bajaji ikifanya kazi.
Ona sasa RPC kawasababishia waendesha bajaji hasara kubwa kwani vijana hao hawakufanya kazi kutwa nzima. Wakati waendesha bajaji wakikosa riziki kwa sababu ya kikao hicho, mwenzetu RPC sidhani kama anajali kwani yeye mshahara wake uko palepale!!
Sina hakika kama afande huyo anajali adha waliyoipata wakazi wa jiji la Mbeya kwa kukosa huduma hiyo.
Hakika waendesha bajaji wanapaswa kufidiwa kwa hasara hiyo iliyosababishwa na ufinyu wa busara za viongozi. Wakuu wajifunze kujali shida za vijana hawa wanaojishughulisha kwa kazi halali.
Ni wakati wa waendesha bajaji kuungana kutetea haki zenu. Epukeni viongozi ndumilakuwili. Fagieni viongozi wote wasaliti hata ikibidi "kuwaloga"!!!