Bado nipo Arusha, bata limeninogea

Arusha noma mkuu, mimi na miezi nane sasa bata lake aibu, yaani watoto wazuri wa kirangi, kimbulu wepesiii. Arusha hali ya hewa safiiiiiiiiii ndio maana bata lake zuri. Pin Point, Picnic, Sky Lounge, Good Hope na Mount Point ndio viwanja vyangu KARIBU ARUSHA MKUU
 
Wakuu hamjambo?

Nilitegemea kurudi [HASHTAG]#DarCityBaby[/HASHTAG] ila kila nikikumbuka hilo joto, na mikelele, na mji ulivyojaa matapeli, kwakweli nakosa hamu. Ila sababu kubwa ni Bata kuninogea hapa Arusha city, kwakweli huu mji ni Paradise ndogo.

Hujakaa sawa toto la kichaga hili hapa, ukiangalia kulia kuna hafcast wa kimarekani na kibongo unachat chat nae, hujashusha glass mara muhudumu anabadilishana nigh shift na mchina....tchaaaa

Nimetembelea viwanja ila naona ni vingi mnooo wadau, nilianza Zest, Pin Point, Viavia, Figgy Tree, nk...yaani nikaona nipumzike maana ni full raha, hali ya hewa inabamba, madon hayana stress, kwakeli nataka nihamie huku.

Pia nimenotice Trending news za Dar huku hazipewi shobo kabisa, yaani watu hawana time na udaku au big news sijui Lulu kaachiwa, mara Kiba amekwama YouTube, au sijui Magufuli katisha watu tena, yaani huku ni kama watu na nchi yao na mambo yao.

Arusha tamu sana. Niishie hapo
Peleka ma uzinzi yako huko...
 
TUNAANIKA NA KUWEKA HADHARANI MTANDAO NA SAFU YA WAHUSIKA WA UTAPELI, UNYAG’ANYI NA UPOKONYAJI DHALIMU (VITENDO VYA UHALIFU/JINAI) WA NYUMBA YA MJANE PRUKERIA PONCIAN BALILEMWA, MALI YA MUMEWE MAREHEMU PONCIAN P. BALILEMWA KIWANJA NA. 95 KITALU G, CT. NO. 1151 KATA YA NYAMANORO JIJINI MWANZA KWA UMMA NA MBELE YA MAHAKAMA KUU YA RUFAA KAMA IFUATAVYO:-


SEHEMU YA KWANZA


1. Benki – “NATIONAL BANK OF COMMERCE LIMITED (THE DEFUNCT)

Wamegundulika kuhusika na mchezo mchafu wa utapeli wa kudai mkopo usiojulikana juu ya nyumba tajwa wakitumia mawakili wa kampuni ya IMMMA – hasa waheshimiwa mawakili Bw. Zephrine Galleba, Sadock D. Magai, Lau K. Masha na Faustine Anton Malongo – kuanzia mwaka 2000/2001 – 2003, 2003 – 2006, 2009 – hadi sasa. Katika miaka yote hii benki ya NBC LTD ilikuwa haipo (ilifanyiwa marekebisho na kuzaa NMB, NBC – 1997 LTD na CHC – Mkusanyaji madeni ya benki ya zamani ya NBC LTD), 1997.

- Wahusika wa benki ya NBC LTD waliojitokeza na kuteua kampuni ya IMMMA na kuwaidhinisha kuwa ni kabidhi/mfilisi wa kuuza nyumba isio na mkopo wowote ni :- GERALD JORDAAN (Mkurugenzi), A.M. MINJA, DEREK DE VILLIERS (Makao makuu DSM) – Manager Collections na Meneja wa Tawi la NBC LTD – MWANZA (Demand notices of 2000 & 2001).

- Kesi Na. 117/2001 MAHAKAMA YA WILAYA YA MWANZA PRUKERIA PONCIAN BALILEMWA DHIDI YA NATIONAL BANK OF COMMERCE. Mshitakiwa NBC LTD aliweka pingamizi dhidi ya kushitakiwa kwake akidai si mhusika wa mkopo daiwa wala hahusiki kukusanya madeni ya benki mfu ya NBC LTD bali mhusika ni shirika la CHC (CONSOLIDATED HOLDING CORPORATION). Uamuzi ulitolewa tarehe 14/01/2003 kwa pingamizi kukubaliwa na kuondokana na kesi dhidi yao kuwa sio wahusika. Mahakama hii ilitenda haki vyema - tunaipongeza.


2. Tarehe 13/07/2001, kupitia TANGAZO katika gazeti la NIPASHE uk. 13 KAMPUNI YA MADALALI YA COMRADE AUCTION MART & COURT BROKERS wa S.L.P 61503 DSM: 0744-262461 wakatangaza wakidai kupewa idhini na SADOCK D. MAGAI na LAU K. MASHA wa kampuni ya IMMMA (ISHENGOMA, MASHA, MUJULIZI NA MAGAI) kuuza nyumba lalamikiwa miongoni mwa nyumba zingine katika mikoa ya: MWANZA, BUKOBA, SHINYANGA, TABORA na KIGOMA.


3. Tarehe 28/11/2003 NBC LTD waliojitoa katika kesi Na. 117/2001, wakala njama na utapeli wa hali ya juu sana pasipo kufahamika wala kutoa taarifa kwa mama mjane (mdhulumiwa) Prukeria kuwa hati ya nyumba yake/ya mumewe ilifanyiwa uhawilishaji (TRANSFER) kwa na kuwa ni mali ya RIZIKI MBISE (Maarufu kama MAMBO YA CHINGA), na kwamba uhawilishaji huo umefanywa na benki mfu ya NBC LTD tarehe 28 Novemba 2003 na HATI YA UHAWILISHAJI WA KITAPELI ulifanywa na KAMPUNI YA IMMMA Plot No. 357 UNITED NATIONS ROAD, UPANGA, P.O.BOX 72484 DSM naye Bw. RIZIKI MBISE hati yake hiyo feki kuthibitishwa mbele ya Mh. MILLINGA, W.J – Wakili wa serikali P.o. Box 331 MWANZA tarehe 18 Desemba 2003 akitambulishwa na Bi. SOPHIA M’KITOSI. Hati ya TRANSFER inaonesha benki kuiuza kwa RIZIKI MBISE Tshs. 4,600,000.00 chini ya thamani ya majengo-nyumba ya mbele na nyuma yenye thamani ya zaidi ya tshs. 250,000,000.00


Tarehe 25/09/2000 mjane Prukeria P. Balilemwa baada ya kupokea Demand notices kadhaa kutoka NBC LTD ambayo alifahamu na kujua wazi kuwa haipo na kutilia mashaka taarifa zake za mkopo na dhamana ya nyumba visivyojulikana wala kufahamika aliamua kuiandikia benki ya NBC (1997) LTD – The Director Collections kutaka kujua kama wao ndio wadai/wakopeshaji watoe ushirikiano kwake kwa kumpa taarifa kamilifu na za uhakika kama kuna mkopo-daiwa kwa marehemu mumewe asioujua ambao haujui ili ashirikishe wanafamilia kutatua tatizo na adha ya kusumbuliwa-sumbuliwa na taarifa nyingi za kampuni ya IMMMA. Barua hiyo iliyonakiliwa kwa Branch Manager, Nyerere Road-Mwanza ilitumwa Posta kwa njia ya rejesta tarehe 27/09/2000. Tangia kutumwa kwa barua hiyo hadi leo haijawahi kujibiwa wala benki kujitokeza kujibu lolote licha ya jitihada nyingi za mlalamikaji-mdhulumiwa kufika mala kadhaa NBC (1997) LTD kupewa taarifa pasipo mafanikio yoyote.


4. Mamlaka za ardhi ambazo zinatuhumiwa kuhusika na mchezo huo mchafu wa hadaa, utapeli na utwaaji wa kidhalimu wa nyumba – lalamikiwa ni Ofisi/idara ya usajiri wa Hati-Mwanza Bi. Mziray kwa tarehe tofauti tofauti katika mwaka wa 2005 kwa kuhusika na usajili wa uhawilishaji umiliki (transfer) na kubadili jina la mmiliki halisi na halali kwenda kwa mmiliki wa kitapeli Bw. Riziki Mbise. Mamlaka nyingine ni HALMASHAURI YA JIJI LA MWANZA. Halmashauri hii ikijua wazi kuwa mmiliki wa ardhi/nyumba bishaniwa kuwa ni Poncian Petro Balilemwa kwa uchunguzi rasmi uliofanyika (official search) miaka ya 2006 na 2009 ilibainisha kuwa ni miliki ya Bw. Balilemwa. Lakini ilipofika tarehe 12/10/2009 wakatoa taalifa watendaji watatu (3) tofauti kwa tarehe hiyo hiyo na wenye majina yaliyofichika, saini zisizojulikana na vyeo (designations) visivyotambulika kuwa mmiliki ni RIZIKI KALEBI MBISE.


NB: (i) PONGEZI KWA HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILEMELA PALIPO NYUMBA YENYE MGOGORO KWA UMAKINI NA KUMTAMBUA MMILIKI HALALI WA NYUMBA HUSIKA KUWA NI PONCIAN PETRO BALILEMWA TANGIA MWANZO 1980s – 2015/2018 NA KUWA NDIYE MWENYE JUKUMU, PIA, LA KULIPA KODI ZA ARDHI NA PANGO.

(ii) Baada ya taarifa hii tutaendelea kuwasilisha taarifa juu ya mamlaka za: WIZARA YA ARDHI NA NYUMBA, TAASISI ZA UCHUNGUZI kuhusiana na uhalifu, rushwa, usimamizi na utoaji wa haki kwa namna walivyoshiriki na kendelea kushiriki kuipotosha sheria na kuipokonya haki bila huruma, maadili na kanuni za utendaji na bila kuzingatia utawala wa sheria.


TUNA USHAHIDI WA KUTOSHA NA USIOTILIWA MASHAKA NA KAMWE HATUMWONEI MTU NA HATUTARAJII MTU KUONEWA, BALI NAOMBA MKUU WA NCHI, RAIS WETU MR. DKT JOHN POMBE JOSEPH MAGUFURI AIAGIZE MAMLAKA HUSIKA ZIWAJIBIKE KWA HAKI.



Chanzo: 1. Wanafamilia (mama mjane) 12/05/2018

2. TBC1 Habari - 11/05/2018
 
mkuu viwanja vya kizamani hivyo....NJOO THE DON CLUB,kula nyama pori TEMBO club,VICHECHE PALE PHILIPS KUNA CLUB MOJA IKO GOROFANI.....
 
Mkuu bado hujaiona arusha huko ni viwanja vichafu ,supu asubuhi kapige stadium bar au ppicnic bar/mchana kale rose garden club ,bot club kisha pita the fuzz kisha mjengoni olasity hutakaa urudi dar
Wabobezi Utawajua Tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom