Bado naishangaa (admire) Urusi

Bado naishangaa (admire) Urusi

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2017
Posts
10,557
Reaction score
19,107
Wataalazmu wa mambo ya intelijensia naomba msaada wenu, uzoefu wangu ni wakusoma vitabu vya espionage ziwe za kitechnolojia, uchumi , kijeshi au za kisiasa zinazohusisha mataifa makubwa ulimwenguni zikiwemo nchi za Marekani, Ulaya ya Magharibi kama Uingereza, Ujerumani Ufaransa na hata zilizokua nchi za kisoshalist za Ulaya ya Mashariki ikiwemo Urusi na Mashariki ya kati Israel ikiwa kinara

Katika usomaji wangu nakuta mara nyingi Urusi inafanya mambo ambayo kiakili unaona hayawezekani. Utakuta Shirika la Ujasusi la Urusi wakati huo linaitwa KGB(sijui sasa linaitwaje) linaendesha (lina run) ma agent wa CIA na kuwafanya kua double agents, yaani CIA agents wanakua informers kwa faida ya Urusi! Tena sio ofisa mmoja wa CIA au wawili ni kwa makumi kama ambavyo Marekani nao wanakua na watu wao ambao wana wa run ma agent wa Kirusi!

Kwa upeo mdogo wa mambo haya niliyokua nao naona ajabu sana Marekani kufanyiwa kitu hiki na Urusi mpaka najiuliza au ni kwavile vitabu ninavyosoma vingi ni fiction labda maana wahusika na matukio ya kubuni tu? Urusi kama inavyofanya Marekani ina run ma agents wa Nchi za Magharibi na kuna wengine wana defect kabisa na kuhamia Urusi!

Bado najiuliza kuna power ya Russia ambayo sisi hatuijui ila Marekani wanaitambua na kuiheshimu?Au Amerika inakua overrated na Russia inalijua hilo kwa hivyo hawaigopi?

Hapa nimemaliza kusoma litabu cha Frederick Forsyth THE DEVIL'S ALTERNATIVE, THE FOUTH PROTOCAl. Hawa jamaa wanapelelezana na wanajuana na huwezi jua nani zaidi. Ila sema tu kitabu ni fiction so sijui ukweli ukoje. Kama kuna anejua atupe darasa wana JF
 
Issue ni kuwa,Warusi walikuwa hawaingiliki kirahisi,sababu ni jamii tofauti na magharibi,na hivyo kuinsert asset katika soviet ilikuwa ngumu zaidi kuliko warusi kujiingiza nchi kama marekani,
Mrusi angeweza kukimbilia marekani kwa kisingizio kama mkimbizi,kumbe ni agent.
Pia mrusi alikuwa ananunua sana ma agents kwa kuwafanya wawe double agents wa kuwaletea information,
Walichokuwa wanazidiwa wamarekani ni Humint ,
Lakini kwa dunia mzima,kwa mambo ya kijasusi kwasasa marekani anatisha.
Has a kwa Electronics intelligence,ELINT,SIGINT
 
Issue ni kuwa,Warusi walikuwa hawaingiliki kirahisi,sababu ni jamii tofauti na magharibi,na hivyo kuinsert asset katika soviet ilikuwa ngumu zaidi kuliko warusi kujiingiza nchi kama marekani,
Mrusi angeweza kukimbilia marekani kwa kisingizio kama mkimbizi,kumbe ni agent.
Pia mrusi alikuwa ananunua sana ma agents kwa kuwafanya wawe double agents wa kuwaletea information,
Walichokuwa wanazidiwa wamarekani ni Humint ,
Lakini kwa dunia mzima,kwa mambo ya kijasusi kwasasa marekani anatisha.
Has a kwa Electronics intelligence,ELINT,SIGINT
Asante kwa maelezo yako mkuu, nadhani wamarekani wapo vizuri sasa hivi kwa kushirikiana na Israel japo ilikua hivyo toka zamani

Lakini kwanini Urusi inapoingilia kati jambo ambalo Marekani inalifanya US wana compromise au wanarudi nyuma kama issue ya Syria?
 
Issue ni kuwa,Warusi walikuwa hawaingiliki kirahisi,sababu ni jamii tofauti na magharibi,na hivyo kuinsert asset katika soviet ilikuwa ngumu zaidi kuliko warusi kujiingiza nchi kama marekani,
Mrusi angeweza kukimbilia marekani kwa kisingizio kama mkimbizi,kumbe ni agent.
Pia mrusi alikuwa ananunua sana ma agents kwa kuwafanya wawe double agents wa kuwaletea information,
Walichokuwa wanazidiwa wamarekani ni Humint ,
Lakini kwa dunia mzima,kwa mambo ya kijasusi kwasasa marekani anatisha.
Has a kwa Electronics intelligence,ELINT,SIGINT
Majibu ni ngumu sana kuyapata kwa maneno ila kwa vitendo na nyia nyepesi sana.ni ngumu sana kujua technologia ya warusi kwa sababu ni watu wenye usiri mkubwa sana katika nchi yao
 
Asante kwa maelezo yako mkuu, nadhani wamarekani wapo vizuri sasa hivi kwa kushirikiana na Israel japo ilikua hivyo toka zamani

Lakini kwanini Urusi inapoingilia kati jambo ambalo Marekani inalifanya US wana compromise au wanarudi nyuma kama issue ya Syria?
Kama waliweza kuingilia electoral systerm za marekani jiulize hao watu wapo vipi katika upande wa systerm.maana kila mtu anajua vizuri uwezo wa marekani katika upande wa systerm.
Edward snowder alitaja mataifa yote yaliyodukuliwa na Shirika la ujajusi la marekani,lakini katika mataifa hayo yaliyotajwa taifa la Urusi alikuwepo.je! inamaana wamarekani awakuwa wanaitaji information zozote kuroka Urusi? .vitu vya kujiuliza sana akika lazima upate majibu
 
Asante kwa maelezo yako mkuu, nadhani wamarekani wapo vizuri sasa hivi kwa kushirikiana na Israel japo ilikua hivyo toka zamani

Lakini kwanini Urusi inapoingilia kati jambo ambalo Marekani inalifanya US wana compromise au wanarudi nyuma kama issue ya Syria?
Inafikaga tu mahali,marekani wanajishitukia,mfano Syria ni mshirika wa Russia toka zamani,
Russia inaheshimu washirika wa marekani,hapo marekani haheshimu washirika wa Russia,
Kinachotokea Syria,ni kuwa imekuwa nchi muhimu kwa Russia kukubali kumwacha Assad aanguke,
Kwa hiyo wanapoona fujo za marekani hapo,Russia wao wanastick mwenye point,na kufuata malengo yao tu,wala hawajibishani sana na marekani zaidi ya kufanya vitendo,
Mtakumbuka Assad alizidiwa kabisa na Isis,na kama sio,Iran kuwahisha wapiganaji wa hezb,Assad angeanguka.
Pamoja na hiyo,Isis waliendelea kumpa Assad wakati ngumu,na marekani akaanza kubet kuwa Assad hamalizi miezi 6 ataanguka,
Kisha ghafla,wakashitukia mrusi kashusha ndege za kivita hapo ,Syria bila hats kuziona zimepita wapi,
Inakuwa ngumu sasa kwa marekani kuendelea na kampeni ya kumtoa Assad,kwa kuhofia kugongana na mrusi
 
Issue ni kuwa,Warusi walikuwa hawaingiliki kirahisi,sababu ni jamii tofauti na magharibi,na hivyo kuinsert asset katika soviet ilikuwa ngumu zaidi kuliko warusi kujiingiza nchi kama marekani,
Mrusi angeweza kukimbilia marekani kwa kisingizio kama mkimbizi,kumbe ni agent.
Pia mrusi alikuwa ananunua sana ma agents kwa kuwafanya wawe double agents wa kuwaletea information,
Walichokuwa wanazidiwa wamarekani ni Humint ,
Lakini kwa dunia mzima,kwa mambo ya kijasusi kwasasa marekani anatisha.
Has a kwa Electronics intelligence,ELINT,SIGINT
Mkuu dunia nzima ujasusi si namba mojaMmarekani, Pakistan kamzidii, orodha ya kijasusi wanaongoza duni ni ISI ya Pakistan ndiyo inaongoza.

Top 10 Most Powerful Intelligence Agencies In The World 2018
 
Kisha ghafla,wakashitukia mrusi kashusha ndege za kivita hapo ,Syria bila hats kuziona zimepita wapi,
Inakuwa ngumu sasa kwa marekani kuendelea na kampeni ya kumtoa Assad,kwa kuhofia kugongana na mrusi
Uchambuzi wako uko makini sana mkuu. Kwa hiyo hao jmaa wanawekeana tu heshima ingawa Marekani wakati mwingine inataka kujionyesha kwa mataifa mengine kua hawana Taifa wanaloliogopa

Ingawa naskia China pia kwa sasa inaogopewa na pande zote mbili kwa kua kwanza hua hawatoi statistics za kweli katika mambo yao mengi. Hata takwimu zao kuhusu ukuaji wao wa uchumi kuna watu wanazitilia shaka kua za uongo, eti wana underestimate muwaone bado wapo chini ingawa kiuhalisia yaweza kua sawa au hata kuipita America na kua the first economy in the world na military-wise wapo juu sana
 
Aliecompose hiyo atakuwa anaota
Na mimi nilikua nashaangaa, hiyo Pakistan ina nini cha zaidi? Technolojia anampita Marekani? Mbona kuna oparations zingine za kijasusi hua zinafanywa na Marekani ndani ya Pakistani na wenyewe hawajui, wakija kushtuka wenzao washamliza mission yao
 
Tena huyo Marekani kapanda mwaka huu hadi namba mbili, alishika nafasi ya nne. ISI ya Pakistan akiongoza, akafuatia RAW ya India, akaja MOSSAD ya Israel ndiyo ikaja CIA.

Wanaume wa kazi hawana tambo za media wao ni kimyakimya
MOSSAD na CIA oparations zao over the years zinajulikana na hata missions walizo zi accomplish successfully zinajulikana.
Its conspired kua hata kuanguka kwa iliyokua USSR kuna mkono wa CIA katika longtime mission plans zao ambapo watu wanawaguna guna kina Mikhail Gorbachev na Boris Yeltsin walioanzisha Glasnost na Perestroika zilizoisambaratisha USSR walikua wakifanya kazi kwa maslahi ya America

Sasa kuilinganisha ISI na CIA au MOSSAD nadhani si sawa mkuu
 
Na mimi nilikua nashaangaa, hiyo Pakistan ina nini cha zaidi? Technolojia anampita Marekani? Mbona kuna oparations zingine za kijasusi hua zinafanywa na Marekani ndani ya Pakistani na wenyewe hawajui, wakija kushtuka wenzao washamliza mission yao
Mmarekani anaongoza kelele za kwenye media tu ila si ujasusi, ingia mtandaoni tafuta list zote za vyanzo vya kuaminika. ISI ndiyo namba moja.
 
MOSSAD na CIA oparations zao over the years zinajulikana na hata missions walizo zi accomplish successfully zinajulikana.
Its conspired kua hata kuanguka kwa iliyokua USSR kuna mkono wa CIA katika longtime mission plans zao ambapo watu wanawaguna guna kina Mikhail Gorbachev na Boris Yeltsin walioanzisha Glasnost na Perestroika zilizoisambaratisha USSR walikua wakifanya kazi kwa maslahi ya America

Sasa kuilinganisha ISI na CIA au MOSSAD nadhani si sawa mkuu
Kwani hao ISI mission zao hazijulikani?

Inter-Services Intelligence - Wikipedia

Inter-Services Intelligence activities in the United States - Wikipedia
 
Back
Top Bottom