Baba Tunakukumbuka

Baba Tunakukumbuka

Fall Army Worm

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2015
Posts
19,371
Reaction score
14,481
Ni usiku wa manane, na ndoto inanijia,
Leo hii jumanne, ndio imenitokea,
Katika kiza kinene, na wewe umenijia,
Baba tunakukumbuka,ulale pema peponi,

Ni mengi tumeongea, nilipokuwa ndotoni,
Pia ukatuusia, ya kufaa maishani,
Nami nikafurahia, pasi jua ni ndotoni,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Upendo uso kifani, baba ulituonyesha,
Ukatutoa kizani, kutufundisha maisha,
Tukapelekwa shuleni, ujinga ukakomesha,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Ulifunza uzalendo, tuijenge nchi yetu,
Ukatufunza upendo, ili iwe tunu kwetu,
Hata walo kandokando,walijifunzia kwetu,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika,
Wanao tunateseka, tunazidi kupigika,
Hayawani watusaka, himaya wameiteka,
Yote uliyokataza, wenzio wanaharibu,

Wale waliokutii, leo wamekugeuka,
Leo hawafuatilii, wote wamekengeuka,
Watoto hatutulii, twazidi Kulalamika,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Uchumi uloujenga, wenzako wauvuruga,
Wanatuona Wajinga,ndio maana watupiga,
Tena wanatusimanga,hata pasipo uoga,
Maisha yetu magumu,kila kona wamebana,

Wale maadui zetu,leo ni wetu rafiki,
Wanataka Mali zetu,waondoke nazo nduki,
Tutabaki bila kitu,kisa urafiki feki,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Wale ulowakataa,amewaleta chumbani,
Vinono wanajilia,na kuficha kibindoni,
Makapi twaambulia,sisi jama masikini,
Mali ulotuachia,zinaliwa na Wahuni,

Mara nikashitukia, ndoto imeniishia,
Nikabaki ninalia,ukiwa kutuachia,
Nani wa kutusemea,watesi kuwaondoa?,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,
 
Kila rais ana kurasa yake kwenye kitabu cha nchi yetu...historia itahukumu..kwasasa tumuunge mkono rais wetu kwa nguvu zote...ingawa kitendo cha January ku abandoni mradi wa Stieglers Gorge na kuelekea "Kusini" kunanikosesha usingizi..ifike mahali tutofautishe kati ya miradi ya kisiasa versus miradi ya kimkakati ya kitaifa. Mradi huu ulipaswa usukumwe kwa nguvu zote, regardless rais atakayekuja anatokea chama gani mabadiliko ya vipaumbele yafanyike kwenye miradi ya kisiasa, sio mikakati ya kitaifa. Idara ya Usalama mngelisimamia hili suala nyeti.
 
Hivi mgao wa umeme ni masaa mangapi?
Au kutwa nzima?
 
Kwa upande wangu Mimi naona yanayoendelea yote ni sawa tu, watanzania tumezidi unafki. Kagufuli alijitoa sana kuipambania nchi hii lakini tuksungana na wezi kumshambulia na kumtukana.
Na bado yajayo yanafurahisha
 
Ni usiku wa manane, na ndoto inanijia,
Leo hii jumanne, ndio imenitokea,
Katika kiza kinene, na wewe umenijia,
Baba tunakukumbuka,ulale pema peponi,

Ni mengi tumeongea, nilipokuwa ndotoni,
Pia ukatuusia, ya kufaa maishani,
Nami nikafurahia, pasi jua ni ndotoni,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Upendo uso kifani, baba ulituonyesha,
Ukatutoa kizani, kutufundisha maisha,
Tukapelekwa shuleni, ujinga ukakomesha,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Ulifunza uzalendo, tuijenge nchi yetu,
Ukatufunza upendo, ili iwe tunu kwetu,
Hata walo kandokando,walijifunzia kwetu,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika,
Wanao tunateseka, tunazidi kupigika,
Hayawani watusaka, himaya wameiteka,
Yote uliyokataza, wenzio wanaharibu,

Wale waliokutii, leo wamekugeuka,
Leo hawafuatilii, wote wamekengeuka,
Watoto hatutulii, twazidi Kulalamika,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Uchumi uloujenga, wenzako wauvuruga,
Wanatuona Wajinga,ndio maana watupiga,
Tena wanatusimanga,hata pasipo uoga,
Maisha yetu magumu,kila kona wamebana,

Wale maadui zetu,leo ni wetu rafiki,
Wanataka Mali zetu,waondoke nazo nduki,
Tutabaki bila kitu,kisa urafiki feki,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Wale ulowakataa,amewaleta chumbani,
Vinono wanajilia,na kuficha kibindoni,
Makapi twaambulia,sisi jama masikini,
Mali ulotuachia,zinaliwa na Wahuni,

Mara nikashitukia, ndoto imeniishia,
Nikabaki ninalia,ukiwa kutuachia,
Nani wa kutusemea,watesi kuwaondoa?,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,
Kwani aliwaambia nchi ni ya wasukuma,tuliingia cha kike sana kwa yule mzee,
 
Kila rais ana kurasa yake kwenye kitabu cha nchi yetu...historia itahukumu..kwasasa tumuunge mkono rais wetu kwa nguvu zote...ingawa kitendo cha January ku abandoni mradi wa Stieglers Gorge na kuelekea "Kusini" kunanikosesha usingizi..ifike mahali tutofautishe kati ya miradi ya kisiasa versus miradi ya kimkakati ya kitaifa. Mradi huu ulipaswa usukumwe kwa nguvu zote, regardless rais atakayekuja anatokea chama gani mabadiliko ya vipaumbele yafanyike kwenye miradi ya kisiasa, sio mikakati ya kitaifa. Idara ya Usalama mngelisimamia hili suala nyeti.
Kweli mkuuu
 
Kwa upande wangu Mimi naona yanayoendelea yote ni sawa tu, watanzania tumezidi unafki. Kagufuli alijitoa sana kuipambania nchi hii lakini tuksungana na wezi kumshambulia na kumtukana.
Na bado yajayo yanafurahisha
📌📌📌📌📌
 
Jana nimekosa dili la pesa ndefu,kwa upuuz mgao wa kukata umeme,sm siku hz u si ajabu mtu akawa hapatkan siku nzma kisa umeme hakuna.wk iliyopta nimeahindwa kufanya Kaz zangu kwa Uhuru,neingia saluni jamaa kanyoa ndevu upqnde mmoja umeme ukakata jumla!
 
Ni usiku wa manane, na ndoto inanijia,
Leo hii jumanne, ndio imenitokea,
Katika kiza kinene, na wewe umenijia,
Baba tunakukumbuka,ulale pema peponi,

Ni mengi tumeongea, nilipokuwa ndotoni,
Pia ukatuusia, ya kufaa maishani,
Nami nikafurahia, pasi jua ni ndotoni,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Upendo uso kifani, baba ulituonyesha,
Ukatutoa kizani, kutufundisha maisha,
Tukapelekwa shuleni, ujinga ukakomesha,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Ulifunza uzalendo, tuijenge nchi yetu,
Ukatufunza upendo, ili iwe tunu kwetu,
Hata walo kandokando,walijifunzia kwetu,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Tangu ulipoondoka, mambo yamebadilika,
Wanao tunateseka, tunazidi kupigika,
Hayawani watusaka, himaya wameiteka,
Yote uliyokataza, wenzio wanaharibu,

Wale waliokutii, leo wamekugeuka,
Leo hawafuatilii, wote wamekengeuka,
Watoto hatutulii, twazidi Kulalamika,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Uchumi uloujenga, wenzako wauvuruga,
Wanatuona Wajinga,ndio maana watupiga,
Tena wanatusimanga,hata pasipo uoga,
Maisha yetu magumu,kila kona wamebana,

Wale maadui zetu,leo ni wetu rafiki,
Wanataka Mali zetu,waondoke nazo nduki,
Tutabaki bila kitu,kisa urafiki feki,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,

Wale ulowakataa,amewaleta chumbani,
Vinono wanajilia,na kuficha kibindoni,
Makapi twaambulia,sisi jama masikini,
Mali ulotuachia,zinaliwa na Wahuni,

Mara nikashitukia, ndoto imeniishia,
Nikabaki ninalia,ukiwa kutuachia,
Nani wa kutusemea,watesi kuwaondoa?,
Baba tunakukumbuka, ulale pema peponi,
Hongera sana utenz mzuri utatufundisha mengi
 
CCM ndiye adui mkubwa wa taifa letu. CCM hawataki katiba mpya, CCM hawataki tume huru na ya haki ya uchaguzi.

Watoto wa vizito wa CCM wanasoma nje ya nchi na shule za kifahari nchini, watoto wetu wanapewa elimu duni kwenye shule za kata
 
Kwa upande wangu Mimi naona yanayoendelea yote ni sawa tu, watanzania tumezidi unafki. Kagufuli alijitoa sana kuipambania nchi hii lakini tuksungana na wezi kumshambulia na kumtukana.
Na bado yajayo yanafurahisha
Sema vizuri, uliungana na mwizi yupi kumshambulia Magumashi?
 
Back
Top Bottom