Baba mwenye nyumba kanisusia kodi yake

kzba

JF-Expert Member
Jun 19, 2014
1,355
789
Katika hali isiyo ya kawaida baba mwenye nyumba kanisusia kodi yake yapata siku ya 15 sasa tangia kodi yangu ya awali kwisha, niliingia kwenye hii nyumba mwaka jana mwezi wa tano kwa makubaliano kuwa nitalipa kodi ya miezi 10 ingawa sikuwa tayari kwa hiyo kodi kulipa kutokana na kipato changu.

Niliomba nimpatie kodi ya miezi 6 akakataa akasema yeye anahitaji kodi ya mwaka ili anifanyie marekebisho kwenye hii nyumba, kama kuniwekea fensi na kukarabati ndani lakini kinyume na makubaliano hakutimiza wala jambo moja mpaka hii leo, akaniambia nijitahidi walau nimpe kodi ya miezi kumi ili aweze kufanya hayo marekebisho.

Kwa maelezo yake kuwa kila mpangaji anapoingia kwa hii nyumba yake sharti umpe kodi ya mwaka alafu kodi inayofuata unalipa miezi 6 ingawa ki uhalisia haifanani kabisa kwa kulipa hiyo kodi ya mwaka ila kwa kuwa nilikuwa na uhitaji wa nyumba kwa haraka kwa wakati huo nikaona siyo kesi acha nimpe tena bila mkataba coz yeye anaishi mkoani huko.

Baada ya miezi kadhaa baadae akaniambia nimmalizie ile kodi ya miezi miwili iliyobaki coz nilimpa miezi kumi kinyume na makubaliano pia coz yeye alisema tu nimpe kodi ya miezi kumi ili afanye hayo mambo tukabishana sana nikaona acha tu nimpe coz bado naendelea kuishi hapa.

Kwa kuwa yeye hakufanya yale mambo alionihaidi mi nikaufanya ule ukarabati wa ndani kwa sababu miundo mbinu mingi ilikuwa imekufa na inaonesha ilikaa muda mrefu bila mpangaji kwa makubaliano nitampatia risiti za gharama halisi ili tu deduct kwa kodi inayofuata.

Sasa kodi imeisha nataka kumtumia kodi yake ya miezi 6 anasema nimsubiri mpaka aje hii ni wiki ya pili tangia anihaidi kuja lakini hajatokea, na mambo ya pesa nafikiri wadau mnafahamu ni za kuunga unga
Je nimfanyeje huyu mtu kabla hajaleta madhara kwangu
Na kisheria ikoje kama mtu anakiuka makubaliano ingawa si kimaandishi ila nina meseji zake zote kuhusiana na haya maelezo niliotoa hapa.

Nategemea michango iliyotukuka
Asanteni.
 
View attachment 346013

Katika hali isiyo ya kawaida baba mwenyenyumba kanisusia kodi yake yapata siku ya 15 sasa tangia kodi yangu ya awali kwisha, niliingia kwa hii nyumba mwaka jana mwezi wa tano kwa makubaliano kuwa nitalipa kodi ya miezi 10 ingawa sikuwa tayari kwa hyo kodi kulipa kutokana na kipato changu coz niliomba nimpatie kodi ya miezi 6 akakataa akasema yeye anahitaji kodi ya mwaka ili anifanyie marekebisho kwa hii nyumba kama kuniwekea fensi na kukarabati ndani lkn kinyume na makubaliano hakutimiza wala jambo moja mpaka hii leo, akaniambia nijitahidi walau nimpe kodi ya miezi kumi ili aweze kufanya hayo marekebisho kwa maelezo kuwa kila mpangaji anapoingia kwa hii nyumba yake sharti umpe kodi ya mwaka alafu kodi inayofuata unalipa miezi 6 ingawa ki uhalisia haifanani kabisa kwa kulipa hyo kodi ya mwaka ila kwa kuwa nilikuwa na uhitaji wa nyumba kwa haraka kwa wakati huo nikaona siyo kesi acha nimpe tena bila mkataba coz yeye anaishi mkoani huko
baada ya miezi kadhaa baadae akaniambia nimmalizie ile kodi ya miezi miwili iliyobaki coz nilimpa miezi kumi kinyume na makubaliano pia coz yeye alisema tu nimpe kodi ya miezi kumi ili afanye hayo mambo tukabishana sana nikaona acha tu nimpe coz bado naendelea kuishi hapa
Kwa kuwa yeye hakufanya yale mambo alionihaidi mi nikaufanya ule ukarabati wa ndani kwa sababu miundo mbinu mingi ilikuwa imekufa na inaonesha ilikaa muda mrefu bila mpangaji kwa makubaliano nitampatia risiti za gharama halisi ili tu deduct kwa kodi inayofuata.

Sasa kodi imeisha nataka kumtumia kodi yake ya miezi 6 anasema nimsubiri mpaka aje hii ni wiki ya pili tangia anihaidi kuja lakini hajatokea, na mambo ya pesa nafikiri wadau mnafahamu ni za kuunga unga
Je nimfanyeje huyu mtu kabla hajaleta madhara kwangu
Na kisheria ikoje kama mtu anakiuka makubaliano ingawa si kimaandishi ila nina messeji zake zote kuhusiana na haya maelezo niliotoa hapa.

Nategemea michango iliyotukuka
Asanteni.

Kama mlikubaliana urekebishe, unaweza fuata sheria ila kama alikuahidi tu, imekula kwako.
 
Unapompa kodi huwa kuna mikataba mnasaini??
Masharti ya mkataba wako yakoje??

Kama hakuna mkataba aisee, anaweza kukuruka futi 100
 
Unapompa kodi huwa kuna mikataba mnasaini??
Masharti ya mkataba wako yakoje??

Kama hakuna mkataba aisee, anaweza kukuruka futi 100
Baadae alinipa mkataba unaosema ukiingia kwa mara ya kwanza unalipa ya mwaka kodi zinazofuata ninmiezi 6 sasa ndo hapo nashindwa kumwelewa anataka tuongee nn wakati sharti lake la hyo kodi ya mwaka nilishalitimiza kwa kodi ile ya mwanzo mkuu.
 
Usiogope faza hause nowdays yuko poa kifedha.... Hana shida na vicenti vyako... We endelea kula bhata tu!
 
Halafu mwanaume kuwa na hofu za kipumbavu mnakera

yaani kabisa unamuogopa huyo mzee kabisa wakati mwenye nyumba ninapokaa anajuta kuwa na mpangaji kama mimi hayo yanayomkuta
 
Duuh! Hapo mkuu anza kutafuta nyumba nyingine. Ukiona mtu anakataa pesa, ujue anakutafutia mpangaji mwingine hapo aje akutoe...
 
Hizo pesa usizile zihifadhi na kwa vile yeye anavyojidai yuko mbali au hana muda andaa mkataba wewe wa makabidhiano na andaa hizo risiti zako kabsaa msubiri aje umsikie anachtaka kusema, lakini pia kujipunguzia stress andaa kodi ya mwaka, hao wenye nyumba ni wakorofi sana, hata akikutamkia kwa mdogo wake rekebisha tutakatiana basi pia atakuja kukuruka.
 
Kwa uzoefu wangu utakutana na moja kati ya haya:-

1. Utatakiwa ulipe kodi yako ya miezi sita, ukarabati ulioufanya ni kwa ajili yako na uliona panafaa kuwa hivyo
2. Kodi itaongezeka kufidia hicho unachotaka kuki-deduct, na ukumbuke kwamba nyumba imepanda thamani baada ya marekebisho uliyoyafanya hivyo ukiondoka atapata mtu
3. Mkishapigiana mahesabu, atakwambia ukae bila kulipa kwa idadi ya miezi inayolingana na hizo gharama, baada ya hapo tafuta nyumba nyingine.
4. Kama mzee ni mtata anakuondoa mara moja, huna mkataba wa ujenzi wa nyuma, utapewa notice ya muda husika then unaondoka zako.

Ili usikutane na yote hayo kama kweli unataka kuendelea kukaa hapo, mlipe kodi yake tu bila kukata kitu, hii inaweza hata kusababisha asikuongezee kodi na mwendelee kuishi kwa amani.
 
1. anataka kuongeza kodi
2. anataka kumpa mpangaji mwingine ili aongeze kodi
3. anza kutafuta alternative mapema au ujiandae na ubishi na ugomvi kama utabaki
 
Katika hali isiyo ya kawaida baba mwenye nyumba kanisusia kodi yake yapata siku ya 15 sasa tangia kodi yangu ya awali kwisha, niliingia kwenye hii nyumba mwaka jana mwezi wa tano kwa makubaliano kuwa nitalipa kodi ya miezi 10 ingawa sikuwa tayari kwa hiyo kodi kulipa kutokana na kipato changu.

Niliomba nimpatie kodi ya miezi 6 akakataa akasema yeye anahitaji kodi ya mwaka ili anifanyie marekebisho kwenye hii nyumba, kama kuniwekea fensi na kukarabati ndani lakini kinyume na makubaliano hakutimiza wala jambo moja mpaka hii leo, akaniambia nijitahidi walau nimpe kodi ya miezi kumi ili aweze kufanya hayo marekebisho.

Kwa maelezo yake kuwa kila mpangaji anapoingia kwa hii nyumba yake sharti umpe kodi ya mwaka alafu kodi inayofuata unalipa miezi 6 ingawa ki uhalisia haifanani kabisa kwa kulipa hiyo kodi ya mwaka ila kwa kuwa nilikuwa na uhitaji wa nyumba kwa haraka kwa wakati huo nikaona siyo kesi acha nimpe tena bila mkataba coz yeye anaishi mkoani huko.

Baada ya miezi kadhaa baadae akaniambia nimmalizie ile kodi ya miezi miwili iliyobaki coz nilimpa miezi kumi kinyume na makubaliano pia coz yeye alisema tu nimpe kodi ya miezi kumi ili afanye hayo mambo tukabishana sana nikaona acha tu nimpe coz bado naendelea kuishi hapa.

Kwa kuwa yeye hakufanya yale mambo alionihaidi mi nikaufanya ule ukarabati wa ndani kwa sababu miundo mbinu mingi ilikuwa imekufa na inaonesha ilikaa muda mrefu bila mpangaji kwa makubaliano nitampatia risiti za gharama halisi ili tu deduct kwa kodi inayofuata.

Sasa kodi imeisha nataka kumtumia kodi yake ya miezi 6 anasema nimsubiri mpaka aje hii ni wiki ya pili tangia anihaidi kuja lakini hajatokea, na mambo ya pesa nafikiri wadau mnafahamu ni za kuunga unga
Je nimfanyeje huyu mtu kabla hajaleta madhara kwangu
Na kisheria ikoje kama mtu anakiuka makubaliano ingawa si kimaandishi ila nina meseji zake zote kuhusiana na haya maelezo niliotoa hapa.

Nategemea michango iliyotukuka
Asanteni.

Jaribu kupunguza hizo coz coz kwenye uandishi wako
 
Unakubaliana na mtu kwa maneno tu kwenye dunia hii ya leo?Haya hebu endelea kumsubiri labda anataka akuuzie hiyo nyumba kwa mkopo.
 
Back
Top Bottom