GE2025 Baba Levo na kura 88 za maoni CCM jimbo la Kigoma Mjini

GE2025 Baba Levo na kura 88 za maoni CCM jimbo la Kigoma Mjini

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini ambaye anatetea kiti hicho, Kirumba Ng’enda ameongoza kwenye kura za maoni za chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika leo, akimzidi kura 88 mpinzani wake mkuu Clayton Chipando (Baba Levo).

Akitoa matokeo ya uchaguzi huo uliofanywa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu katika Kata 19 za jimbo hilo, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kigoma Mjini Sadick Kibwana Kadulo amesema kuwa Ng’enda ameshinda kwa kura 2,168 akifuatiwa na Clayton Chipando aliyepata kura 2,080, Baruani Muhuza kura 264, Dkt. Ahmad Sovu kura 247, Maulid Kikondo kura 180, huku Moses Basila akipata kura 12.

Kadulo amesema kuwa kura 12 pekee ndizo ziliharibika, huku akieleza kuwa kuhusu tetesi za zilizokua zikisambaa mitandaoni za kukamatwa kwa kura feki katika baadhi ya vituo kuwa si taarifa za kweli.

Pia soma >> GE2025 - Baba Levo aangukia pua, Ng’enda aibuka mshindi Kigoma Mjini kwa kura 2,168 dhidi ya 2,080
 
Nilichojifunza hapa sio kushindwa kwa babalevo. Somo hapa ‘in life if you don’t try, you will never know the outcome’.

Binafsi sikutegemea B-Levo kusumbua huko, lakini almanusura abwage mtu nadhani kashangaza wengi; that’s an achievement to me.

Sasa angekuwa mmbunge wa aina gani hayo ni matatizo ya CCM.
 
Umeaangalia vyema, ila pia jiulize kama Baba Levo anaaminiwa na kidg apite.

Je wananchi wana umakini kweli na uchaguzi wa viongozi au hawajui lolote,mbungu awe baba levo kweli?
Nilichojifunza hapa sio kushindwa kwa babalevo. Somo hapa ‘in life you if you don’t try you will never know the outcome’.

Binafsi sikutegemea B-Levo kusumbua huko, lakini almanusura abwage mtu nadhani kashangaza wengi; that’s an achievement to me.

Sasa angekuwa mmbunge wa aina gani hayo matatizo ya CCM.
 
Umeaangalia vyema, ila pia jiulize kama Baba Levo anaaminiwa na kidg apite.

Je wananchi wana umakini kweli na uchaguzi wa viongozi au hawajui lolote,mbungu awe baba levo kweli?
Not ideał lakini kwa sasa ndio norm, hizi ndio siasa CCM ya Samia inazotaka watu kusifia tu.
 
Nilichojifunza hapa sio kushindwa kwa babalevo. Somo hapa ‘in life if you don’t try, you will never know the outcome’.

Binafsi sikutegemea B-Levo kusumbua huko, lakini almanusura abwage mtu nadhani kashangaza wengi; that’s an achievement to me.

Sasa angekuwa mmbunge wa aina gani hayo ni matatizo ya CCM.
IMG-20250805-WA0002.jpg
 
Nilichojifunza hapa sio kushindwa kwa babalevo. Somo hapa ‘in life if you don’t try, you will never know the outcome’.

Binafsi sikutegemea B-Levo kusumbua huko, lakini almanusura abwage mtu nadhani kashangaza wengi; that’s an achievement to me.

Sasa angekuwa mmbunge wa aina gani hayo ni matatizo ya CCM.
Ni kweli hili ni somo tosha kwa mashangingi wa mjini na madada wa bongo movie...wasijikite tu kujiuza mijini kwani kuna maisha baada ya kuzeeka. Ubunge kama mtu unachaguliwa (mwanamke) unakwenda kuliwa na wabunge wenzako kwa manufaa zaidi kabla hawajaambukizwa maradhi na kuungizwa kwenye gridi la taifa.
 
Ni kweli hili ni somo tosha kwa mashangingi wa mjini na madada wa bongo movie...wasijikite tu kujiuza mijini Imani kuna maisha baada ya kuzeeka. Ubunge kama mtu unachaguliwa (mwanamke) unakwenda kuliwa na wabunge wenzako kwa manufaa.
Aiseeeh!
 
Kwa kura alizopata tayari anaweza ameliweka jina lake sehemu nzuri anaweza kupata uteuzi wowote kama mkuu wa wilaya
 
Aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini ambaye anatetea kiti hicho, Kirumba Ng’enda ameongoza kwenye kura za maoni za chama cha Mapinduzi (CCM) uliofanyika leo, akimzidi kura 88 mpinzani wake mkuu Clayton Chipando (Baba Levo).

Akitoa matokeo ya uchaguzi huo uliofanywa na Wajumbe wa Mkutano Mkuu katika Kata 19 za jimbo hilo, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kigoma Mjini Sadick Kibwana Kadulo amesema kuwa Ng’enda ameshinda kwa kura 2,168 akifuatiwa na Clayton Chipando aliyepata kura 2,080, Baruani Muhuza kura 264, Dkt. Ahmad Sovu kura 247, Maulid Kikondo kura 180, huku Moses Basila akipata kura 12.

Kadulo amesema kuwa kura 12 pekee ndizo ziliharibika, huku akieleza kuwa kuhusu tetesi za zilizokua zikisambaa mitandaoni za kukamatwa kwa kura feki katika baadhi ya vituo kuwa si taarifa za kweli.

Huu uchaguzi una madudu jana niliona clip kwanza wakati wanahesabu kura umeme ulikatika,mara kuna clip nyingine mida ya mchana kuna watu walikamatwa na kura feki.
 
Umeaangalia vyema, ila pia jiulize kama Baba Levo anaaminiwa na kidg apite.

Je wananchi wana umakini kweli na uchaguzi wa viongozi au hawajui lolote,mbungu awe baba levo kweli?
CCM ni tatzo sana RUSHWA inatawala sana wajumbe ni maskini wana njaaa sana
 
Yes is possible , kwani Said Nkumba alipoteuliwa na Magufuli alikuwa na degree au diploma.?
Said Nkuba alipokosa ubunge Sikonge bado kidogo aende Chadema,alibembelezwa sana na by then baba yake marehemu mzee Nkuba ndo alikuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora.
Ushawishi wa ile familia na Said him self ndo ulifanya Said arudishwe kwenye reli kupitia ukuu wa Wilaya Ushirombo.
All in all sio kila aliye kosa kosa kushinda ubunge CCM ana sifa ya kuwa mkuu wa Wilaya. MAONI YANGU BINAFSI
 
Back
Top Bottom