Baba hataki nioe mama anataka nioe

Baba hataki nioe mama anataka nioe

Mtu mzima anapangiwa kuoa na mzazi wake. Kweli wanaume wa sasa wana "umama" .
 
kiukweli ndoa haitaki maigizo.kama kweli una miaka 20 na binti 25 nakushauri fata ushaur wa mzazi wako wa kiume.mke unaoa wewe na si mama yako mzazi na kamwe utamlea wewe na si mama yako.jipange kwanza ndoa siyo mchezo wa kuigiza

Late 20's na sio miaka 20.
 
Kama una miaka 29, huo umri unafaa kuwa na mke! Maana wanaume huwa tunaanza kujitambua tukiwa na miaka 28-35, na mambo mengi ya ujana huwa yanapungua. Baba yako anakupa sababu gani za msingi za kutooa? Msikilize mzee maana anauzoefu na mambo ya ndoa. Wanawake mara nyingi huwa hawana sababu za msingi kwenye mambo ya ndoa
 
labda ungemuuliza mzee maswal yafuatayo
01:km ww uko kwnye 26au zaid anataka ukifikia umrigan ndo uoe
pia mwambie umri unamchango mdog sn ktk mapenz sababu kuna watu wameoana wakiwa kwenye 40s lkn bd hawaja kua stable
02😛ia mwambie saiv maisha c km zaman life expectancy imeshuka ukijitahid sn 50s maanayake unatakiwa at least ukiwa kwenye 20s uwe umeshaoa upate wkt mzur wakulea wtt ww n mkeo
mwisho kbs ht bible imeandikwa utaacha wazaz utamfuata mkeo so we fanya kile kitu. ambacho unaskia aman moyon ucjal m2 yyt pia omba sn Mungu uwe na hekima ya kufanya hayo yt
 
Habari za mapumziko ya mwisho wa wiki wana Jf, ni matumaini yangu tu salama na tunaendelea na majukumu wengine na mapumziko ya mwisho wiki.

Ninakuja kwenu great thinkers mnisaidie kwa mawazo na ushauri juu ya mada jatwa "Baba hataki nioe, mama anataka nioe"

Natanguliza shukrani kwanza kwa msaada wa mawazo na ushauri toka kwenu.

Kama nilivyoeleza katika threed yangu ya kwanza humu iliyohusu "nimvumilie huyu mwanamke mpaka ndoa au nipige chini"
Nashukuru wengi walinipa mawazo na ushauri mzuri na hata sasa nimefikia maamuzi ila katika utekelezaji wake napata ugumu.

Tulipanga na mtarajiwa wangu yakuwa at least tujipange kuwasogeza wadogo zetu kielimu na mimi kujiendeleza hata nitakapo kuwa masomoni tufunge ndoa sasa uhitaji wa ndoa umekuwa wa haraka kwa mwenzangu sababu anategemea kumaliza chuo mwaka ujao( ingawa ni mwajiriwa ) ila baada ya kumaliza kuna kozi nyingine anatakiwa aende, ameleta hiyo demand na niliipokea na kama ilivyo desturi zetu za kiafrika lazima wazee wakubaliane nawe (wakupe baraka) ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa mambo ya muhimu ili kupewa mke kihalali.

Baada ya kumweleza mama, kama ilivyokawaida ya akina mama alifurahi sana na aliniunga mkono akinisihi nifanye mapema, Kwa upande wa mzee mambo yalikuwa tofauti hakuliunga mkono akidai bado umri ( am in late 20's) nawahi wapi kiufupi hakunielewa kabisa na alikataa, pia akilikumbushia swala wadogo zangu ambao wapo masomoni bado (wazazi hawaishi pamoja).

Binti naye anawasiliana na ma mkwe wake mtarajiwa, yakuwa nimempotezea muda na aliachana na mipango ya mahusiano na wengine kwa zaidi ya mwaka sasa leo namwambia bado (she is 25) anadai anakimbizana na umri wa kuzaa.

Mim nina kazi ya kudumu serikalini na binti naye ana kazi ya kudumu serikalini.

Naombeni msaada wa kutegea hiki kitendawili great thinkers wenzangu!
"Naomba kuwasilisha"
Kwani Muu ni kuwa na Kazi ya Kudumu au ni suala la wewe kuwa na Utayari wa Kuwa baba au Kuwa mama.. Ndoa za siku hizi zinaletwa na mihemko mingi ,. Unaona Mwanamke wako anakimbizana na Umri wa Kuzaa.. Kwa hiyo yeye anachotaka ni kuwahi Umri wa Kuzaa kwa kifupiu hakuna Ndoa hapo ila kuna Mbio za uzaa zinakimbiwa... Walkati Mzee wako anajua kuwa bado sana kwa umri wako.. Ningekushauri Ujihakikishie kuwa kama Kweli wewe upo Tayari au unataka kumridhisha Mwanamke wako ambaye yeyey hitaji lake ni Umri unakimbizana na Umri wa Kuzaa...
 
Oa mapema...zaa...tunza wanao ungali na nguvu, uepuke majuto ..umri ndo huo unakwendaaaa..Niko early 40s na ndo Nina katoto ka 1.7 yrs. Japo elimu ninayo lakini....
 
Oa mapema...zaa...tunza wanao ungali na nguvu, uepuke majuto ..umri ndo huo unakwendaaaa..Niko early 40s na ndo Nina katoto ka 1.7 yrs. Japo elimu ninayo lakini....
Asante kwa experience Mkuu
 
Back
Top Bottom