Baba hataki nioe mama anataka nioe

Baba hataki nioe mama anataka nioe

Mremaaa

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2015
Posts
293
Reaction score
325
Habari za mapumziko ya mwisho wa wiki wana Jf, ni matumaini yangu tu salama na tunaendelea na majukumu wengine na mapumziko ya mwisho wiki.

Ninakuja kwenu great thinkers mnisaidie kwa mawazo na ushauri juu ya mada jatwa "Baba hataki nioe, mama anataka nioe"

Natanguliza shukrani kwanza kwa msaada wa mawazo na ushauri toka kwenu.

Kama nilivyoeleza katika threed yangu ya kwanza humu iliyohusu "nimvumilie huyu mwanamke mpaka ndoa au nipige chini"
Nashukuru wengi walinipa mawazo na ushauri mzuri na hata sasa nimefikia maamuzi ila katika utekelezaji wake napata ugumu.

Tulipanga na mtarajiwa wangu yakuwa at least tujipange kuwasogeza wadogo zetu kielimu na mimi kujiendeleza hata nitakapo kuwa masomoni tufunge ndoa sasa uhitaji wa ndoa umekuwa wa haraka kwa mwenzangu sababu anategemea kumaliza chuo mwaka ujao( ingawa ni mwajiriwa ) ila baada ya kumaliza kuna kozi nyingine anatakiwa aende, ameleta hiyo demand na niliipokea na kama ilivyo desturi zetu za kiafrika lazima wazee wakubaliane nawe (wakupe baraka) ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa mambo ya muhimu ili kupewa mke kihalali.

Baada ya kumweleza mama, kama ilivyokawaida ya akina mama alifurahi sana na aliniunga mkono akinisihi nifanye mapema, Kwa upande wa mzee mambo yalikuwa tofauti hakuliunga mkono akidai bado umri ( am in late 20's) nawahi wapi kiufupi hakunielewa kabisa na alikataa, pia akilikumbushia swala wadogo zangu ambao wapo masomoni bado (wazazi hawaishi pamoja).

Binti naye anawasiliana na ma mkwe wake mtarajiwa, yakuwa nimempotezea muda na aliachana na mipango ya mahusiano na wengine kwa zaidi ya mwaka sasa leo namwambia bado (she is 25) anadai anakimbizana na umri wa kuzaa.

Mim nina kazi ya kudumu serikalini na binti naye ana kazi ya kudumu serikalini.

Naombeni msaada wa kutegea hiki kitendawili great thinkers wenzangu!
"Naomba kuwasilisha"
 
Wewe binafsi unataka kipi? Mi nakushaur fuata moyo wako. Mzazi ambaye utakuwa tofaut nae utamuelewesha tu naiman atakuelewa.
Nashukuru Mkuu wa ushauri wako
 
hata mimi naunga mkono hoja ya kusema bado mdogo.. kasome kwanza ujue mengi kwenye dunia..!!!
 
Jisimamie, usitegemee mawazo ya watu wengine mfano wazazi
 
Baba yako anajua kweli nyingi kuhusu mwanamke maana ameshalala na wengi, mama yako amespecialize kwa wanaume pekee, so chagua nani wa kumfuata hapo.
 
Sio kila wakati kila mtu atakubaliana na mawazo yako. Huwezi kumridhisha kila mmoja. Na swala la mimba kidini sio sahihi kupata kabla ya ndoa,.. ila likitokea huwa linawalazimishaga wengi including wazazi kutokua na maamuzi tofauti nakuoa....out of experience unaweza kufanya vivyo tena Kwa sababu binti ndio anataka ndoa hawezi kataa mimba..
Usimuoneshe 'directly' mzee kwamba hukubaliani nae, laana Sio nzuri.
 
Daah aiseeeh kuoa au kuolew n mipango ya mtu mwenyew wala hupangiw fuata akili yako ila lazima ukubali yatakayotokea
 
kiukweli ndoa haitaki maigizo.kama kweli una miaka 20 na binti 25 nakushauri fata ushaur wa mzazi wako wa kiume.mke unaoa wewe na si mama yako mzazi na kamwe utamlea wewe na si mama yako.jipange kwanza ndoa siyo mchezo wa kuigiza
 
Kama una ndugu zako wanahitaji msaada wako hasa kuhusu Elimu bhasii usioee maana majukumu atakuzidi alafu ndugu zako wanahitaji msaada wako..!! Sio vizuri wazazi wako waanze kukopa akati wew umefanikiwaa unaweza kuwasaidia ndugu zako... Afuu umri wako badoo...ndoa si mchezoo
 
kiukweli ndoa haitaki maigizo.kama kweli una miaka 20 na binti 25 nakushauri fata ushaur wa mzazi wako wa kiume.mke unaoa wewe na si mama yako mzazi na kamwe utamlea wewe na si mama yako.jipange kwanza ndoa siyo mchezo wa kuigiza
Sio 20 miaka ya mwishoni mwa ishirini 29
 
Habari za mapumziko ya mwisho wa wiki wana Jf, ni matumaini yangu tu salama na tunaendelea na majukumu wengine na mapumziko ya mwisho wiki.

Ninakuja kwenu great thinkers mnisaidie kwa mawazo na ushauri juu ya mada jatwa "Baba hataki nioe, mama anataka nioe"

Natanguliza shukrani kwanza kwa msaada wa mawazo na ushauri toka kwenu.

Kama nilivyoeleza katika threed yangu ya kwanza humu iliyohusu "nimvumilie huyu mwanamke mpaka ndoa au nipige chini"
Nashukuru wengi walinipa mawazo na ushauri mzuri na hata sasa nimefikia maamuzi ila katika utekelezaji wake napata ugumu.

Tulipanga na mtarajiwa wangu yakuwa at least tujipange kuwasogeza wadogo zetu kielimu na mimi kujiendeleza hata nitakapo kuwa masomoni tufunge ndoa sasa uhitaji wa ndoa umekuwa wa haraka kwa mwenzangu sababu anategemea kumaliza chuo mwaka ujao( ingawa ni mwajiriwa ) ila baada ya kumaliza kuna kozi nyingine anatakiwa aende, ameleta hiyo demand na niliipokea na kama ilivyo desturi zetu za kiafrika lazima wazee wakubaliane nawe (wakupe baraka) ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa mambo ya muhimu ili kupewa mke kihalali.

Baada ya kumweleza mama, kama ilivyokawaida ya akina mama alifurahi sana na aliniunga mkono akinisihi nifanye mapema, Kwa upande wa mzee mambo yalikuwa tofauti hakuliunga mkono akidai bado umri ( am in late 20's) nawahi wapi kiufupi hakunielewa kabisa na alikataa, pia akilikumbushia swala wadogo zangu ambao wapo masomoni bado (wazazi hawaishi pamoja).

Binti naye anawasiliana na ma mkwe wake mtarajiwa, yakuwa nimempotezea muda na aliachana na mipango ya mahusiano na wengine kwa zaidi ya mwaka sasa leo namwambia bado (she is 25) anadai anakimbizana na umri wa kuzaa.

Mim nina kazi ya kudumu serikalini na binti naye ana kazi ya kudumu serikalini.

Naombeni msaada wa kutegea hiki kitendawili great thinkers wenzangu!
"Naomba kuwasilisha"
Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye....


Fuata ushauri wa baba yako au ukiona mambo yamekuwia magumu, wape muda wazazi wako wawili wajadiliane alafu baada ya hapo waje na jibu moja...hili linawezekana kabisa.
 
Mwana mwenye hekima humfurahisha babaye....


Fuata ushauri wa baba yako au ukiona mambo yamekuwia magumu, wape muda wazazi wako wawili wajadiliane alafu baada ya hapo waje na jibu moja...hili linawezekana kabisa.
Asante kwa ushauri mzuriii
 
Back
Top Bottom