Determinantor
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 61,202
- 99,941
Ni hatari sana kuwa na Baba mwenye ndimi mbili, akija kwa jirani akionana nae anasema hili, akitoka akienda kwa huyu anasema lile. Hana msimamo, sio mkweli, yeye kila siku ana kzai ya kusoma upepo unavyokwenda. Haamini anachokisema, anakazi ya kuwafurahisha watu, akiona mtanuna akija kazi yake ni kuwachekesha ili yaishe apite aendelee na yake. Ni lini baba ataacha kutuchonganisha?
Baba huyu huyu ndio alianzishaga mambo ya Udini, tena akatamka hadharani kuwa Tanzania kuna udini, mambo yalivyozidi akakana, watu wakaumizana weee, baba huyu huyu ndie aliesema Wana-jumuiya wenzake walikua hawataki Kitabu kipya cha maarifa, mambo ya sirini Baba akayatoa hadharani, hivi huku si kuchonganisha wana jumuiya? akasahau kuwa alishakaa na jirani wa kikundi fulani na akawwahidi kuwa uandishi wa kitabu ungesitishwa, Waaapi, alipotoka kakimbilia kwenda kuwaeleza kuwa "nimewaweza" nyie endeleeni tu.
Baba huyu huyu ndio anasema kura isipigwe hadi Daftari liboreshwe lakini ndani ya sentensi hio hio anasema anatakiwa kusaini ndani ndani ya siku 84, baba kachanganyikiwa hajui aende na la uandikishaji au aende na la kusaini. Maskini Baba, hivi hana washauri?
Naskia kaibuka mtoto mmoja leo, kaweka ngumu anasema lazima waototo wote wawekewe kwenye orodha kwanza, haya sasa tusubitri mapambazuko ya kesho, Baba atasemaje, je atamchapa huyu mtoto na kumfunga mdomo ili kura iwahi ndani ya siku 84 au atasoma upepo kwanza?
Baba Muombe MUNGU sana, una kipindi kigumu. MUNGU akutangulie
Baba huyu huyu ndio alianzishaga mambo ya Udini, tena akatamka hadharani kuwa Tanzania kuna udini, mambo yalivyozidi akakana, watu wakaumizana weee, baba huyu huyu ndie aliesema Wana-jumuiya wenzake walikua hawataki Kitabu kipya cha maarifa, mambo ya sirini Baba akayatoa hadharani, hivi huku si kuchonganisha wana jumuiya? akasahau kuwa alishakaa na jirani wa kikundi fulani na akawwahidi kuwa uandishi wa kitabu ungesitishwa, Waaapi, alipotoka kakimbilia kwenda kuwaeleza kuwa "nimewaweza" nyie endeleeni tu.
Baba huyu huyu ndio anasema kura isipigwe hadi Daftari liboreshwe lakini ndani ya sentensi hio hio anasema anatakiwa kusaini ndani ndani ya siku 84, baba kachanganyikiwa hajui aende na la uandikishaji au aende na la kusaini. Maskini Baba, hivi hana washauri?
Naskia kaibuka mtoto mmoja leo, kaweka ngumu anasema lazima waototo wote wawekewe kwenye orodha kwanza, haya sasa tusubitri mapambazuko ya kesho, Baba atasemaje, je atamchapa huyu mtoto na kumfunga mdomo ili kura iwahi ndani ya siku 84 au atasoma upepo kwanza?
Baba Muombe MUNGU sana, una kipindi kigumu. MUNGU akutangulie