Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,951
- 156,113
SERIKALI imetangaza kubomoa nyumba zote zilizojengwa ndani ya mita 60 kutoka usawa wa bahari ikiwa ni moja ya mkakati wa kuokoa maeneo oevu, fukwe ambazo zimevamiwa na kuilinda mikoko inayokatwa ovyo.
Mkakati huo unaendeshwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira pamoja na wizara ya Maliasili na Utalii.
Viongozi wa wizara hiyo juzi walifanya kikao kwa pamoja na kubaini kuwa fukwe nyingi nchini zimevamiwa.
Miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka, Waziri wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Teresa Huvisa, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Mazingira Dk. Robert Ntakamulnega na Zawadi Mbwambo ambaye ni Ofisa kutoka Maliasili na Utalii.
Profesa Tibaijuka baada ya mkutano huo aliliambia gazeti hili kuwa kwa kuanzia wameanza kusoma ramani za fukwe zilizoko Kawe na Mbezi na kugundua uvamizi mkubwa umefanywa na watu kujenga makazi.
Tunawaambia hawa waliojenga baharini wahame kabla ya tsunami kuwakumba, hatutakuwa na huruma na mtu, alisema Profesa Tibaijuka na kusisitiza kuwa wanafanya kzi wakiwa na Baraka za Rais Kikwete Rais ametuhakikishia kuwa hawezi kuhalalisha haramu.
Waziri huyo alisisitiza kuwa wametoa saa 48 kwa maofisa ardhi waende kwenye maeneo hayo kupiga picha za satelaiti na watawasilisha taarifa yao kwa kikao cha makatibu wakuu kitakachofanyika kesho.
Alisema kuna watu wamemilikishwa maeneo hayo kihalali kabla ya Sheria ya Mazingira ambao watafutiwa hati miliki hizo na watabomolewa nyumba zao, lakini watalipwa fidia. Kwa wale waliopatiwa vibali kinyume cha tararibu hawatalipwa fidia.
Naye Dk. Huvisa alisema mkakati huo ni kulinda mazingira nchi nzima na fukwe zote zitakazohusika ni za nchi nzima.
tunataka maeneo hayo yasiendelezwe kwani sheria ya mazingira inakataza, hizi fukwe kila mtu ana haki ya kwenda kuzuru sio baadhi ya watu wajihalalishie.
Mkakati huo unaendeshwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira pamoja na wizara ya Maliasili na Utalii.
Viongozi wa wizara hiyo juzi walifanya kikao kwa pamoja na kubaini kuwa fukwe nyingi nchini zimevamiwa.
Miongoni mwa waliohudhuria mkutano huo ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka, Waziri wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Teresa Huvisa, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Charles Kitwanga, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Mazingira Dk. Robert Ntakamulnega na Zawadi Mbwambo ambaye ni Ofisa kutoka Maliasili na Utalii.
Profesa Tibaijuka baada ya mkutano huo aliliambia gazeti hili kuwa kwa kuanzia wameanza kusoma ramani za fukwe zilizoko Kawe na Mbezi na kugundua uvamizi mkubwa umefanywa na watu kujenga makazi.
Tunawaambia hawa waliojenga baharini wahame kabla ya tsunami kuwakumba, hatutakuwa na huruma na mtu, alisema Profesa Tibaijuka na kusisitiza kuwa wanafanya kzi wakiwa na Baraka za Rais Kikwete Rais ametuhakikishia kuwa hawezi kuhalalisha haramu.
Waziri huyo alisisitiza kuwa wametoa saa 48 kwa maofisa ardhi waende kwenye maeneo hayo kupiga picha za satelaiti na watawasilisha taarifa yao kwa kikao cha makatibu wakuu kitakachofanyika kesho.
Alisema kuna watu wamemilikishwa maeneo hayo kihalali kabla ya Sheria ya Mazingira ambao watafutiwa hati miliki hizo na watabomolewa nyumba zao, lakini watalipwa fidia. Kwa wale waliopatiwa vibali kinyume cha tararibu hawatalipwa fidia.
Naye Dk. Huvisa alisema mkakati huo ni kulinda mazingira nchi nzima na fukwe zote zitakazohusika ni za nchi nzima.
tunataka maeneo hayo yasiendelezwe kwani sheria ya mazingira inakataza, hizi fukwe kila mtu ana haki ya kwenda kuzuru sio baadhi ya watu wajihalalishie.