emmanuel1976
JF-Expert Member
- Jun 17, 2011
- 301
- 80
Kutokana na nyakati tunazopitia kama taifa imenilazimu kutafakari kwa kujiuliza kuwa ni dalili gani huambatana na dola ziangukazo. Katika tafakari hiyo nimeorodhesha baadhi ya dalili hizo na pia waweza ongezea zingine kwani hizi zaweza kuwa baadhi tu.
1. Kuporomoka kwa maadili ya viongozi wa umma. (rushwa, wizi, ubadhirifu wa mali za umma).
2. Propaganda za uongo na uzushi kutiwa uhai na kuonekana kama ukweli. Hii huwafanya wananchi kudhani wanashughulikia mambo sahihi ili kupata majibu ya ukweli kumbe sivyo.
3. Kuongezeka kwa umaskini wa kipato kwa wananchi.
4. Vijana wengi kubaki mitaani pasipo ajira.
5. Viongozi wa dola wenyewe KUTOKUWA na umoja na mshikamano thabiti. Utaona wakipingana na kushambuliana kwa maneno hadharani na kwa siri. Mwana falisafa maarufu duniani Yesu Kristo aliwahi sema ufalme (taifa) ukifitinika hauwezi kusimama.
6. Kiwango cha elimu kuwa duni.
7. Viongozi wa dola hudharau viongozi wa dini na kuweka matumaini yao katika ushirikina na uchawi ama mambo yanayo fanana na hao.
8. Anasa. Hii nayo ni dalili muhimu sana kwa taifa linaloanguka. Viongozi wake hawapendi kujishughulisha kwa bidii katika kushughulikia matatizo ya jamii zao bali hutumia vibaya pesa ya umma katika anasa. Warumi walikuwa wamebobea katika kusaka anasa kwa gharama yoyote.
9. Vyombo vya dola vya ulinzi na usalama hutumika katika kuwatisha na kuwanyamazisha raia wake pale wanapodai uwajibikaji wa viongozi wao.
Ongezea dalili zingine sote tujifunze
1. Kuporomoka kwa maadili ya viongozi wa umma. (rushwa, wizi, ubadhirifu wa mali za umma).
2. Propaganda za uongo na uzushi kutiwa uhai na kuonekana kama ukweli. Hii huwafanya wananchi kudhani wanashughulikia mambo sahihi ili kupata majibu ya ukweli kumbe sivyo.
3. Kuongezeka kwa umaskini wa kipato kwa wananchi.
4. Vijana wengi kubaki mitaani pasipo ajira.
5. Viongozi wa dola wenyewe KUTOKUWA na umoja na mshikamano thabiti. Utaona wakipingana na kushambuliana kwa maneno hadharani na kwa siri. Mwana falisafa maarufu duniani Yesu Kristo aliwahi sema ufalme (taifa) ukifitinika hauwezi kusimama.
6. Kiwango cha elimu kuwa duni.
7. Viongozi wa dola hudharau viongozi wa dini na kuweka matumaini yao katika ushirikina na uchawi ama mambo yanayo fanana na hao.
8. Anasa. Hii nayo ni dalili muhimu sana kwa taifa linaloanguka. Viongozi wake hawapendi kujishughulisha kwa bidii katika kushughulikia matatizo ya jamii zao bali hutumia vibaya pesa ya umma katika anasa. Warumi walikuwa wamebobea katika kusaka anasa kwa gharama yoyote.
9. Vyombo vya dola vya ulinzi na usalama hutumika katika kuwatisha na kuwanyamazisha raia wake pale wanapodai uwajibikaji wa viongozi wao.
Ongezea dalili zingine sote tujifunze